Friday, August 31, 2018




TAARIFA KWA UMMA

KUHUSU MATOKEO YA AWALI YA NAFASI ZA AJIRA KATIKA SERETARIETI YA SADC ZILIZOTANGAZWA KWA MWAKA 2018.                                            

Sekretarieti ya SADC ilitangaza nafasi 50 katika kada mbalimbali mwezi wa Mei, 2018. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utmishi wa Umma na Utawala Bora (UTUMISHI) ilitangaza nafasi hizo kupitia vyombo mbalimbali vya habari.

Wizara inapenda kuutangazia umma kuwa baada ya mchujo wa duru ya kwanza uliofanywa na Kikosi Kazi Maalum, jumla ya waombaji 141 kati ya waombaji 1,472 wamepita katika uchambuzi wa awali. Katika muktadha huo, Wizara inaweka orodha ya awali ya mchujo wa Tanzania ya waombaji waliochaguliwa katika nafasi mbalimbali pamoja na jedwali lenye kuonyesha idadi ya waombaji hao.

Wizara inapenda kuutaarifu umma na waombaji wa nafasi za ajira zilizotangazwa na SADC kuwa taarifa zaidi itatolewa na Sekretarieti ya SADC kwa wale tu watakao kuwa kwenye orodha ya mchujo wa duru ya pili (shortlisted) utakayofanywa na Sekretarieti ya SADC.

Aidha, tutakumbuka kuwa mwezi wa Mei, 2017 Sekretarieti ya SADC ilitangaza nafasi 44 ambapo zoezi la usaili wake lilikamilika mwaka huu. Kwenye nafasi 44, Tanzania imefanikiwa kupata nafasi tano za kimkakati na maafisa hao tayari wamesharipoti kwenye kituo chao cha kazi Gaborone, Botswana. Nafasi hizo zinaainishwa kama ifuatavyo:

i.    Afisa Mwandamizi anayeshughulikia masuala ya Sera na Mikakati ya Maendeleo, (Senior Officer - Policy and Strategy Development);

ii.    Afisa Mwandamizi Mipango anayeshughulikia masuala ya Viwanda na Ushindani, (Senior Programme Officer - Industrialization and Competitiveness);

iii.   Afisa Mipango anayeshughulikia masuala ya Ushuru na Utaratibu, (Programme Officer Customs and Procedures);

iv.   Afisa anayeshughulikia masuala ya Ufuatiliaji, Tathmini na utoaji wa Taarifa, (Monitoring, Evaluation and Reporting Officer); na
v.    Afisa Fedha anayeshughulikia masuala ya Hazina na Bajeti, (Finance Officer - Treasury and Budget )

Tunawapongeza kwa dhati wote waliochaguliwa na kufanikiwa kuingia kwenye orodha ya mchujo wa awali uliofanyika Tanzania kwa mwaka 2018.  
Aidha, kwa aina ya pekee, tunawapongeza maafisa waliochaguliwa kwenye nafasi tano (5) zilizotajwa na tunawatakia kila la heri katika majukumu yao mapya sambamba na kuwasihi daima kukumbuka kuwa wanaliwakilisha Taifa letu kwenye nafasi hizo.
Mwisho, Wizara inapenda kutaarifu kuwa itaendelea kuzitangaza fursa kama hizi zitapojitokeza kupitia SADC na Jumuiya zingine za Kikanda na Kimataifa ambazo Tanzania ni nchi mwanachama, kwa manufaa ya watanzania wote. Hivyo, tunawaomba Watanzania wasikate tamaa na wasisite kuwasilisha maombi ya ajira kama hizi pale fursa zinapojitokeza.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam,
27 Julai, 2018



LIST OF APPLICANTS FOR JOB POSTS ADVERTISED BY SADC SECRETARIAT

1. SENIOR LEGAL COUNSEL

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
John Nzunda
Senior Legal Counsel
2
Kitandu Paulo Ugula
Senior Legal Counsel
3
Phines Leonard Matto
Senior Legal Counsel
4
Edson Rwechungura
Senior Legal Counsel



2. HEAD CIVILIAN

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Naomi Z. Mpemba
Head Civilian
2
Josey Stephen Mwakasyuka
Head Civilian
3
Minja Tumaini Anthony
Head Civilian



