Wednesday, May 13, 2020
Saturday, May 9, 2020
SERIKALI: DAWA YA COVID 19 KUTOKA MADAGASCAR NI KWA AJILI YA UTAFITI KWANZA
Serikali
kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, imesema kuwa
dawa ambayo nchi ya Madagascar imeitoa kama msaada kwa Serikali ya Tanzania ni
kwa ajili ya utafiti kwanza.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John
Kabudi (Mb) amewaambia waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuwa dawa
hiyo inayojulikana kaitaalamu kama "COVIDORGANICS" ni kwa ajili ya
utafiti na siyo kwa ajili ya matumizi ya binadamu.
"Huu
mzigo (dawa) ni kwaajili ya kufanyiwa utafiti…….na kazi kubwa tunayoianza leo
ni na wataalamu wetu wa afya ni kufanya utafiti," Amesema Prof. Kabudi
Prof.
Kabudi ameongeza kuwa dawa hiyo siyo kwa ajili ya kugawa kwa wananchi, bali ni
kwa ajili ya utafiti na mara baada ya utafiti kukamilika wataalamu wa afya
watatoa maelekezo ya jinsi ya utumiaji wa dawa hiyo.
Aidha,
dawa hiyo imegawanyika katika makundi mawili ambapo kundi la kwanza la dawa ni
kwa ajili ya kujikinga na maambukizi ya COVID 19 kwa wale ambao hawajaambukizwa
ugonjwa wa Corona. Kundi la pili ni kwa ajili ya matibabu kwa wananchi ambao
tayari wameathirika na COVID 19.
"Dawa
hii tuliyokuja nayo jana kutoka Madagascar mara baada ya utafiti kukamilika na
kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu wetu wa afya itatumika kukinga
wananchi ambao hawajaathirika na kutibu wale walioathirika," Prof. Kabudi
Kwa
upande wake Mganga
Mkuu wa serikali Prof. Abel Makubi amesema kuwa mara baada ya kupokea dawa hiyo
kazi ya kwanza ya ni kuanza utafiti ambao utaonesha kama dawa hiyo ni salama na
haina madara kwa wananchi na pili utafiti wa kuangalia ubora wa kutibu au
kupunguza makali ya COVID 19.
"Mara
baada ya utafiti wa dawa hii kukamilika itatumika katika makundi matatu ambayo
kundi la kwanza ni wagonjwa kutumia dawa ya kawaida, kundi la pili watapata
dawa ya kawaida na hii iliyotoka Madagascar na kundi la tatu wagonjwa watatumia
dawa ya kawaida na ile inayozalishwa na Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya
Binadamu (Nimr)," Amesema Prof. Makubi
Prof.
Makubi pamoja na mambo mengine, ametoa wito kwa watanzania kuchukua tahadhari
katika kujikinga na ugonjwa wa COVID 19 na wasibweteke na lolote.
Nae
Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (Nimr) Prof. Yunus
Mgaya amesema kuwa Nimr imejipanga kushirikiana na taasisi nyingine za Serikali
hasa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali katika kuhakikisha inafanya utafiti wa
kina juu ya matumizi ya dawa hiyo.
"Nimr
inafanya tafiti mbalimbali za kupambana na ugonjwa huu wa COVID 19 na
itaendelea kufanya tafiti hizo ili kuwasaidia watanzania," amesema Prof. Mgaya
Kwa
upande wake Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko amesema kuwa Ofisi
ya Mkemia Mkuu inalo jukumu lakuchunguza dawa au sumu zozote kwenye sampuli, kukadiria
kwa usahihi kiasi cha dawa, umetaboli au sumu.
Drkt.
Mafumiko ameongeza kuwa, kupitia utafiti wa dawa hiyo, ofissi yake kwa
kushirikiana na wataalamu wa afya watatafsiri matokeo ya uchunguzi katika dawa
hiyo kutoa maelekezo sahihi juu ya matumizi yake kwa mwananchi.
