Wednesday, March 22, 2017

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Mabalozi Wateule nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) leo tarehe 22 Machi, 2017 amepokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Mabalozi Wateule 7 wanaowakilisha nchi zao nchini kutoka Hungary, Belarus, Guinea, Botswana, Niger, Cyprus na Bangladesh. Pichani Balozi Mahiga akipokea nakala za hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Hungary nchini, Mhe. Laszlo Eduard Mathe mwenye makazi yake Nairobi, Kenya.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akipokea nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Belarus nchini, Mhe. Dmitry Kuptel mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa na Balozi Mteule wa Guinea nchini Mhe. Sidibe Fatoumata KABA mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia mara baada ya kupokea Nakala zake za Hati za Utambulisho.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Botswana nchini, Mhe. Lebonaamang Thanda Mokalake mwenye makazi yake Lusaka, Zambia.
Waziri Mahiga akizungumza na Mhe. Mokalake mara baada ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho. Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin.
Mazungumzo yakiendelea kushoto ni Maafisa wa Ubalozi wa Botswana ambao waliambatana na Mhe. Mokalake.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Niger nchini, Mhe. Adam Maiga ZAKAKARIAOU mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. 
Waziri Mahiga akiagana na Mhe. ZAKAKARIAOU mara baada ya kuwasilisha Nakala za Utambulisho.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Cyprus nchini, Mhe. Andreas Panayiotou mwenye makazi yake Muscat, Oman.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Bangladesh nchini, Mhe. Meja Jenerali Abul Kalam Mohammad ahaumayun KABIR mwenye makazi yake Nairobi, Kenya. 
Waziri Mahiga akizungumza na Mhe. KABIR.Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin na kushoto ni Afisa kutoka Ubalozi wa Bangladesh ambaye aliambatana na Mhe. KABIR.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.