 3. SENIOR OFFICER- DISSASTER RISK REDUCTION

S/N
NAME
POST APPLIED               
1.
Dismas Laurean Mwikila
Senior Officer- Dissaster Risk Reduction Grade-7
2
Alfei Daniel
Senior Officer- Dissaster Risk Reduction Grade-7
3
Danford E. Manyema
Senior Officer- Dissaster Risk Reduction Grade-7
4
Egidius D. Nyetabula
Senior Officer- Dissaster Risk Reduction Grade-7


 4. SENIOR PROGRAMME OFFICER HEALTH AND NUTRITION

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Rehema Idriss Mzimbiri
Senior Programme Officer Health and Nutrition
2
Dr. Dominic Franklin Mosha
Senior Programme  Officer Health and Nutrition 
3
Dr. Janet Mwambona
Senior Programme  Officer Health and Nutrition 
4
Coline Mahende
Senior Programme  Officer Health and Nutrition 


 5.SENIOR OFFICER INTERNAL AUDIT

S/N
NAME
POST APPLIED           
1.
Noah Mgana

Senior Internal Auditor
2
UphooSwai
Senior Internal Auditor

6.SENIOR OFFICER – ICT- GRADE 4

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Alex David Mhagama
Senior Officer - ICT
2
Elizabeth Sylvester Mkoba
Senior Officer - ICT
3
Joan K. Rwegalulira
Senior Officer - ICT
4
Keneth L. Mlelwa
Senior Officer - ICT

7. SENIOR OFFICER LEARNING, DEVELOPMENT AND PERFORMANCE MANAGEMENT

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Denis KigoiMbaga
Senior Officer-Learning Development and Performance Management
2
SakinaB.Mwinyimkuu
Senior Officer-Learning Development and Performance Management
3
Josephine RogateKimaro
Senior Officer-Learning Development and Performance Management
4
Ahmada Suleiman
Senior Officer-Learning Development and Performance Management


 8.SENIOR OFFICER ADMINISTRATION

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Lilian Amri
Senior  Officer Administration
2
Anicia Ng’weshemi
Senior  Officer Administration
3
Dr. Edith M. Rwiza
Senior  Officer Administration
4
Devine Mbuya
Senior  Officer Administration

 9.SENIOR OFFICER RESEARCH AND STATISTICS

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
AbdallahAthumani Mhagama
Senior Officer Research and Statistics
2
William H Matee
Senior Officer Research and Statistics
3
Zakayo Elisa Msokwa
Senior Officer Research and Statistics
4
Bahati Marcel Ilembo
Senior Officer Research and Statistics


 10.SENIOR PROGRAMME OFFICER EDUCATION SKILLS AND DEVELOPMENT




S/N
NAME
POST APPLIED
1
Samson M. Bishati
Senior Programme Officer Education and Skills Development
2
Dkt. Elia Y.K. Kibga
Senior Programme Officer Education and Skills Development
3
Maria T. Mdachi
Senior Programme Officer Education and Skills Development

11.SENIOR PROGRAMME OFFICER WATER

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
John S. Msengi
Senior  Progamme Officer Water
2
Omari R. Mwinjaka
Senior  Progamme Officer Water
3
Mwanamkuu Mwanyika
Senior  Progamme Officer Water
4
Aron Swai
Senior  Progamme Officer Water

12. SENIOR PROGRAMME OFFICER FOOD SECURITY AND AGRICULTURE

S/N
NAME
POST APPLIED            
1
TheophordCosmasNdunguru
Programme Officer Food Security and Agriculture
2
AbeidMsangi
Programme Officer Food Security and Agriculture
3
DeagratiusNshoroLwezaura
Programme Officer Food Security and Agriculture
4
Joseph William Maziku
Programme Officer Food Security and Agriculture


S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Sayumwe Jasson Yotham
Senior Programme Officer - ICT
2
Cecil Nkomola Francis
Senior Programme Officer - ICT
3
Engelbert Linus Chuwa
Senior Programme Officer - ICT
4
Magori Alphonce
Senior Programme Officer - ICT


 14. SENIOR PROGRAMME OFFICER MACROECONOMIC CONVERGENCE 

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Juvenal Lema
Senior Programme Officer Macroeconomic Convergence
2
Michael Kadebe
Senior Programme Officer Macroeconomic Convergence
3
Allan SyrilMhula
Senior Programme Officer Macroeconomic Convergence


