Thursday, March 23, 2017

Katibu Mkuu Mambo ya Nje apokea vifaa vya kuendesha mikutano kwa njia ya Video


Katibu Mkuu wa  Wizara ya Mambo ya Nje  na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz P. Mlima (Kushoto) akipokea maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy wakati wa makabidhiano ya vifaa vya kuendeshea Mikutano kwa njia ya Video Wizarani Jijini Dar es Salaam tarehe 23 Machi, 2017. Makabidhiano yanakamilisha sehemu ya vifaa vilivyotolewa na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Bi. Awa Dabo ambavyo vilikabidhiwa tarehe 2 Februari, 2017 ili kuiwezesha Wizara kufanya kazi kwa ufanisi zaidi sambamba na kupunguza gharama za uendeshaji wa ofisi.
Katibu Mkuu akimpongeza Balozi Mushy kwa jitihada zake za kuimarisha mahusiano mazuri na wadau wa maendeleo sambamba na kuhakikisha shughuli za kiutendaji za Wizara zinaenda na kasi ya maendeleo ya teknolojia.
Katibu Mkuu na Balozi Mushy wakipokea maelezo kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eric Kombe kuhusu namna vifaa hivyo vinavyoweza kurahisisha Mawasiliano.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.