Tuesday, January 15, 2019

Waziri Mahiga akutana kwa Mazungumzo na Balozi wa Misri.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Misri hapa nchini Mhe. Mohamed Gaber Abouelwafa. Katika mazungumzo yao Balozi Abouelwafa alimweleza Dkt. Mahiga kuwa wanafurahishwa na mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na Misri, ambapo kwa sasa Misri wanatekeleza mradi mkubwa wa Bwawa la kuzalisha Umeme Nchini, vilevile Misri itaendelea kuboresha miundombinu ya uzalishaji wa maji kwa kuchimba visima vingine vya maji Nchini.
Pamoja na Mambo mengine Dkt. Mahiga alimweleza Balozi Abouelwafa kuwa Tanzania itaendelea kumpa ushirikiano wa kutosha  katika utekelezaji wa majukumu yake hapa nchini.
Aidha, Dkt. Mahiga alimweleza Balozi kuwa Tanzania inatambua mchango wa Misri kwenye sekta mbalimbali zikiwemo Afya, Elimu na Biashara. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, zilizopo jijini Dar Es Salaam 
Katibu wa Waziri Bw. Magabilo Murobi (wa kwanza kushoto), pamoja na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Afrika Bw. Wilbroad Kayombo wakifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Dkt. Mahiga na Balozi Abouelwafa (hawapo pichani).
Mazungumzo yakiendelea kati ya Dkt. Mahiga na Balozi Abouelwafa
Maafisa kutoka Ubalozi wa Misri nchini Tanzania wa kwanza kushoto ni Bw. Ahmed Elghoul na Bi. Nevine Elsaeed nao wakifuatilia kwa makini mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kati ya Dkt. Mahiga na Balozi Abouelwafa (hawapo pichani).



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.