 15.  SENIOR PROGRAMME OFFICER SCIENCE TECHNOLOGY AND INNOVATION

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Kenneth Longo Mlelwa
Senior Programme Officer Science Technology and Innovation
2
Maskat Erick Mliwanga
Senior Programme Officer Science Technology and Innovation
3
SayuniMbwilo
Senior Programme Officer Science Technology and Innovation

16. AUC LIAISON SENIOR OFFICER

S/N
NAME
POST APPLIED             
1
Benedict Theresia Msuya
AUC Liaison Senior Officer
2
Eustace Damian Lubuva
AUC Liaison Senior Officer
3
Jossey Stephen Mwakasyuka
AUC Liaison Senior Officer
4
Jacob Joachim Lisakafu
AUC Liaison Senior Officer


 17. SENIOR PROGRAMME OFFICER -INVESTMENT AND FINANCE

S/N
NAME
POST APPLIED     
1
KabulaIreneMulihano
Senior Programme Officer -Investment And Finance


18. SENIOR OFFICER RENUMERATION, RECRUITMENT AND RELATIONS

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Edith Martin Rwiza
Senior Officer Renumeration, Recruitment and Relations
2
Denis KigoiMbaga
Senior Officer Renumeration, Recruitment and Relations
3
Neema Mourice Mhagama
Senior Officer Renumeration, Recruitment and Relations
4
Justine  S Rumanyika
Senior Officer Renumeration, Recruitment and Relations

19.SENIOR PROGRAMME OFFICER TRADE

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
James HeriMackav
Senior Programme Officer Trade
2
Aneth Eli Simwela
Senior Programme Officer Trade
3
MguneMasatuMgune
Senior Programme Officer Trade


 20. SENIOR PROGRAMME OFFICER EX-SITU CONSERVATION (SPGRC)

S/N
Name
Post Applied            
Comments
1
LouranceNjopilaiMapunda
Senior Programme Officer Exisitu Conservation Sadc Plants Genetic Resource Centre (Spgrc)

2
MujuniSospeterKabululu
Senior Programme Officer Exisitu Conservation SadcPlants Genetic Resource Centre (Spgrc)

3
VettesKalema
Senior Programme Officer Exisitu Conservation Sadc Plants Genetic Resource Centre (Spgrc


21. FINANCE OFFICER – PROJECT AUDITS AND COMPLIANCE

S/N
NAME
POST APPLIED
1.
Samwel John
Finance Officer Projects Audits and Compliance
2
Mkufya H. Matope
Finance Officer Projects Audits and Compliance
3
Neema S. Umbellah Beda
Finance Officer Projects Audits and Compliance
4.
Kauthar  Othman
Finance Officer Projects Audits and Compliance

22. OFFICER RESEARCH AND STATISTICS

S/N
NAME
POST APPLIED        
1
Shadrack Elia Kibona
Officer Research And Statistics
2
Mohamed Mbwana Mlanzi
Officer Research And Statistics
3
Suleiman Follogo Biki
Officer Research And Statistics
4
Christopher Onesmo Sanga
Officer Research And Statistics

23.PROGRAMME OFFICER HIV AND AIDS

S/N
NAME
POST APPLIED       
1.
Dr. Majaliwa Gerald Marwa
Programme Officer Hiv And Aids

2
JaivingChapaulinjiKazitanga
Programme Officer HIV and Aids
3
Siril Michael Kullaya
Programme Officer HIV and Aids
4
Yahaya Musa Mmbaga
Programme Officer HIV and Aids

24. PROGRAMME OFFICER GENDER MAINSTREAMING

S/N
NAME
POST APPLIED       
1
LucasKisimboMkwizu
Programme Officer Gender Mainstreaming
2
DorahG.Neema
Programme Officer Gender Mainstreaming
3
MwajumaLugendo
Programme Officer Gender Mainstreaming
4
JovinFaustineMwehozi
Programme Officer Gender Mainstreaming


No.
NAMES AND CONTACT
POST APPLIED
1
Nickson Jackson
P.O Box 90180 DSM
Mobile  0713899042    
Internal Auditor
2
Grace SangiwaSimba
P.O Box 3163  Dar es Salaam
Mobile  0717810950   E-mail:              
Internal Auditor
3
AmnonMwasakatili
P.O Box 9080 Dar es Salaam
Mobile  0768631776  
Internal Auditor
4
WaziriShabani
P.O Box 174 Mwanza
Mobile  0717112689  
E-mail: waziri.shabani@gmail.com
Internal Auditor
























