Wednesday, January 23, 2019

Balozi wa Tanzania, Ujerumani awasilisha hati za utambulisho nchini Bulgaria

Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani ambaye anawakilisha pia nchini Bulgaria , Mhe. Dkt. Abdallah Posi akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Bulgaria, Mhe. Rumen Radev. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu ya nchi hiyo hivi karibuni.
Mhe. Balozi Dkt. Posi akizungumza na Mhe. Rais Radev mara baada ya kuwasilisha hati za utambulisho
Mhe. Balozi Dkt. Posi akiagana na Mhe. Rais Radev mara baada ya kuwasilisha hati za utambulisho


Mhe. Balozi Dkt. Posi akiwa mbele ya gwaride la heshima alipowasili Ikulu ya Bulgaria kwa ajili ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais wa nchi hiyo.

Thursday, January 17, 2019

Tanzania kushiriki Maonesho ya Biashara ya Dunia ya EXPO 2020


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania kushiriki Maonesho ya Biashara ya Dunia ya EXPO 2020

Tanzania itashiriki Maonesho ya Dunia ya Biashara (Expo 2020 yatakayofanyika Dubai kuanzia mwezi Oktoba 2020 na kumalizika mwezi April 2021.

Uwekaji saini wa Mkataba wa ushiriki wa Tanzania katika Maonesho hayo ulifanywa tarehe 16 Januari 2019 na Balozi wa Tanzania nchini UAE ambaye pia ni Kamishna Mkuu wa Tanzania wa DUBAI EXPO 2020, Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk.

Kwa upande wa UAE, mkataba huo uliwekwa saini na Mkurugenzi wa DUBAI EXPO 2020, Mhe. Najeeb Mohammed Al Ali.

Baada ya uwekaji saini wa Mkataba huo, Mhe. Balozi Mbarouk alieleza kuwa Serikali inayapa umuhimu mkubwa maonesho hayo kwa kuwa ni fursa adhimu ya kuitangaza Tanzania kwenye sekta za uwekezaji, biashara, viwanda, utalii na mila na utamaduni.

Aidha, Mkurugenzi wa DUBAI EXPO 2020 alieleza kuwa amefurahishwa na hatua ya Tanzania kusaini Mkataba huo ambapo itatoa fursa kwa nchi kujiandaa mapema na taratibu nyingine za ushiriki.

Baada ya uwekaji saini wa Mkataba huo,` kitakachofuata ni utayarishaji wa simulizi ya maudhui ya maonesho (pitch story) ambayo inatakiwa kuthibitishwa na Kamati ya Kitaifa ya Tanzania ya DUBAI Expo 2020. Simulizi ya maudhui hayo yatahusu vipaumbele vya Tanzania kama vile maendeleo ya viwanda, miundombinu, masuala ya biashara na uwekezaji, utalii, kilimo, elimu, afya, sanaa na utamaduni.  Simulizi ya maudhui pia itatumika katika kusanifu muonekana wa banda la maonesho la Tanzania.

Tanzania inakuwa miongozi mwa nchi washiriki zipatazo 100 ambazo tayari zimesaini Mkataba wa Ushiriki tangu Dubai ilipochaguliwa kuwa mwenyeji wa maonensho hayo.

Wengine walioshuhudia uwekaji saini wa Mkataba huo ni Bw. Ali Jabir Mwadini, Kansela Mkuu, Ubalozi Mdogo wa Tanzania, Dubai; Bi Samira Ahmed Diria, Afisa Ubalozi; na kwa upande wa DUBAI EXPO 2020 ni  Bi Manuela Garcia Pascual, Mkurugenzi wa Washiriki wa Kimataifa na Bi. Esther Omondi, Meneja wa Nchi/Afisa dawati la Tanzania.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
17 Januari 2019