Mkutano
huu ulihudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), Mganga Mkuu wa serikali Prof. Abel Makubi, Mkurugenzi
wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (Nimr) Prof. Yunus Mgaya, Mkemia
Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Tiba za
Asili Dkt. Paul Mkama.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John
Kabudi (Mb) akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) dawa ambayo
imetolewa na Madagascar leo Jijini Dae es Salaam
Mganga
Mkuu wa serikali Prof. Abel Makubi akiongea na waandishi wa habari (hawapo
pichani) wakati wa mkutano uliofanyika leo Jijini Dae es Salaam
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Prof. Yunus Mgaya akiongea
na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mkutano uliofanyika leo
Jijini Dae es Salaam
Mkemia
Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko akiongea na waandishi wa habari
(hawapo pichani) wakati wa mkutano
Mkuu
wa Kitengo cha Tiba za Asili Dkt. Paul Mkama akiongea na waandishi wa habari
(hawapo pichani) wakati mkutano ukiendelea
Wednesday, May 6, 2020
SERIKALI YAENDELEA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZINAZOJITOKEZA MIPAKANI
Serikali
ya Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
imesema changamoto zinazojitokeza katika mipaka mbalimbali ya Tanzania wakati
wa usafirishaji wa bidhaa hususan katika kipindi hiki cha janga la COVID-19
zinaendelea kutatuliwa kwa majadiliano.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Kanali
Wilbert Ibuge ameyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa
Tanzania Nchini Zambia Mhe. Benson Keith Chali ili kuangalia namna ya kutatua
changamoto mbalimbali za usafirishaji wa bidhaa hususani zile zinazotoka katika
bandari ya Dar es Salaam kuelekea katika nchi za Ukanda wa Jumuiya ya Maendeleo
Kusini mwa Afrika SADC.
Ameongeza
kuwa katika kipindi hiki cha janga la COVID – 19 unaosababishwa na virusi vya
Corona changamoto mbalimbali zimejitokeza katika utoaji wa huduma za
usafirishaji wa huduma na bidhaa mbalimbali na hivyo serikali inafanya jitihada
za majadiliano na baadhi ya nchi katika mipaka ili kutatua changamoto
zinazojitkeza na kuwezesha huduma ya usafirishaji kuendelea bila ya vikwazo.
Nae
Balozi wa Zambia nchini Tanzania, Mhe. Chali amemuahidi Balozi Kanali Ibuge
kuwa Serikali ya Zambia imeshaanza kuzifanyia kazi changamoto zinazojitokeza.
"Suala hili limeshaanza kufanyiwa kazi na kila kitu kitakuwa sawa hivi
karibuni," amesema Balozi, Chali.
Katika
tukio jingine Balozi Kanali Wilbert Ibuge amekutana na kufanya mazungumzo na
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Bi.
Christine Musisi ambapo katika mazungumzo hayo wameongelea zaidi namna ya
kushirikiana na kuwezesha kujenga uwezo wa kuzalisha bidhaa mbalimbali kwa
wawekezaji wadogo na wakati wa Tanzania na kuwa na ubia na wawekezaji wakubwa
hususani katika kipindi hiki cha COVID – 19 na baada ya COVID – 19 ili
kuunusuru uchumi wa Taifa kuanguka.
"Tumekubaliana
kuongea ushirikiano katika sekta za afya, maji, maendeleo na uwekezaji …….kwa
hili tunawashukuru sana UNDP kwa kazi wanayoifanya lakini pia hata katika
ushirikiano wa kisera tumekuwa tukishirikiana nao jambo ambalo linazidi
kuimarisha uhusiano wetu hasa katika wakati huu wa COVID - 19 kwani jambo hili
linasaidia kunusuru uchumi wa taifa kuanguka," amesema Balozi, Kanali
Ibuge.
Katika
hatua nyingine, Balozi Ibuge amekutana na kufanya mazungumzo kwa nyakati
tofauti na Balozi wa Uingereza nchini Bi. Sarah Cooke pamoja na Mratibu Mkazi
wa Shughuli za Umoja wa Mataifa (UN) nchini Tanzania Bw. Zlatan Milišić ambapo wamezungumzia
masuala mbalimbali ya ushirikiano hususani katika kipindi hiki cha janga la
COVID – 19.