26. IT SUPPORT OFFICER – SADC REGIONAL PEACEKEEPING \
TRAINING CENTRE (RPTC) (HARARE, ZIMBABWE) – GRADE 6

S/N
NAME
POST APPLIED          
1
Boniphace Peter Mtakwa
IT Support Officer 
2
Adam Pharouk Musa
IT Support Officer
3
Geofrey Bukuku Mwakijungu
IT Support Officer
4
Lina Rujweka
IT Support Officer

27. LIAISON OFFICER DISASTER RISK REDUCTION

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Lawrence Mtui
Liaison Officer Disaster Risk Reduction 
2
Alfei Daniel
Liaison Officer Disaster Risk Reduction 
3
Masoud Makame Faki
Liaison Officer Disaster Risk Reduction 
4
Jacqueline Colleta Dominic Mwakanga
Liaison Officer Disaster Risk Reduction 

 28.ELECTIONS AND GOOD GOVERNANCE OFFICER

S/N
NAME
POST APPLIED
1
Dr. Victor Rugumamu
Election and Good Governance Officer
2
Raymond Maro
Election and Good Governance Officer
3
Ahmed Nyang’anyi
Election and Good Governance Officer
4
Msemo S. Mavare
Election and Good Governance Officer

29.MEDIATION AND PEACE BUILDING OFFICER 

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Thomas C. Munzerere
Mediation and Peace Building Officer 

2
Paul J. Makelele
Mediation and Peace Building Officer 
3
Zulekha Fundi
Mediation and Peace Building Officer 
4
Evance Siangicha
Mediation and Peace Building Officer 

30.OFFICER –LOGISTICS 

S/N
NAME
POST APPLIED
1
Joan Thobias
Officer –logistics 
2
Stephen Mayani
Officer –logistics 
3
Ngumoi Laizer
Officer –logistics 
4
Justine Selekwa
Officer –logistics 


31. OPERATION AND PLAN OFFICER

S/N
NAME
POST APPLIED     
1
Idrissa HashimMajamba
Operation and Plan Officer

32.PLANNING AND BUDGET SUPPORT OFFICER X 2

S/N
NAME
POST APPLIED  
1.
Juvenal D. Lema
Planning And Budget Support Officer X 2
2
Joseph NingisigweKatamba
Planning And Budget Support Officer X 2
3
Nicodemus T. Massao
Planning And Budget Support Officer X 2
4
Martin MlingoSapanjo
Planning And Budget Support Officer X 2


33.PROGRAMME OFFICER SQAM

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Happy Brown Kanyeka
Programe Officer SQAM
2
Safari Fungo
Programe Officer SQAM
3
Bhoke John Rotente
Programe Officer SQAM



34.PROGRAMME OFFICER CUSTOMS CAPACITY BUILDING

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
January S. Qamana
Programme Officer Customs Capacity Building
2
Ambrose A. Bahati
Programme Officer Customs Capacity Building
3
Semainda G. Mhina
Programme Officer Customs Capacity Building


35.PROGRAMME OFFICER CAPITAL MARKETS

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Patrick Gondwe
Programme Officer Capital Markets
2
Fidelis Mkatte
Programme Officer Capital Markets


36.PROGRAMME OFFICER FINANCIAL SECTOR

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Mahyono Rashid
Programme Officer Financial Sector
2
Fredrick Romani
Programme Officer Financial Sector
3
John Madaba
Programme Officer Financial Sector
4
Eliamlisi Joseph Mlay
Programme Officer Financial Sector


 37. PROGRAMME OFFICER INVESTIMENT

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Annamaria Mwamyalla
Programme Officer Investment
2
Lilian Maua Mwamdanga
Programme Officer -Investment
3
MeshackJoramAnyingisye
Programme Officer -Investment


38. PROGRAMME OFFICE REGIONAL TRADE
S/N
NAME
POST APPLIED         
1.    
FelistaS.Rugambwa
Officer Resource Mobilization X2
2.    
Alphonce N. Mayala
Officer Resource Mobilization X2
3.    
Said R. Nyenge
Officer Resource Mobilization X2