Balozi wa Tanzania nchini UAE ambaye pia ni Kamishna Mkuu wa Tanzania wa DUBAI EXPO 2020, Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk (kushoto) na Mkurugenzi wa DUBAI EXPO 2020, Mhe. Najeeb Mohammed Al Ali wakiweka saini Mkataba wa ushiriki wa Tanzania katika Maonesho ya Biashara ya Dunia (Dubai Expo 2020. Uwekaji saini huo ulifanyika Dubai tarehe 16 Januari 2019.  
Balozi wa Tanzania nchini UAE ambaye pia ni Kamishna Mkuu wa Tanzania wa DUBAI EXPO 2020, Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk (kushoto) na Mkurugenzi wa DUBAI EXPO 2020, Mhe. Najeeb Mohammed Al Ali wakionesha Mkataba mara baada ya zoezi la kuweka saini kukamilika.
Balozi wa Tanzania nchini UAE ambaye pia ni Kamishna Mkuu wa Tanzania wa DUBAI EXPO 2020, Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk (kushoto) na Mkurugenzi wa DUBAI EXPO 2020, Mhe. Najeeb Mohammed Al Ali wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa wao.

Balozi wa Tanzania nchini UAE ambaye pia ni Kamishna Mkuu wa Tanzania wa DUBAI EXPO 2020, Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk (kushoto) na Mkurugenzi wa DUBAI EXPO 2020, Mhe. Najeeb Mohammed Al Ali wakibadilishana mawazo mara baada ya zoezi la kuweka saini kukamilika.

Wednesday, January 16, 2019

DKT. NDUMBARO ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO UBALOZI WA NIGERIA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Nigeria hapa nchini kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa sita wa nchi hiyo Mhe. Alhaji Shehu Shagari kilichotokea tarehe 28 Desemba 2019. Dkt. Ndumbaro alipata fursa ya kufanya mazungumzo na Balozi wa Nigeria hapa nchini Mhe. Dkt.Sahabi Isa Gada. Tukio hilo limefanyika jijini Dar Es Salaam katika Ubalozi wa Nigeria hapa nchini.  
Balozi Gada akimwelezea jambo Dkt. Ndumbaro wakati wa mazungumzo.
Sehemy ya Maafisa wa Ubalozi wa Nigeria nchini wakisikiliza kwa makini mazungumzo kati Dkt. Ndumbaro na Balozi Gada (hawapa pichani).
Dkt. Ndumbaro akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Gada na maafisa wa Ubalozi huo.
Dkt. Ndumbaro akiagana na Balozi Dkt. Gada. 





Balozi wa Italia atembelea Wizara ya Mambo ya Nje


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Italia hapa nchini Mhe. Roberto Mengoni. Wawili hao walijadiliana umuhimu wa kuibua maeneo mapya ya Ushirikiano baina ya Tanzania na Italia hussusan katika sekta ya biashara na uwekezaji.  Dkt. Mahiga alitumia fursa hiyo pia kueleza juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya awamu ya tano za kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini.
Balozi Mengoni akimwelezea jambo Dkt. Mahiga


Katibu wa Mhe. Waziri, Bw. Magabilo Murobi pamoja na Bi Happyness Lwangisa wakifuatilia na kunukuu mambo muhimu ya mazungumzo hayo.

Dkt. Mahiga akagua ujenzi wa ofisi ya Wizara Ihumwa, Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akiweka saini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye eneo linalojengwa jengo la ofisi ya Wizara Ihumwa, Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la ofisi ya Wizara Ihumwa Dodoma. Mhe. Waziri alielezwa kuwa ujenzi huo unaenda katika kasi inayoridhisha ambapo wakandarasi wapo mbele ya mpangoa kazi.

Waziri Mahiga na Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Hamid Mbegu wakioneshana alama za mipaka ya kiwanja cha Wizara.