Tarehe
6 Aprili, 2020 ulifanyika Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya
ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo pamoja na mambo mengine, mkutano
huo ulijadili janga la COVID-19 unaosababishwa na virusi vya Corona. Mkutano
huo ulihusisha Mawaziri wenye dhamana ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki, Fedha,Viwanda,Biashara, Utalii, Mambo ya Ndani na Uchukuzi, kutoka
nchi 16 wanachama wa SADC.
Katika
mkutano huo, Baraza la Mawaziri lilitoa mwongozo kuhusu Usafirishaji wa Bidhaa
Muhimu na Huduma katika Nchi za SADC katika kipindi hiki cha janga la Virusi
vya Corona. Mwongozo huu unatumika katika kipindi hiki unalenga kupunguza safari
zisizo za lazima na kuwezesa usafirishaji wa bidhaa muhimu wakati huu wa janga
la COVID - 19.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na UShirikiano
wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge akimueleza jambo Balozi wa
Uingereza nchini Mhe. Sarah Cooke wakati walipokutana kwa mazungumzo leo jijini
Dar es Salaam
Balozi wa Uingereza nchini Mhe.
Sarah Cooke akiongea na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na UShirikiano wa
Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge wakati walipokutana kwa
mazungumzo leo jijini Dar es Salaam
Balozi wa Zambia nchini Mhe. Benson
Keith Chali akiongea na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na UShirikiano wa
Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge wakati walipokutana kwa
mazungumzo leo jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya
Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge akiongea na
Balozi wa Zambia nchini Mhe. Benson Keith Chali leo jijini Dar es Salaam
Mratibu Mkazi wa Shughuli za
Umoja wa Mataifa (UN), Bw. Zlatan Milišić akimuelezea jambo Katibu Mkuu Wizara
ya Mambo ya Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge
wakati walipokutana kwa mazungumzo leo jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya
Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge akiongea na
Mratibu Mkazi wa Shughuli za Umoja wa Mataifa (UN), Bw. Zlatan Milišić wakati
walipokutana kwa mazungumzo leo jijini Dar es Salaam
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Bi. Christine Musisi akimuelezea jambo
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali
Wilbert Ibuge wakati walipokutana kwa mazungumzo leo jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya
Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge akimfafanulia
jambo Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Bi.
Christine Musisi
Wednesday, April 29, 2020
Tuesday, April 28, 2020
TANZANIA NA KUWAIT ZAAHIDI KUIMARISHA USHIRIKIANO
Mazungumzo yakiendelea. |
Thursday, April 23, 2020
MUONGOZO WA USAFIRISHAJI BIDHAA KATIKA NCHI ZA SADC
Wednesday, April 8, 2020
SADC YAAZIMIA USAFIRISHAJI WA BIDHAA MUHIMU KUDHIBITI COVID - 19
MKUTAO WA DHARURA WA SADC KUHUSU COVID - 19 WAFANYIKA DAR ES SALAAM KWA NJIA YA MTANDAO
Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali kutoka Tanzania wakifuatilia Mkutano wa dharura kwa njia ya video ambao unawahusisha Maafisa Waandamizi Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), kuhusu mwenendo ya mlipuko wa ugonjwa wa virusi vya Corona (Covid-19), mkutano ambao umefanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Wednesday, April 1, 2020
KAMPUNI YA JAPAN YASAIDIA TAASISI YA MIFUPA (MOI) MSAADA WA VIFAA TIBA VYA MILIONI 80.9
Kampuni
ya EAA Co. Ltd ya nchini Japan bandia imetoa msaada wa viungo bandia vyenye thamani ya Shilingi milioni 80.9 kwa
Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) leo Jijini Dar es Salaam.
Akipokea
msaada huo, Mkurugenzi wa Tiba (MOI) Dkt. Samwel Swai amesema kuwa msaada huo utasaidia
kwa kiasi kikubwa matibabu ya wagonjwa wenye ulemavu wa miguu naa mikono.
