Tuesday, June 21, 2022

SERIKALI YASISITIZA KUZINGATIA SHERIA ZA KIMATAIFA, KUHESHIMU HAKI ZA BINADAMU

Na Waandishi wetu, Dar

Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeihakikishia Jumuiya ya Kimataifa nchini kuwa inazingatia na kutekeleza sheria za kimataifa za haki za binadamu huku ikiendelea kulinda uhifadhi wa eneo la Ngorongoro.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) leo Jijini Dar es Salaam alipozungumza na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro.

“Napenda kuchukua nafasi hii kuuhakikishia umma wa Watanzania na Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tanzania inazingatia na kutekeleza sheria za kimataifa za haki za binadamu na hakuna nanma itaendesha mipango yake kwa kukiuka sheria za haki za binadamu”, alisema Balozi Mulamula.

Balozi Mulamula ameongeza kuwa Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii inatekeleza mpango wa kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro nchini kwa wananchi kuridhia kuhama kwa hiari yao na kwamba hakuna aliyeondolewa katika eneo hilo kwa nguvu kama inavyoelezwa.

“Tanzania siku zote italinda watu wake, maliasili zake na mipaka yake kwa kuzingatia sheria za kimataifa,” alisema Balozi Mulamula.

Akizungumza katika kikao hicho maalum kwa ajili ya kuielezea Jumuiya ya Kimataifa iliyopo nchini, Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amesema kinachoendelea katika eneo la Ngorongoro kwa wakati huu ni uhamaji wa hiari wa wananchi waliokuwa ndani ya eneo la Ngorongoro na sio kwamba kuna uhamishaji wa nguvu unaofanywa na Serikali.

“Serikali imekuja na mpango wa kulinda eneo la Ngorongoro, imechukua miaka 20 kuandaa na kuratibu mpango huu, ambao unatekelezwa sasa na hakuna uhamishaji wa nguvu unaofanywa kwa wanachi kama inavyodaiwa, wananchi husika wameshirikishwa vya kutosha na ndio maana wamekubali na kuamua kuhama kwa hiari wenyewe,” alisema Dkt. Ndumbaro.

Amesema Katiba ya Tanzania inasema watu wote ni sawa na kila mtu ana haki ya kuishi popote na kuongeza kuwa Serikali itaendelea kulinda na kuheshimu wananchi wake wote bila ya kujali rangi, kabila au dini zao.

Amesema wananchi wamepewa umiliki kwa miaka kadhaa na endapo itaonekana kuna haja ya kuichaukua ardhi hiyo anayeimiliki hulipwa fidia na kupewa ardhi katika eneo lingine na kuongeza kuwa wananchi wanaohama kwa hiari yao kutoka katika hifadhi ya Ngorongoro wanalipwa fidia na kupatiwa nyumba za makazi, maeneo yenye huduma za kijamii na ardhi kwa ajili ya malisho ya mifugo. 

Naye Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja (Mb) amesema kwamba katika wilaya ya Ngorongoro kuna maeneo mawili ambayo yamekuwa yakizua mjadala ambayo ni eneo la hifadhi la Ngorongoro ambalo ni urithi wa dunia na Pori Tengefu la Loliondo.

Amesema Serikali imechukua uamuzi wa kutekeleza mpango huo kutokana na changamoto kadhaa ambazo zinatishia uhifadhi wa eneo la Ngorongoro na kuongeza kuwa uhamaji wa hiari unaofanyika katika eneo la Ngorongoro una lengo la kuendelea kuhifadhi eneo hilo kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vizazi vijavyo.

Akizunguma katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongela amewahahakikishia wanadiplomasia nchini kuwa zoezi hilo lilihusisha wananchi wa jumuiya zote waliokuwa wakiishi katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro na kuahidi kuwa majadiliano bado yanaendelea ili kuhakikisha wananchi wote wanakuwa na uelewa wa pamoja katika suala hilo na hivyo kufanikisha utekelezaji wa azma ya uhifadhi wa hifadhi ya Ngorongoro.

Mkutano huo uliohusisha viongozi waandamizi wa Serikali kutoka Wizara za mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Maliasili na Utalii, Katiba na Sheria pamoja na Wakuu wa Mikoa ya Arusha na Tanga.

Mkutano huo ulilenga kuwafahamisha wanadiplomasia walioko nchini juu ya utekelezaji wa mpango wa Serikali wa kuhama kwa hiari kunakofanywa na wananchi waliokuwa na makazi ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro na hivyo kuondoa sintofahamu iliyokuwepo kuwa wananchi hao wanahamishwa kwa nguvu na serikali na hivyo kukiuka haki za binadamu.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani) kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza katika kikao na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani) kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja akizungumza na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani) kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Naibu katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akimkaribisha Waziri wa mambo ya Nje kuzungumza na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani) kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Balozi wa Visiwa vya Comoro Nchini, Dkt. Ahmada El Badaoui Mohammed  akitoa salamu za shukrani baada ya kikao kati ya Serikali na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani)

Mkurugenzi wa Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga akiwakaribisha Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa katika mkutano

Mkurugenzi wa Diaspora, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi James Bwana akifuatilia mkutano kati ya Serikali na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa

Balozi wa Ufaransa Nchini,  Mhe. Nabil Hajlaoui akichangia katika kikao kati ya Serikali na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini (hawapo pichani) kuwaelezea mpango wa Serikali katika kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro

Baadhi ya Mabalozi katika picha ya pamoja na meza kuu baada ya kikao kati ya Serikali na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini 



Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola kukutana Rwanda

Na Mwandishi Maalum Kigali, Rwanda

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola hatimaye unafanyika jijini Kigali, Rwanda baada ya kuahirishwa mara mbili (2020 na 2021) kwa sababu ya ugonjwa wa Corona.

Mkutano huo unaofanyika kuanzia tarehe 20 hadi 25 Juni 2022 umegawanywa katika makundi mbalimbali kama vile ya vijana, wanawake, wafanyabiashara, Mawaziri wa Mambo ya Nje, Wakuu wa Nchi pamoja na matukio ya pembezoni ambayo kwa pamoja mijadala yake inajikita katika maeneo matano.

Maeneo hayo ni utawala bora, utawala wa sheria, haki za binadamu; vijana, afya, teknolojia na uvumbuzi; maendeleo endelevu na mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.

Mkutano huo unaofanyika kwa kaulimbiu “Kufikia Mustakabali wa Pamoja: Kuunganisha, Kufanya uvumbuzi, Kufanya mabadiliko” (Delivering a Common Future: Connecting, Innovating, Transforming) umejipanga kujadili na kutafutia ufumbuzi wa changamoto zinazozikabili nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola ili kufikia maendeleo ya kweli katika nyanja zote.

Tanzania inashiriki kikamilifu katika mkutano huo na kimsingi masuala yanayojadiliwa yanakwenda sanjari na vipaumbele vya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Ikumbukwe, Rais Samia tangu aingie madarakani, Serikali yake imejipambanua katika kuheshimu haki za binadamu na kuzingatia masuala ya utawala wa sheria na demokrasia. Serikali ya awamu ya sita pia inafanya jitihada mbalimbali zenye lengo la kuyawezesha makundi maalum ya wanawake, vijana na wazee kiuchumi pamoja na kuhakikisha kuwa huduma za afya zinaboreshwa na zinapatikana kwa wananchi wote.

Aidha, mageuzi makubwa ya kiuchumi yameshuhudiwa katika Serikali ya awamu ya sita na uwekezaji mkubwa katika elimu na elimu ya ufundi unaendelea kufanyika` kwa lengo la kuchochea ubunifu bila kusahau mikakati madhubuti ya kukabiliana na madiliko ya tabianchi.


: Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais-Ikulu, Dkt. Moses Kusiluka (katikati waliokaa), Balozi wa Tanzania nchini, Uingereza, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro na Mkurugenzi wa  Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Robert Kahendaguza wakiwa katika picha ya pamoja na vijana kutoka Tanzania wanaoshiriki Jukwaa la Vijana
kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.


Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro (mwenye kilemba) akiongea jambo wakati vijana kutoka Tanzania wanaoshiriki Jukwaa la Vijana katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola walipotembelea Ofisi za Balozi wa Tanzania nchini Rwanda. kulia kwa Balozi Migiro ni Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais-Ikulu, Dkt. Moses Kusiluka na anayefuatia     ni Mkurugenzi wa  Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Robert Kahendaguza.

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro akimsikiliza mmoja wa vijana kutoka Tanzania wanaoshiriki Jukwaa la Vijana katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Zanzibar, Mhandisi Zena Said na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro wakiwa katika kikao cha maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.

Viongozi wa Tanzania wakiwa katika kikao cha maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.


Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Mhe. Meja Jenerari Richard Makanzo akiwa katika picha ya pamoja na vijana kutoka Tanzania wanaoshiriki Jukwaa la Vijana
kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola unaofanyika Kigali, Rwanda tarehe 20 hadi 25 Juni 2022.

 

Monday, June 20, 2022

WAZIRI MULAMULA APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO BALOZI WA JAPAN

Na Mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) amepokea nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Japan nchini, Mhe. Misawa Yasushi leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Akipokea nakala ya hati hizo, Balozi Mulamula amemhakikishia Balozi huyo mteule ushirikiano wakati wote katika utekelezaji wa majukumu yake hapa nchini.

“Nakuhakikishia ushirikiano kutoka Serikalini wakati wote, naamini tutaendelea kushirikiana katika kukuza na kuendeleza ushirikiano baina yetu kwa masahi ya pande zote mbili kwani uhusiano wa Tanzania na Japan ni wa muda mrefu na umekuwa imara katika kipindi chote,” amesema Balozi Mulamula

Naye Balozi Mteule wa Japan nchini Mhe. Misawa Yasushi amesema atahakikisha uhusiano kati ya Tanzania na Japan unaimarika zaidi na kukua kwa ushirikiano baina ya nchi hizi kupitia nyanja za biashara na uwekezaji na hivyo kunufaisha pande zote mbili. 

“Tanzania na Japan zitaendelea kushirikiana kufanya biashara na uwekezaji kwa maslahi ya nchi zote mbili,” amesema Balozi Yasushi.

Katika tukio jingine, Balozi Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wa China anayeshughulikia masuala ya Afrika, Bw. Wu Peng katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Pamoja na mambo mengine, Waziri Mulamula na mgeni wake, walijadili namna ya kuendelea kuimarisha maeneo ya ushirikiano katika sekta za afya, elimu, bishara na uwekezaji, nishati, miundombinu na usafirishaji.

Bw. Peng ameahidi kuwa China itaendelea kushirikiana na Tanzania na kuhakikisha inafanikisha mipango yake ya maendeleo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akipokea Nakala ya Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Japan nchini Mhe. Misawa Yasushi leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi Mteule wa Japan nchini Mhe. Misawa Yasushi katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Itifaki Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Yusuph Mdolwa (katikati), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Caesar Waitara pamoja 
Mkurugenzi wa Mawasiliano Serikalini Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga wakifuatilia uwasilishaji wa nakala za hati za utambulisho za Balozi mteule wa Japan nchini Mhe. Misawa Yasushi


Maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Afisa kutoka Ubalozi wa Japan nchini wakifuatilia uwasilishaji wa nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mteule wa Japan nchini Mhe. Misawa Yasushi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akimueleza jambo Mkurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wa China anayeshughulikia masuala ya Afrika, Bw. Wu Peng katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wa China anayeshughulikia masuala ya Afrika, Bw. Wu Peng akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (hayupo pichani) katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Picha ya pamoja 



   


Saturday, June 18, 2022

WAZIRI MULAMULA AZUNGUMZA NA UONGOZI WA CHAMA CHA WAFANYABIASHARA WA NORWAY NA AFRIKA NA UONGOZI WA MFUKO WA MAENDELEO WA NORWAY


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula ametembelea ofisi za Makao Makuu ya Mfuko wa Maendeleo wa Norway (NORFUND) na kuzungumza na uongozi wa mfuko huo pamoja na uongozi wa Chama cha ushirikiano wa Wafanyabiashara kati ya Norway na Nchi za Afrika (NABA) tarehe 17 Juni 2022 jijini Oslo, Norway.
Katika ziara yake nchini Norway Waziri Mulamula amekutana na taasisi hizo za maendeleo ili kuona namna ya kuboresha sekta za ushirikiano zilizopo kati ya Norway na Tanzania na kuleta manufaa kiuchumi kwa pande zote mbili.



Sehemu ya uongozi wa Chama cha ushirikiano wa Wafanyabiashara kati ya Norway na Nchi za Afrika na Mfuko wa Maendeleo wa Norway wakifatilia mazungumzo ambapo waneonesha nia ya kuongeza maeneo ya ushirikiano ili kuleta tija zaidi katika soko la kimataifa na kuboresha miundombinu wenzeshi.

Mhe. Waziri Mulamula akipokelewa na viongozi wa Chama cha ushirikiano wa Wafanyabiashara kati ya Norway na Nchi za Afrika na Mfuko wa Maendeleo wa Norway.

Picha ya pamoja na viongozi wa NABA na NORFUND.

Sehemu ya Ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo, kutoka kushoto ni Bi. Tunsume Mwangolombe na wa pili kushoto ni Bw. Seif Kamtunda.

Mazungumzo yakiendelea, Kutoka kulia Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga na Afisa Mambo ya Nje Bi. Kisa Doris Mwaseba.

Picha ya pamoja Mhe. Waziri Mulamula na Mkurugenzi wa NABA, Bw. Eivind Fjeldstad (kulia) na Mkurugenzi wa NORFUND Bw. Tellef Thorleifsson (kushoto).