Waziri Mahiga akiendelea na ukaguzi wa jengo la ofisi ya Wizara.
Waziri Mahiga akitoa maelekezo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Hamid Mbegu 

Watanzania 70 wahitimu Chuo Kikuu cha Galgotias nchini India


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Watanzania 70 wahitimu Chuo Kikuu cha Galgotias nchini India

Watanzania zaidi ya 70 wakiwemo wawili wa shahada ya uzamivu wamehitumu masomo yao katika Chuo Kikuu cha Galgotias nchini India katika fani mbalimbali tarehe 14 Januari 2019.

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika mahafali ya nne ya chuo hicho aliwatunuku vyeti wanafunzi hao na wengine kutoka nchi mbalimbali duniani na kuwasihi  kutumia ujuzi walioupata kuchangia kikamilifu maendeleo ya nchi walizotoka.

‘Ulimwengu unasubiri uongozi mpya na mawazo mapya na kanuni na miiko madhubuti kutoka kwenu. Hivyo, kifanyeni chuo kijivune kupitia kwenu kwa kutoa michango yenye tija katika mataifa na jamii zenu, hususan kwa kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na uadilifu mkubwa katika kutimiza majukumu yenu', Balozi Luvanda alisema.

Balozi Luvanda alisema kuwa wanafunzi hao wanahitimu huku dunia ikishuhudia mapinduzi ya teknolojia mbalimbali zikiwemo za kidigitali, teknolojia ya matumizi ya sarafu za kidigitali (block chain), matumizi ya kiwango kikubwa cha data katika kufanya maamuzi (big data revolution), usalama wa mitandao (cybersecurity) na matumzi ya teknolojia katika kutekeleza kazi ambazo awali zilikuwa zinafanywa na mwanadamu (artificial intelligence). Alielezea matumaini yake kuwa chuo hicho kitakuwa kimewandaa vyema wahitimu hao  kukabiliana na changamoto za mapinduzi ya teknolojia katika kutekeleza majukumu yao.

Mhe. Balozi alihitimisha hotuba yake kwa kuwasihi wahitimu hao kuwa, kutunukiwa vyeti sio mwisho wa kujifunza. Wanatakiwa waendelee kusoma vitabu kwa kuwa kusoma vitabu ni sawa na kuufanyia matengenzo ubungo. ‘Akili ya mwanadamu ni kama bustani, bustani isipomwagiwa maji na kupaliliwa itaota magugu na kufa kabisa.   Mhe. Balozi alimaliza.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
16 Januari 2019

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Chuo Kikuu Galgotias kutunukuu vyeti kwa wahitimu wa chuo.
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akitoa heshima katika picha ya Mahatma Gandhi kwa kuweka shada la maua.
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akitoa hotuba katika mahafali ya nne ya Chuo Kikuu cha Galgotias

Umati wa wahitimu wa chuo kikuu cha Galgotias
wakisikiliza kwa makini hotuba ya Balozi Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda.
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akipokea memento kutoka kwa mwanzilishi na mkuu wa chuo kikuu cha  Galgotias, Bw. Suneel Galgotia.






Tuesday, January 15, 2019

Dkt. Ndumbaro akutana na Mwakilishi wa UNHCR

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.), amekuatana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la kutetea wakimbizi la Umoja wa Mataifa Tanzania UNHCR, Chansa Kapaya.

Katika mazungumzo yao Bi. Chansa alitumia fursa hiyo kujitambulisha kwa mara ya kwanza pamoja na Kumpongeza Dkt. Ndumbaro kwa Kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Wizara wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kwa upande wake Dkt. Ndumbaro alimshukuru kwa kuja ofisini kwake na kumwahidi kumpatia ushirikiano wa kutosha wakati wote wautendaji wa majukumu yake akiwa hapa nchini. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi Ndogo ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.  
Mazungumzo yakiendelea.
Dkt. Ndumbaro akimkaribisha Bi. Shansa ofisini kwake walipokutana kabla ya kuanza kwa mazungumzo yao. 