Kwa
upande wake Meneja wa Kampuni ya EAA Co. Ltd, Josiah Benedict amesema wameguswa
na changamoto zinazowakabili watanzania ndiyo maana wameamua kuunga mkono
jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Dkt John Pombe Magufuli
ya kuboresha huduma za afya hapa nchini.
Msaada
huo unatokana na juhudi za Ubalozi wa Tanzania Japan kwa kushirikiana na
Watanzania waishio nchini Japan.
Mkurugenzi
wa Tiba (MOI) Dkt. Samwel Swai (kulia) akipokea baadhi ya vifaa kutoka kwa Meneja
wa Kampuni ya EAA, Josiah Benedict leo katika viwanja vya (MOI) jijini Dar es
Salaam
|
Mkurugenzi
wa Tiba (MOI) Dkt. Samwel Swai (kulia) akipokea baadhi ya vifaa kutoka kwa Meneja
wa Kampuni ya EAA Josiah Benedict leo katika viwanja vya (MOI) jijini Dar es
Salaam
|
Tuesday, March 31, 2020
PROF. KABUDI ATEMBELEA IDARA NA VITENGO WIZARANI AZUNGUMZA NA WATUMISHI
Mhe. Waziri Prof. Kabudi akimsikiliza mmoja wa watumishi wa Idara ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakitoa ufafanuzi kuhusiana na utekelezaji wa majukumu ya idara. |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi ametembelea Idara na vitengo vya wizarani na kuzungumza na watumishi walioko katika ofisi za wizara
kwenye majengo ya Chuo Kikuu cha Dodoma, tarehe 31 Machi 2020.
kwenye majengo ya Chuo Kikuu cha Dodoma, tarehe 31 Machi 2020.
Prof. Kabudi ametumia nafasi hiyo kuzungumza na mtumishi mmoja mmoja ili kuwafahamu na kuona jinsi wanavyoyafahamu na kutekeleza majukumu yao ikiwa ni pamoja na kuona namna wanavyogeuza changamoto wanazokutana nazo kuwa fursa katika sehemu zao za kazi
KATIBU MKUU BALOZI KANALI IBUGE AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA CHINA NCHINI KWA NJIA YA VIDEO
KATIBU MKUU BALOZI KANALI IBUGE AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA CHINA NCHINI KWA NJIA YA VIDEO
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge akiwa Dodoma, terehe 30 Machi 2020 amefanya mazungumzo kwa njia ya video (video conference) na Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke.
Pamoja na kujadili masuala mbalimbali ya mahusiano ya pande mbili (bilateral relations), viongozi hawa walizungumzia utayari wa Serikali wa nchi zote mbili katika kupambana na mgonjwa wa COVID-19. Sambamba na utayari huo, Katibu Mkuu alimfahamisha Balozi Wang Ke kuhusu hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Tanzania katika kupambana na kuenea kwa ugonjwa wa virusi vya corona. Wakati huohuo, alimweleza kuhusu utayari wa Serikali kushirikiana na wadau wengine duniani ikiwemo China katika kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona.
Vilevile, Katibu Mkuu ametumia fursa hiyo kuipongeza Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, kwa jitihada kubwa walizozifanya kiasi cha kufanikiwa kudhibiti kuenea zaidi kwa COVID-19 nchini humo na jitihada wanazozifanya ikiwemo kusaidia wataalamu, vifaa tiba na vya kujikinga kwa Mataifa mengine duniani ambapo COVID-19 inaendelea kuleta madhara. Hadi sasa China imefanya mazungumzo na nchi 24 za Afrika ikiwemo Tanzania yanayolenga kushauri na kubadlishana uzoefu na taarifa muhimu zitakazo saidia kutokomeza COVID-19.