WAZIRI MULAMULA AFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA NORWAY

Waziri wa mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. BaloziLiberata Mulamula amefanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway, Mhe. Anniken Huifeldt katika ofisi za Wizara hiyo tarehe 17 Juni 2022  jijini Oslo, Norway.

Mazungumzo ya mawaziri hao yalihusu juu ya kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo mbili mathalan katika diplomasia, siasa na uchumi.

Pamoja na hayo masuala mengine yaliyojadiliwa kwenye mazungmzo hayo ni pamoja na umuhimu wa kufanyika kwa mageuzi ya kiuchumi ili kuwa na maendeleo jumuishi kwa wananchi wote, uhuru wa kisisasa na uhuru wa kuongea ili kuruhusu ushirikishwaji kwa makundi yote katika jamii hususan wanawake na vijana.

Aidha, nchi za Tanzania na Norway zitaendelea kushirikiana katika masuala ya afya ili kupunguza vifo vya uzazi, vifo vya watoto na masuala mengine ya ugonjwa wa UVIKO-19.

Kadhalika viongozi hao wamejadili umuhimu wa usalama na amani katika kusaidia jamii kuinuka kiuchumi na utulivu wa kufanya shughuli za kijamii kwa maendeleo ya taifa na jamii kwa ujumla.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa kwenye mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway, Mhe. Anniken Huifeldt tarehe 17 Juni 2022 jijini Oslo, Norway. 
Waziri Mulamula yupo nchini Norway kwa ziara ya kikazi ambapo pamoja na mambo mengine viongozi hao wamezungumza juu ya kuimarisha ushirikiano wa kihistoria uliopo baina ya nchi hizo mbili ili kukuza biashara, uwekezaji na utalii.

Mazungumzo yakiendelea kati ya Mhe.  Waziri Mulamula na Mhe.Anniken Huifeldt
 

Kutoka kushoto Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano katika Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga na Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Seif Kamtunda wakifuatilia mazungumzo.

Kutoka kulia Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme, Afisa Ubalozi Norway, Bi. Tunsume Mwangolombe na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Kisa Doris Mwaseba wakifuatilia mazungumzo.

Wakibadilishana zawadi.

Picha ya pamoja Mhe. Waziri Mulamula (kati), Balozi wa Tanzania nchini Norway mwenye makazi yake nchini Sweden, Mhe. Grace Alfred Olutu  (wa tatu kulia), Balozi wa Norway nchini Tanzania, Mhe. Elisabeth Jacobsen (wa tatu kushoto) pamoja na ujumbe ulioambana na Mhe. Waziri kutoka Wizarani.


TANZANIA NA NORWAY KUANZISHA USHIRIKIANO KATIKA MASUALA YA BUNGE

Serikali ya Tanzania na Norway zimeahidi kuanzisha ushirikiano katika masuala ya Bunge kufuatia ziara ya kikazi ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika Bunge hilo tarehe 17 Juni 2022 jijini Oslo, Norway.

Kufuatia ziara hiyo Mhe. Balozi Mulamula na ujumbe wake walipata fursa ya kukutana na Wajumbe wa Kamati ya Mambo ya Nje na Ulinzi wa Bunge la Norway.

Mhe. Mulamula na Wajumbe wa Kamati ya Mambo ya Nje na Ulinzi walijadili kuhusu umuhimu wa ushirika kwa vyama vya siasa na madhara ya chuki na uhasama, umuhimu wa kupigania na kujenga amani na umuhimu wa maridhiano kwa vyama kunapotokea tofauti.

Masuala mengine yaliyojadiliwa ni pamoja na ulinzi na usalama katika ukanda wa Afrika na Ukanda wa Ulaya pamoja na madhara mbalimbali yanayosababishwa na migogoro inayoendelea duniani.

Hata hivyo, Waziri Mulamula ametumia wasaha huo kujadili na kamati hiyo juu ya changamoto mbalimbali zinazoendelea ulimwenguni na madhara yake kwa nchi na jamii kwa ujumla. Ameiomba Norway kuendele kufadhili Mfuko wa Afya, na kushukuru kwa michango mbalimbali kutoka katika hiyo mathalan msaada wa mapambano juu ya homa ya UVIKO-19.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiongea na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ulinzi ya Norway alipofanya ziara katika Bunge hilo tarehe 17 Juni 2022 jijini Oslo, Norway. 

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ulinzi wa Bunge la Norway wakijadili juu ya kuimarisha ushirikiano kati ya Bunge la Norwaya na Bunge la Tanzania.

Mazungumzo yakiendelea.