Waziri Mahiga akutana kwa Mazungumzo na Balozi wa Misri.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Misri hapa nchini Mhe. Mohamed Gaber Abouelwafa. Katika mazungumzo yao Balozi Abouelwafa alimweleza Dkt. Mahiga kuwa wanafurahishwa na mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na Misri, ambapo kwa sasa Misri wanatekeleza mradi mkubwa wa Bwawa la kuzalisha Umeme Nchini, vilevile Misri itaendelea kuboresha miundombinu ya uzalishaji wa maji kwa kuchimba visima vingine vya maji Nchini.
Pamoja na Mambo mengine Dkt. Mahiga alimweleza Balozi Abouelwafa kuwa Tanzania itaendelea kumpa ushirikiano wa kutosha  katika utekelezaji wa majukumu yake hapa nchini.
Aidha, Dkt. Mahiga alimweleza Balozi kuwa Tanzania inatambua mchango wa Misri kwenye sekta mbalimbali zikiwemo Afya, Elimu na Biashara. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, zilizopo jijini Dar Es Salaam 
Katibu wa Waziri Bw. Magabilo Murobi (wa kwanza kushoto), pamoja na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Afrika Bw. Wilbroad Kayombo wakifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Dkt. Mahiga na Balozi Abouelwafa (hawapo pichani).
Mazungumzo yakiendelea kati ya Dkt. Mahiga na Balozi Abouelwafa
Maafisa kutoka Ubalozi wa Misri nchini Tanzania wa kwanza kushoto ni Bw. Ahmed Elghoul na Bi. Nevine Elsaeed nao wakifuatilia kwa makini mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kati ya Dkt. Mahiga na Balozi Abouelwafa (hawapo pichani).



Monday, January 14, 2019

Dkt. Ndumbaro awaaga Watanzania wanaokwenda Japan kujifunza masuala ya Uongozi

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Japan, Mhe. Shinichi Goto aliyeambatana na washiriki kutoka Tanzania wanao kwenda Nchini Japan kwa ajili ya kupata mafunzo ya Uongozi katika sekta mbalimbali. Mafunzo hayo yatadumu kwa muda wa siku 50. Aidha, Dkt. Ndumbaro amemshukuru Balozi Goto kwa kuendelea kuiwakilisha vyema nchi ya Japan hapa nchini ambapo aliahidi kuwa Japan itaendelea kuchangia maendeleo katika sekta mbalimbali.
 Dkt. Ndumbaro amewaasa Washiriki wanaokwenda katika mafunzo hayo kuitumia fursa hiyo vyema kwa kujifunza mambo mampya kutoka Taifa hilo. 


Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw. Caesar Waitara (hayupo pichani) yamefanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  jijini Dar Es Salaam.
Mazungumzo yakiendelea 
Dkt. Ndumbaro akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Goto
Dkt. Ndumbaro pamoja na Balozi Goto wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki kutoka Tanzania wanao kwenda nchini Japani.  




Saturday, January 12, 2019

Tanzania yatafuta Soko la Utalii Uholanzi

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania yatafuta Soko la Utalii Uholanzi

