Wednesday, January 16, 2019

Dkt. Mahiga akagua ujenzi wa ofisi ya Wizara Ihumwa, Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akiweka saini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye eneo linalojengwa jengo la ofisi ya Wizara Ihumwa, Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la ofisi ya Wizara Ihumwa Dodoma. Mhe. Waziri alielezwa kuwa ujenzi huo unaenda katika kasi inayoridhisha ambapo wakandarasi wapo mbele ya mpangoa kazi.

Waziri Mahiga na Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Hamid Mbegu wakioneshana alama za mipaka ya kiwanja cha Wizara.

Waziri Mahiga akiendelea na ukaguzi wa jengo la ofisi ya Wizara.
Waziri Mahiga akitoa maelekezo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Hamid Mbegu 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.