Aidha,katika mazungumzo hayo Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke amebainisha kuridhishwa kwake juu ya hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania katika kukabiliana na kusambaa kwa maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona. Balozi Wang Ke aliongezea kusema pamoja na kutokuwepo maambukizi mapya nchini China, Serikali ya nchi hiyo bado inaendelea kuchukua tahadhari na hatua za kuzuia maambukizi mapya, na kuwa wataendelea kutoa mchango kwa Jumuiya ya Kimataifa katika kukabiliana na COVID-19. Balozi Wang Ke amesisitiza kuwa, Serikali ya China ipotayari kushirikiana kwa karibu na Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya COVID-19.
Katibu Mkuu ameushukuru Ubalozi wa China kwa utayari wake wa kushirikiana na Tanzania dhidi ya mapambano ya COVID-19, na kueleza kwamba Wizara itawasiliana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto ili kuandaa orodha ya mahitaji ambayo Ubalozi wa China unaweza kusaidia. Katibu Mkuu alirejea kauli ya Serikali kwamba mapambano dhidi ya virusi vya corona ni vita ambayo Tanzania haina budi kukabiliana navyo, kwa ujumla wake na kwamba hatua zote ambazo Tanzania inachukua chini ya uongozi wa Waziri Mkuu zinalenga kudhibiti kusambaa kwa virusi hivyo bila kuathiri shughuli za kila siku. Alisistiza kwamba Tanzania inaamini kwa jitihada inazochukua na kwa ushirikiano kutoka China itafanikiwa kushinda janga hili.
Mwisho, Balozi Wang Ke alimpongeza Katibu Mkuu kwa kuendelea kufanya mikutano na Waheshimiwa Mabalozi licha ya changamoto iliyopo ya COVID-19 kwa kuweka utaratibu wa kufanya kwa mikutano hiyo kwa njia ya Video akiwa Ofisini kwake Mtumba, Dodoma wakati Mabalozi wakiwa Dar es Salaam.
Friday, March 27, 2020
Thursday, March 26, 2020
KATIBU MKUU BALOZI KANALI IBUGE AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA VIETNAM
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Wilbert Ibuge na Balozi Nguyen Doanh wa
Vietnam wakiagana walipomaliza mazungumzo yao Ofisini jijini Dodoma .
|
Katibu
Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi
Col. Wilbert A. Ibuge leo tarehe 26 Machi, 2020 amekutana na kufanya mazungumzo
na Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Nguyen Kim Doanh katika ofisi za Wizara,
Makao Makuu, Jijini Dodoma.
Balozi
Doanh alikuja jijini Dodoma kufuatia wito wa Balozi Ibuge na kufanya mazungumzo
yaliyohusu mambo mbalimbali kuhusu mahusiano baina ya Tanzania na Vietnam, likiwemo
suala la uwekezaji wa Vietnam nchini kupitia Kampuni ya simu ya Halotel.
Katika
mazungumzo yao, viongozi hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha mahusiano
baina ya Nchi mbili hizo, ikiwemo uendelevu wa mawasiliano ya Kidiplomasia
ambapo mahusiano ya Tanzania na Vietnam yamefikisha miaka 55 mwaka huu huku fursa za uwekezaji nchini zikiendelea
kuimarishwa na hivyo kuiwezesha Serikali ya Vietnam ambayo ni mmiliki wa
Kampuni ya Simu ya mkononi ya Halotel kuwekeza nchini na kuendesha shughuli zake.
Balozi Ibuge
pia alimjulisha Mhe. Balozi Doanh kuwa Serikali ya Tanzania kupitia Wizara
itaendelea kuhimiza uwekezaji kutoka Vietnam na kusisitiza uwekezaji huo
kuzingatia sheria za nchi, kwa lengo la kuwepo tija kwa pande zote
zinazohusika.
Kufuatia
kikao hicho, Mhe. Balozi Doanh aliahidi kuendelea kuyasisitiza makampuni ya
Vietnam Nchini ikiwemo kampuni ya Halotel kuzingatia Sheria, Taratibu na Kanuni
zilizowekwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuhakikisha
pande zote mbili zinanufaika.
Subscribe to:
Posts (Atom)