Taasisi za Serikali na kampuni binafsi mbalimbali za utalii zipo nchini Uholanzi kushiriki maonesho ya utalii ya kimataifa kwa lengo la kutafuta fursa mpya za soko la utalii nchini humo.
Maonesho hayo maarufu kama Holday Fair 2019 (Vakantiebeurs2019) yalianza tarehe 9 Januari na yatakamilika tarehe 13 Januari 2019, hufanyika kila mwaka katika mji wa Utrecht na kushirikisha taasisi mbalimbali kutoka duniani kote.
Taasisi za Serikali zinazoshiriki ni Bodi ya Utalii Tanznaia (TTB), Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA). Kwa upande wa kampuni binafsi ni into Africa Eco Travel Ltd, Migada Adventures, Mbalaget Tented Camp Ltd, Kili Fair Promotions Ltd, East Africa Camps na Makasa Tanzania Safaris.
Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Irene Kasyanju amesema kuwa maonesho hayo ni fursa adhimu kwa nchi kutangaza vivutio vya utalii ambapo kwa mwaka 2019, waandaji kwa mara ya kwanza wametoa nafasi kwa Balozi za nje zilizopo nchini humo kutangaza pia fursa za biashara na uwekezaji.
Balozi Kasyanju ambao Ubalozi wake unashiriki katika maonesho hayo alieleza kuwa maonesho hayo yataenda sanjari na Vakantiebeurs Travel Congress, Vakantiebeurs Consumer Day na Vakantiebeurs Trade Day ambapo washiriki watapata fursa ya kupeana taarifa muhimu kuhusu mwelekeo na maendeleo ya biashara ya utalii katika maeneo mbalimbali duniani, vivutio vipya pamoja na kufanya biashara.
Ushiriki wa Tanzania katika maonesho hayo utasaidia washiriki kukutana na wadau na kuanzisha uhusiano wa kibiashara unaotarajiwa kufungua soko la utalii nchini baada ya wadau hao kupata maelezo ya kutosha kuhusu vivutio vilivyopo nchini na faida zake. 

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma, Tanzania
11 Januari 2019

Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Irene Kasyanju (mwenye miwani) akiwa na washiriki wengine katika Maonesho ya Utalii ya Kimataifa yanayofanyika nchini Uholanzi kuanzia tarehe 9 hadi 13 Januari 2019.

Wageni mbalimbali wanatembelea banda la Tanzania ili kupata maelezo kuhusu vivutio vya uwekezaji nchini

Banda la Tanzania linatia fora kwa kutembelewa na idadi kubwa ya watu wanaotaka kupata maelezo kuhusu fursa na vivutio vya utalii nchini.

Wageni katika banda la Tanzania.

Balozi Kasyanju na washiriki wenzake wakiwa katika badna la Tanzania tayari kuanza kazi ya kuuza vivutio vya utalii nchini Uholanzi.

Dkt. Ndumbaro akutana na Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi, Mhe. Rwegasira Mukasa Oscar  (kushoto) akiwakaribisha wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi katika kikao na uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Bunge Dodoma tarehe 11 Januari 2019.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro aliongoza ujumbe wa Wizara katika kikao na Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Bunge Dodoma tarehe 11 Januari 2019. Wengine katika picha, kuli ni Bw. Hamid Mbegu, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu na kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Bw. Japahary Kachenje.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro aliwasilisha taarifa mbili katika kikao hicho. Taarifa ya kwanza ilihusu hatua zinazochukuliwa na Wizara katika mapambano dhidi ya Ukimwi na taarifa ya pili ilihusu namna Wizara inavyoshirikiana na mashirika ya kimataifa, kikanda na nchi mbalimbali katika kukabiliana na biashara haramu ya dawa za kulevya.

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na uongozi wa Wizara ukisikiliza kwa makini taarifa zilizokuwa zinawasilishwa na Mhe. Naibu Waziri.

Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi walioshiriki kikao hicho.

Mhe. Amina Mollel, Mbunge wa Viti Maalum akichangia jambo wakati wa kikoa kati ya Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Mhe. Masoud Abdallah akichangia jambo katika kikao hicho.

Ujumbe wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ulioshiriki kikao kati ya Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje.

Sehemu nyingine ya Ujumbe wa Wizara ulioshiriki kikao hicho.

Waheshimiwa Wabjumbe wa Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi wakisalimiana na Mhe. Naibu Waziri kabla ya kikao kuanza.

Mhe. Allan Kiula, Mbunge wa Iramba Mashariki akisalimiana na  Mhe. Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mbunge akibadilishana mawazo na Mhe. Naibu Waziri kabla ya kuanza kikao.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Joyce Kimey akiongea machache na Mhe. Naibu Waziri kabla hawajaingia katika kikao na Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi.