Tuesday, March 3, 2020

PROF. KABUDI APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO KUTOKA UN, UNHCR


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amepokea hati za utambulisho kutoka kwa Mratibu Mkazi wa Shughuli za Umoja wa Mataifa (UN) Bw. Zlatan Milišić Pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Antonio Canhandula Jijini Dar es Salaam.

Waziri Kabudi amewaeleza Bw. Milišić na Bw. Canhandula kuwa UN pamoja na UNHCR zimekuwa na mchango mkubwa kwa kuiunga mkono Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kukuza maendeleo pamoja na zile za kushughulikia masuala ya wakimbizi.

“Kwa ujumla UN imekuwa ikisaidia Tanzania kufanikisha agenda zake za maendeleo endelevu ya kijamii, na kiuchumi hivyo Serikali itaendelea kuhakikisha inaendeleza uhusiano huu," Amesema Prof. Kabudi.

Kwa upande wake Mratibu Mkazi wa Shughuli za Umoja wa Mataifa nchini (UN) Bw. Milisic amesema kuwa uhusiano wa UN na Serikali ya Tanzania ni wa muda mrefu na hivyo ni jukumu la UN kuhakikisha inaimarisha uhusiano huo na kuuboresha.

 “Ni matumaini yangu kuwa uhusiano huu tutauboresha vizuri na kuimarisha kwa maslahi mapana na maendeleo endelevu ya taifa la Tanzania," Amesema Bw. Milišić

Nae Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Canhandula amesema wanatambua mchango mkubwa ambao Tanzania imekuwa ikiutoa kuhakikisha inaimarisha ulinzi wa maeneo ya wakimbizi ili wananchi wa maeneo hayo waendelee kuishi kwa amani na utulivu pamoja na kupatiwa mahitaji muhimu kama vile malazi na mavazi.

"Kwa kweli UNHCR tunafurahishwa na jinsi Serikali ya Tanzania ambavyo imekuwa ikipokea wakimbizi na kuwapatia baadhi ya mahitaji muhimu……tunaomba tuendeleze ushirikiano huu kwa maendeleo yetu," Amesema Bw. Canhandula.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimfafanulia jambo Mratibu Mkazi wa Shughuli za Umoja wa Mataifa (UN) Bw. Zlatan Milišić katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiisoma hati ya utambulisho mara baada ya kuipokea kutoka kwa Mratibu Mkazi wa Shughuli za Umoja wa Mataifa (UN) Bw. Zlatan Milišić katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Antonio Canhandula akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) kabla ya kukabidhi hati ya utambulisho katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akipokea hati ya utambulisho kutoka kwa Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Antonio Canhandula katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 



BALOZI MBELWA ATOA RAI KWA WAFANYABIASHARA WA TANZANIA

Mhe. Mbelwa Kairuki Balozi wa Tanzania nchini China, ametoa rai kwa wafanyabiashara wa Tanzania ambao shughuli zao zinahushisha China, kuwa na subira ya kuzuru China wakati huu ambao tatizo la Corona Virus (COVID-19) bado linaendelea kushughulikiwa nchini humo.


Monday, March 2, 2020

MKUTANO WA BARAZA LA MAWAZIRI WA SADC KUFANYIKA TAREHE 16 - 17 MACHI


Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unatarajiwa kufanyika hapa nchini kuanzia tarehe 11 hadi 17 Machi, 2020 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amesema kuwa mkutano huo utafanyika kuanzia tarehe 12 hadi 17 Machi 2020 ambapo utatanguliwa na mkutano wa wataalamu pamoja na Makatibu Wakuu na kufuatiwa na mkutano wa mawaziri tarehe 16 - 17 Machi, 2020.

"Pamoja na mambo mengine, mkutano huu utahusisha Mawaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mawaziri wa Fedha, Uchumi na Mipango pamoja na Mawaziri wa Viwanda na Biashara," Amesema Prof. Kabudi

Waziri Kabudi amesema kuwa mkutano huo utahudhuriwa na Mawaziri 16 kutoka Nchi wanachama wa SADC za Angola, Namibia, Zambia, Zimbabwe, Comoro, Lesotho, Mauritius, Madagascar, Kongo DRC, Shelisheli, Msumbiji, Afrika Kusini, Tanzania, Malawi, Botswana pamoja na Eswatini)

Aidha, Kwa mujibu wa Mhe. Waziri Kabudi, Mkutano huo utakuwa mkutano wa kwanzawa SADC wa Baraza la Mawaziri kuendeshwa kwa lugha ya Kiswahili baada ya lugha hiyo kuwa miongoni mwa lugha rasmi za Jumuiya hiyo.

Prof. Kabudi aliongeza kuwa, mkutano huo utajadili masuala mbalimbali muhimu kwa mustakabali wa maendeleo na ustawi wa nchi wananchama wa SADC.

"Mktano huu utapokea taarifa na kutolea maelekezo taarifa za vikao mbalimbali vya kisekta vya kamati za mawaziri ambavyo vimefanyika nchini tangu Septemba 2019," Ameongeza Prof. Kabudi.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo ktk picha) kuhusu Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC utakaofanyika tarehe 11 – 17 Machi, 2020 Jijini Dar es Salaam. Kulia mwenye kilemba ni Bibi. Zamaradi Kawawa, akifuatiwa na Naibu Katibu MKuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Mwinyi, kulia kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bibi. Agnes Kayola

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC utakaofanyika tarehe 11 – 17 Machi, 2020 Jijini Dar es Salaam  




Friday, February 28, 2020

MASENETA WA UFARANSA KUFANYA ZIARA NCHINI


Ujumbe wa maseneta sita (6) kutoka Ufaransa unatarajiwa kufanya ziara nchini kuanzia tarehe 01 hadi 08 Machi, 2020.  

Ujumbe huo utawasili nchini tarehe 29 Februari, 2020 kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman Karume Zanzibar utaongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge la Ufaransa inayoshughulikia masuala ya Maendeleo Endelevu na Naibu Rais wa Kikundi cha Kirafiki na nchi za Bahari ya Hindi Seneta Harve Maurey.


PROF. KABUDI AHUTUBIA BARAZA LA HAKI ZA BINADAMU LA UMOJA WA MATAIFA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akihutubia katika Kikao cha 43 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa linaloendelea Geneva,nchini Uswisi ambalo linatarajiwa kumalizika March 20,2020 ambapo masuala kadhaa kuhusu haki za binadamu yanajadiliwa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akitoa hotuba ya Tanzania katika Kikao cha 43 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa linaloendelea Geneva,nchini Uswisi ambalo linatarajiwa kumalizika March 20,2020 ambapo masuala kadhaa kuhusu haki za binadamu yanajadiliwa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akipongezwa na Balozi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Maimuna Tarishi pamoja na baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki mara baada ya kutoa hutuba katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, Geneva, Uswisi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akipongezwa na baadhi ya viongozi wa Mataifa ya Afrika wanaohudhuria Mkutano wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa linaloendelea Geneva,Uswisi




Wednesday, February 26, 2020

PROF. KABUDI AKUTANA NA KATIBU MKUU JUMUIYA YA MADOLA


Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) (katikati aliyeshika kalamu) akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland. Kushoto kwa Prof. Kabudi ni Balozi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Geneva,Uswisi Balozi Maimuna Tarishi pamoja na Wakurugenzi na Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Jumuiya hiyo zilizopo Geneva,Uswisi
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland akiwa katika mazungumzo na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) (hayupo pichani) Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Jumuiya hiyo zilizopo Geneva,Uswisi. Kulia ni msaidizi wa Bi Patriacia Scotland.
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland.Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Jumuiya hiyo zilizopo Geneva,Uswisi.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na  Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Jumuiya hiyo zilizopo Geneva,Uswisi. Kushoto kwa Bi. Patricia Scotland ni Balozi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Geneva,Uswisi Balozi Maimuna Tarishi
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiagana na  Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Jumuiya hiyo zilizopo Geneva,Uswisi.




TANZANIA YAKABIDHIWA TAKWIMU ZA UFANYAJI BIASHARA KATI YAKE NA JUMUIYA YA MADOLA.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Patricia Scotland mazungumzo yaliyolenga masuala kadhaa ikiwa ni pamoja na mradi ambao Jumuiya ya Madola umeufanya kuhusu Tanzania.

Mradi huo umelenga kuangalia takwimu mbalimbali zinazohusu biashara kwa kuangalia nchi ambazo Tanzania inaagiza ama kuuza bidhaa zake kwa wingi katika nchi za Jumuiya ya Madola mradi ambao umeelezwa kuwa na manufaa makubwa kwa Tanzania ambapo kwa sasa nchi za India na Afrika kusini ndizo kinara.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland amesema Tanzania ni mdau muhimu katika jumuiya hiyo na kwamba amefurahi kumkabidhi Prof. Kabudi nakala ya utafiti huo kwa niaba ya Tanzania jambo litakaloifanya Tanzania kuendelea kuangalia maeneo ya kujiimarisha katika ufanyaji wa biashara na nchi za Jumuiya ya Madola.

Mbali na masuala hayo ya mradi huo wa takwimu wa biashara kuhusu Tanzania uliofanywa bure na Jumuiya hiyo ya Madola pia wawili hao wamezungumzia masuala mengine ikiwa ni pamoja na namna Jumuiya hiyo na Tanzania zitakavyofanya kuongeza usawa wa jinsia,masuala ya haki za binadamu pamoja na uimarishaji wa mfumo wa mahakama nchini Tanzania.




Tuesday, February 25, 2020

TANZANIA YASHIRIKI KWA MARA YA KWANZA KATIKA MAONESHO YA KIMATAIFA YA BIDHAA ZA KILIMO YA PARIS

Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Samwel Shelukindo (katikati) akiwa  kwenye picha ya pamoja na Ujumbe wa Tanzania unaoshiriki kwa mara ya kwanza katika Maonesho ya Kimataifa ya Bidhaa za Kilimo ya Paris yanayofanyika mjini humo kuanzia tarehe 22 Februari 2020 hadi tarehe 1 Machi 2020.
Wageni mbalimbali wakipata maelezo kuhusu fursa za bidhaa za kilimo zinazopatikana Tanzania walipotembelea Banda la la Tanzania wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Bidhaa za Kilimo yanayofanyika jijini Paris kuanzia tarehe 22 Februari 2020 hadi tarehe 1 Machi 2020.
======================================================


TANZANIA YASHIRIKI KWA MARA KWANZA KATIKA MAONESHO YA KIMATAIFA YA BIDHAA ZA KILIMO YA PARIS 2020, UFARANSA

Tanzania inashiriki kwa mara ya kwanza katika Maonesho ya Kimataifa ya Bidhaa za Kilimo ya Paris 2020 yanayofanyika jijini Paris, Ufaransa kuanzia tarehe 22 Februari 2020 hadi tarehe 1 Machi 2020.

Maonesho hayo ambayo yalifunguliwa na Mhe. Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, yanatarajiwa kutembelewa na zaidi ya watu 600,000.

Wakati wa maonesho hayo, Tanzania itapata fursa ya kuonyesha bidhaa zake yakiwemo mazao ya kimkakati. Ujumbe wa Tanzania katika maonyesho hayo unaongozwa na Bw. Victor Rugemalila kutoka TANTRADE.

Ubalozi wa Tanzania ambao unaratibu maonesho hayo kupitia  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, unaishukuru Kampuni ya Tanzania Re-assurance (TAN-RE) ya Dar es Salaam, Tanzania, kwa kufadhili kwa kiasi kikubwa ushiriki wa Tanzania katika maonyesho. Aidha, Ubalozi unatambua mchango wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Kampuni ya Kahawa  ya Inter State.


Monday, February 24, 2020

PROF. KABUDI AKUTANA NA VIONGOZI MBALIMBALI AKIWA GENEVA - USWISI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi(Mb) akisaini katika kitabu cha wageni katika ubalozi  wa kudumu wa Tanzania umoja wa Mataifa uliopo Geneva Nchini Uswisi

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika kikao cha 43 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kinachofanyika Geneva,Uswisi


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika mazungumzo na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Filippo Grand(hayupo Pichani). Mazungumzo hayo yamefanyika katika Makao Makuu ya Ofisi za UNHCR zilizopo Geneva-Uswisi

Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Filippo Grand akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) (hayupo pichani)
Mazungumzo hayo yamefanyika katika Makao Makuu ya Ofisi za UNHCR zilizopo Geneva-Uswisi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika mazungumzo na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Filippo Grand Mazungumzo hayo yamefanyika katika Makao Makuu ya Ofisi za UNHCR zilizopo Geneva-Uswisi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiagana na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Filippo Grand mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika Makao Makuu ya Ofisi za UNHCR zilizopo Geneva-Uswisi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland Mhe. Simon Coveney. Mazungumzo hayo yamefanyika katika jengo la Umoja wa Mataifa Kuhusu Haki za Binadamu Geneva,Uswisi

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland Mhe. Simon Coveney akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) Mazungumzo hayo yamefanyika katika jengo la Umoja wa Mataifa Kuhusu Haki za Binadamu Geneva,Uswisi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiagana na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland Mhe. Simon Coveney mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika jengo la Umoja wa Mataifa Kuhusu Haki za Binadamu Geneva,Uswisi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akizungumza na Waziri wa mambo ya Nje wa Denmark Bw. Jeppe Kofod.Mazungumzo hayo yamefanyika katika jengo la Umoja wa Mataifa Kuhusu Haki za Binadamu Geneva,Uswisi. Anayeshuhudia kulia ni Balozi wa kudumu wa Tanzania umoja wa Mataifa Geneva,Balozi Maimuna Tarishi.