S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Viola Sawere
Programme Officer Regional Trade
2
Mosses Lufuke
Programme Officer Regional Trade
3
Mussa Martine
Programme Officer Regional Trade

39. PUBLIC SECURITY OFFICER

S/N
NAME
POST APPLIED               
1
Joseph Musuguri
Public Security Officer
2
Daniel Masasi
Public Security Officer
3
Kichere Chacha Mwita
Public Security Officer

40.OFFICER RESOURCE MOBILIZATION X2

S/N
NAME
POST APPLIED    
1
Justine Mdamila
Human Resource Officer
2
Mary William Minja
Human Resource Officer
3
AminathaSirajuKaboyonga
Human Resource Officer

Thursday, August 30, 2018

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.







TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KUHUSU MKUTANO WA JUKWAA LA USHIRIKIANO KATI YA CHINA NA AFRIKA (FOCAC)

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya Afrika na China (FOCAC) utafanyika Beijing kuanzia tarehe 01 hadi 04 Septemba, 2018.

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo utaongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa. Viongozi wengine watakaoshiriki Mkutano huo ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga; Mhe. Khalid Salum Mohamed, Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mhe. Rashid Ali Juma, Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, na Viongozi wengine Waandamizi.

Mkutano huo utafunguliwa na Rais wa China, Mhe. Xi Jinping ambaye pia ni Mwenyekiti wa jukwaa hilo, kwa kushirikiana na Mwenyekiti Mwenza, Rais wa Afrika Kusini, Mhe. Matamela Cyril Ramaphosa, utahudhuriwa pia na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika ambaye pia ni Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mhe. Antonio Guterres na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Afrika ambaye pia ni Rais wa Chad, Mhe. Idriss Deby Itino. Mkutano huo pia utashuhudia uchaguzi wa Mwenyekiti Mwenza mpya kutoka Afrika.

Kaulimbiu ya Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika kwa mwaka 2018 ni “China na Afrika: Kuelekea Jumuiya Imara kwa mustakabali wa wote kupitia ushirikiano kwa manufaa ya wote” (China and Africa: Toward an Even Stronger Community with a Shared Future through Win-Win Co-operation).

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali utatanguliwa na kikao cha Makatibu Wakuu kitakachofanyika tarehe 01 Septemba, 2018. Kikao hicho pamoja na mambo mengine kitapitia agenda za mkutano huo na kuziwasilisha kwenye kikao cha Mawaziri kitakachofanyika tarehe 02 Septemba, 2018.

Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano kati Afrika na China pamoja na mambo mengine utajadili namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya Afrika na China na kufanya mapitio ya mikakati ya pamoja ya maendeleo iliyopo kati ya Afrika na China. Jukwaa hilo ambalo lilianzishwa mwaka 2000 huwaleta pamoja viongozi wa Afrika na China kujadili masuala ya ushirikiano na maendeleo na kutathmini utekelezaji wa makubaliano mbalimbali yanayofikiwa kati yao.

Aidha, masuala ya ushirikiano katika uendelezaji Miundombinu kama Barabara, Reli, Bandari na upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa Bara la Afrika yatajadiliwa kwa kina. Agenda nyingine itahusu kilimo cha kisasa ambapo China itatoa uzoefu wake katika kutumia sayansi na ubunifu wa kiteknolojia katika kufikia uzalishaji wenye tija na kuongeza thamani kwa mazao ili kuwa na soko la uhakika.

FOCAC 2018 pia itajadili masuala ya biashara na uwekezaji ambapo kwa kuona umuhimu huo, Mhe. Xi Jinping, Rais wa China atafungua rasmi Mkutano wa Jukwaa la Biashara kati ya China na Afrika utakaofanyika tarehe 03 Septemba, 2018.

Mkutano wa kwanza wa Wakuu wa Nchi wa Jukwaa hili ulifanyika Beijing mwaka 2006 na Mkutano wa Pili ulifanyika nchini nchini Afrika Kusini mwaka 2015.

Wakati wa Mkutano wa pili, China ilitangaza mpango kabambe wa kuhamasisha mapinduzi ya viwanda na kilimo cha kisasa kwa Afrika wenye gharama ya Dola za Marekani bilioni 60 katika utekelezaji wake. Kufuatia ushirikiano kupitia Jukwaa hilo biashara kati ya China na Afrika imeongezeka pamoja na ongezeko la ushirikiano wa kiutamaduni na biashara baina ya watu wa China na Afrika.

