Friday, January 4, 2019

Tangazo la Nafasi za Kazi


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tangazo la Nafasi za Kazi
Sekretarieti ya Shirika la Kuzuia Silaha za Kemikali (Secretariat of the Organization for the Prohibition of Chemical Weapons- OPCW) imetangaza nafasi za kazi za Afisa Mwandamizi wa Masuala ya Umma na Afisa wa Masuala ya Umma (Public Affairs Officer P-4 and Public Affairs Officer P-2).  

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inawahimiza Watanzania, hususan wanawake kuchangamkia nafasi hizo ambapo mwisho wa kufanya maombi kwa nafasi ya Public Affairs Officer P-4 ni tarehe 24 Januari 2019 na ile ya Public Affairs Officer P-2 ni tarehe 9 Januari 2019.  

Maombi yafanywe kwa njia ya mtandao kupitia tovuti www.opcw.org ambayo pia ina maelezo zaidi kuhusu nafasi hizo.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
4 Januari 2019

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.