Sunday, February 23, 2020

TANZANIA YASHINDA TUZO YA UTALII NCHINI INDIA

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda (kulia) akipokea Tuzo ya Utalii baada ya Tanzania kuibuka mshindi kwa kuonekana ni eneo bora zaidi la Utalii wa Wanyamapori duniani nchini India kwa mwaka 2020 (The Best International Wildlife Destination) iliyotangazwa katika hafla ya kutoa tuzo hizo zilizotolewa na Jarida la Utalii la "Outlook Traveller Magazine" na kufanyika katika Hoteli ya Rossette jijini New Delhi, India tarehe 22 Februari 2020.
Mhe. Balozi Luvanda akifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea katika hafla ya kutoa tuzo za utalii zilizotolewa na Jarida la "Outlook Traveller Magazine" na kufanyika katika Hoteli ya Rossette jijini New Delhi, India tarehe 22 Februari 2020. Tanzania iliibuka mshindi kwa kuonekana ni eneo bora zaidi la utalii wa wanyamapori duniani nchini India kwa mwaka 2020.
===============================================================


TANZANIA YASHINDA TUZO YA UTALII NCHINI INDIA

Tanzania imeshinda tuzo ya utalii kwa kuonekana ni eneo bora zaidi la utalii wa wanyamapori duniani nchini India kwa mwaka 2020 (The Best International Wildlife Destination).

Balozi wa Tanzania nchini India Mhe. Baraka H. Luvanda amepokea Tuzo hiyo kutoka Jarida la kihindi la “Outlook Traveller Magazine” katika hafla maalum iliyofanyika katika Hoteli ya Roseate jijini New Delhi kwa niaba ya Tanzania. Hafla hiyo ilihudhuriwa na takriban washiriki 200.  

Tanzania imepata ushindi huo kutokana na kura zilizopigwa kwenye mtandao wa jarida hilo la “Outlook Traveller” lililoshirikisha wapiga kura 1,200,000 kwa njia ya mtandao.

Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kushinda tuzo hiyo ambayo hutolewa kila mwaka nchini India, washiriki kupitia jarida hilo wameichagua Tanzania kama eneo bora zaidi la utalii wa wanyamapori duniani.

Aidha, Shelisheli na Indonesia kwa pamoja zilishinda tuzo kama maeneo bora zaidi duniani kwenye utalii wa fukwe.

The Outlook Traveller Award ni tuzo ya kifahari zaidi katika sekta ya utalii nchini India na hutolewa na Jarida la Utalii la “Outlook Traveller Magazine” ambalo ni jarida namba moja nchini India linalojishughulisha kutangaza utalii, ndani na nje ya India.

Wakati akipokea tuzo hiyo, pamoja na mambo mengine Balozi Luvanda aliushukuru uongozi wa Jarida hilo kwa kuandaa tuzo hizo muhimu ambazo zinasaidia kutanganza utalii wa nchi mbalimbali nchini India na akaeleza kuwa kupitia tuzo hiyo, watu wengi zaidi wataijua Tanzania na vivutio vingi vya utalii vilivyopo nchini na kuwavutia kutembelea Tanzania.

Mafanikio hayo yanatokana na jitihada zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini India, Wizara za Utalii za Tanzania Bara na Zanzibar, na Taasisi zote zinazosimamia masuala ya utalii za ndani na nje ya nchi katika kutangaza vivutio vya utalii kwa nchi mbalimbali duniani ikiwemo India.

Kupitia juhudi hizi, idadi ya watalii wanaokuja Tanzania kutoka India imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Kwa mfano, idadi hiyo iliongezeka kutoka watalii 39,115 mwaka 2016 hadi watalii 69,876 mwaka 2017.  

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia Balozi zake ukiwemo Ubalozi wa Tanzania nchini India na wadau wengine itaendelea kuongeza juhudi za kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania ili kuhakikisha idadi ya watalii kutoka India na nchi zingine duniani inaongezeka. Hii ni pamoja na kutumia Shirika la Ndege la Tanzania ambalo limeanza safari za moja kwa moja kutoka Dar es Salaam kwenda Mumbai kuanzia mwezi Julai 2019 kwa upande wa India.