Pembezoni mwa Mkutano huo, Tanzania na China zimeandaa Kongamano la Biashara ambalo litafunguliwa rasmi na Mhe. Waziri Mkuu tarehe 02 Septemba, 2018. Kongamano hilo ambalo litajadili kwa kina masuala ya uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na China litashirikisha takribani makampuni 80 kutoka nchi hizi mbili.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dodoma.
30 Agosti 2018

Wednesday, August 29, 2018

TAMASHA LA KWANZA LA MICHEZO LA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI LAFIKIA TAMATI


Bw. Addo Komba Afisa kutoka Wizara ya Habari, Sanaa na Michezo, akikabidhiwa kombe kufuatia ushindi timu ya mpira wa miguu ya Wanawake ya Tanzania kwenye Tamasha la Michezo la Afrika Mashariki lililofanyika Bujumbura, Burundi.

Tamasha la Kwanza la Michezo la Jumuiya ya Afrika Mashariki lililokuwa likifanyika jijini Bujumbura limefikia tamati leo tarehe 29 Septemba, 2018. Hafla ya kufunga tamasha hilo ilihudhuriwa na Viongozi waandamizi wa Serikali kutoka nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya nchini Burundi.

Akizungumza katika hafla hiyo Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Bw. Liberatus Mfumukeko alisema maadhimisho  ya tamasha hilo yameleta tija kubwa katika kuleta na kuimarisha umoja na shirikiano, kuibua na kuendeleza vipaji mbalimbali vya wananchi wa Afrika Mashariki.

Mhe. Sindimwo Gaston Makamu wa Kwanza wa Rais wa Burundi, kwa upande wake amesema ni fahari kubwa kwa Burundi kuandaa tamasha hilo lililofanyika kwa kipindi cha wiki mbili. Aliongeza kusema washiriki wa wamichezo hiyo watakuwa mabalozi wa kuelezea sifa nzuri za amani na utulivu ulipo nchini Burundi tofauti na inavyosemwa na baadhi ya watu.

Katika tamasha hilo Tanzania imeshinda kombe moja la mpira wa miguu wa wanawake ,medali ya fedha katika riadha, mpira wa pete na karatee.

Tamasha hili lilifanyika kuanzia tarehe 16 hadi 29 Agosti 2018, katika Jiji la Bujumbura na Gitega nchini Burundi.

Kikundi cha ngoma ya asili ya nchini Burundi kikisherehesha kwenye hafla ya kufunga Tamasha la  Michezo la Afrika Mashariki.

Bw. Liberatus Mfumukeko Katibu Mkuu wa  Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (kulia) akikabidhi kombe kwa mkuu wa msafara wa Uganda.

Bw. Liberatus Mfumukeko Katibu Mkuu wa  Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki akizungumza katika sherehe za kufunga Tamasha la Michezo la Afrika Mashariki
Wachezaji wa timu ya wanawake ya mpira wa miguu Tanzania wakionyesha furaha yao ya kupata kombe baada ya kuibuka washindi katika mchezo huo kwenye Tamasha la Michezo la Afika Mashariki



Monday, August 27, 2018

Makamu wa Rais ashiriki sherehe za kuapishwa Majaji wapya wa Mahakama ya Afrika

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Majaji wapya wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ambao wameapishwa jijini Arusha. Kutoka kushoto ni Mhe. Jaji Amani Aboud (Tanzania), Mhe.Jaji Blaise Tchikaye (Congo) na kulia ni Mhe. Jaji Stella Isibhakhonem Anukam (Nigeria) 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa hafla ya kuapishwa kwa majaji wapya watatu wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu jijini Arusha.


Viongozi Mablimbali wa Serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (wa pili kulia) wakimsiliza  Mhe. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akihutubia kwenye hafla ya kuapishwa majaji watatu wapya wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu jijini Arusha. 
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia hotuba ya Mhe. Samiha Suluhu Hassan 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi kutoka kwa  Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Sylvain Ore mara baada ya kuapishwa kwa Majaji wapya watatu wa mahakama hiyo jijini Arusha.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akimpongeza Mhe. Jaji Stella Isibhakhonem Anukam (Nigeria) mara baada ya kuapishwa
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bibi Caroline Chipeta akisalimiana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk Adelardus Kilangi katikati ni Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Wilbroad Kayombo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samiha Suluhu Hassan na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), wakiwa kwenye picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu jijini Arusha. 























Saturday, August 25, 2018

Tanzania yajitwalia medali za dhahabu katika Tamasha la Michezo la Afrika Mashariki



Timu za mpira wa miguu za Wanawake  ya Tanzania (waliovalia jezi nyeupe) na Burundi wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya kuanza kwa mechi ya marudiano iliyofanyika katika uwanja wa Gitega, Burundi. Katika mpambano huo  wa Tamasha la Michezo la Afrika Mashariki linaloendelea nchini humo Tanzania imeibuka na ushindi wa goli 5-0 dhidi  ya Burundi.

Aidha, Tamasha la Michezo la Afrika Mashariki katika kipengele cha mpira wa miguu limekamilisha ratiba kwa mpambano kati ya Tanzania na Burundi, ambapo Tanzania imejishindia medali ya dhahabu kufuatia ushidi ilioupata. Burundi imejitwalia medali ya fedha kwa kushika nafasi ya pili katika mchezo huo.

Katika mchezo wa awali Tanzania iliibuka na ushindi wa goli 8-1 dhidi ya wenyeji wa tamasha Burundi.
 
Timu ya mpira wa miguu ya Wanawake ya Tanzania ikishangilia ushindi wa medali za dhahabu kufuatia ushindi  wa goli 5-0 ilioupata dhidi ya Burundi katika Tamasha la Michezo la Afrika Mashariki

Sehemu ya mashabiki wakishangilia mchezo uliokuwa ukiendelea kati ya Tanzania na Burundi
Mmoja wa wachezaji wa timu ya Tanzania akipongezwa na Bw. Addo Komba Afisa kutoka Wizara ya Habari, Sanaa na Michezo mara baada ya kuvishwa medali ya dhahabu

Picha na Matukio ya Mpira pete

Timu ya mpira wa pete ya Tanzania ikiwa tayari kwa mchuano dhidi ya Uganda kwenye Tamasha la Michezo la Afrika Mashariki. Katika mchuano huo Uganda iliibuka na ushindi wa goli 53-33 dhidi ya Tanzania.

Katika mchezo wa awali Tanzania iliibuka na ushindi mnono wa goli 79-14 dhidi ya wenyeji wa mashindano Burundi.
Wachezaji wa timu ya Tanzania (waliovalia jezi rangi ya waridi) wakijaribu kuzuia moja ya shambulio lililofanywa na timu pinzani ya Uganda
Mchezo wa mpira wa pete kati ya Tanzania na Uganda ukiendelea

Mshambuliaji wa timu ya Tanzania akilekeza mashambulizi kwa timu pinzani ya Uganda kwenye moja ya pambano la Tamasha la Michezo la Afrika Mashariki.

Friday, August 24, 2018

Waziri Mahiga amuaga Balozi wa Ubelgiji nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), akizungumza kwenye hafla ya kumuaga Balozi wa Ubelgiji aliyemaliza muda wa kuiwakilisha nchi yake hapa Tanzania Mhe. Paul Cartier (wa tatu kutoka kulia). Dkt. Mahiga alitumia fursa hiyo kumpongeza kwa kuiwakilisha nchi yake vyema hapa Tanzania. Hafla hiyo imehudhuriwa pia na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani), Kaimu Mkurugenzi Idara ya  Ulaya na Amerika, Bw.Jestas  Nyamanga na baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Hyatt Regency  jijini Dar es Salaam.
Balozi Paul Cartier naye alipata fursa ya kuishukuru Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, kwa ushirikiano aliokuwa akipata kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 
Mhe. Mwakyembe akisikiliza hotuba zilizokuwa zikitolewa na Dkt, Mahiga pamoja na Mhe.Cartier
Dkt. Mahiga akimkabidhi Balozi Cartier zawadi yenye mchoro wa Hifadhi ya  Mlima Kilimanjaro kama ukumbusho wa moja ya vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania
Waziri Mahiga (katikati), Balozi Cartier (wa nne kutoka kulia), Waziri Mwakyembe (wa tatu kutoka kulia), Bw. Nyamanga (wa tatu kutoka kushoto), Mke wa Balozi Cartier (wa nne kutoka kushoto) pamoja na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja.