Wednesday, January 16, 2019

DKT. NDUMBARO ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO UBALOZI WA NIGERIA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Nigeria hapa nchini kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa sita wa nchi hiyo Mhe. Alhaji Shehu Shagari kilichotokea tarehe 28 Desemba 2019. Dkt. Ndumbaro alipata fursa ya kufanya mazungumzo na Balozi wa Nigeria hapa nchini Mhe. Dkt.Sahabi Isa Gada. Tukio hilo limefanyika jijini Dar Es Salaam katika Ubalozi wa Nigeria hapa nchini.  
Balozi Gada akimwelezea jambo Dkt. Ndumbaro wakati wa mazungumzo.
Sehemy ya Maafisa wa Ubalozi wa Nigeria nchini wakisikiliza kwa makini mazungumzo kati Dkt. Ndumbaro na Balozi Gada (hawapa pichani).
Dkt. Ndumbaro akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Gada na maafisa wa Ubalozi huo.
Dkt. Ndumbaro akiagana na Balozi Dkt. Gada. 





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.