Mhe. Waziri Mulamula na Ujumbe wake wakifuatilia mazungumzo.



Mazungumzo yakiendelea.


WAZIRI MULAMULA AFANYA ZIARA KATIKA KAMPUNI YA EQUINOR YA NCHINI NORWAY

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amefanya ziara katika Makao Makuu ya Kampuni ya Equinor ya nchini Norway inayojishughulisha na utafiti na uchimbaji wa mafuta na gesi tarehe 17 juni 2022 jijini Oslo, Norway.

Akizungumza na uongozi wa kampuni hiyo Waziri mulamula amewahakikishia kuwa Serikali ya Awamu ya Sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ipo tayari kushirikiana nao katika uwekezaji wa sekta ya gesi utaofanyika mkoani Mtwara. Hivyo ni wakati sasa mipango ya utekelezaji wa mradi huo ulioingiwa makubaliano ukawekewa mkazo zaidi.

Waziri mulamula amesema kwakuwa mradi huo baada ya kukamilika unategemewa kuwa wa kwanza kwa ukubwa barani Afrika hivyo ni fursa ya ajira kwa watanzania na italeta suluhu ya changamoto za nishati sambamba na kupunguza matatizo yaliyopo sasa.

Hivyo, ametoa rai kwa kampuni ya Equinor kuweka bajeti ya kujenga uwezo kwa watanzania ili waweze kuwa sehemu ya utekelezaji wake kwa kushiriki kazi za kitaalamu zitakazowawezesha kupata uzoefu kwaajili ya miradi mingine kama hiyo

Naye Makamu wa Rais wa Kampuni ya Equinor, Ms. Unni Merethe Skorstad alieleza kuwa kampuni yake mpaka sasa imetoa zaidi ya nafasi 1000 za ufadhili za masomo katika vyuo vikuu vya nchini Tanzania ambavyo ni pamoja na chuo Kikuu cha Dodoma, Chuo Kikuu cha Zanzibar na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Baadhi ya wahitimu waliofadhiliwa na kampuni hiyo wameajiriwa na sekta za nishati za nchini Tanzania na Nje ya Nchi ikiwemo Norway na wengine wameajiriwa kufundisha katika vyuo walivyosoma.

Huduma nyingine za kijamii zinazotolewa na Kampuni ya Equinor kwa Tanzania kufuatia kuingiwa makubaliano ya uchimbaji wa gesi mkoani Mtwara ni pamoja na; kujengea uwezo juu ya uelewa wa mradi huu na manufaa yake kwa jamii itakayozunguka mradi na taifa kwa ujumla, kusaidia sekta ya elimu, afya na kuwajengea uwezo wafanyakazi katika sekta ya nishati hususani katika mafuta na gesi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa kampuni ya Equinor alipotembelea Makao Makuu ya kampuni hiyo tarehe 17 Juni 2022 jijini Oslo, Norway.

Makamu wa Rais wa Kampuni ya Equinor, Ms. Unni Merethe Skorstad akiwatambulisha kwa Mhe. Waziri Mulamula vijana wa kitanzania walioajiriwa katika kampuni ya Equinor na katika vyuo vya Norway katika fani ya mafuta na gesi.



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na uongozi wa kampuni ya Equinor ya nchini Norway.

Makamu wa Rais wa Kampuni ya Equinor, Ms. Unni Merethe Skorstad na Mshauri Maalum wa Mawasiliano wa Kampuni ya Equinor, Bw. Tarjei Skirbekk wakiwa katika mazungumzo na Mhe. Waziri Mulamula.

Uongozi wa Kampuni ya Equinor ukifatilia mazungumzo.

Sehemu ya ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mazungumzo.

Mazungumzo yakiendelea.

Picha ya pamoja Mhe. Waziri Mulamula na watanzania wanaofanya kazi katika kampuni ya Equinor.

TANZANIA NA NORWAY ZAWEKA MSISITIZO KUKUZA DIPLOMASIA YA UCHUMI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Norway zaweka msisitizo wa kuimarisha ushirikiano kwenye Diplomasia ya Uchumi ili kuinua shughuli za maendeleo kwa mataifa hayo na kuboresha huduma kwa jamii.

Hayo yamesemwa wakati wa mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Norway, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim. Mazungumzo hayo yamefanyika tarehe 17 Juni 2022 wakati wa ziara ya Mhe. Mulamula nchini Norway.

Waziri Mulamula alieleza kuwa Tanzania kupitia sera yake ya taifa na sera ya mambo ya nje imeweka mipango imara ili kuhakikisha inainua sekta za uzalishaji hususani sekta ya kilimo, biashara na utalii. Hivyo, maeneo hayo ni ya kipaumbele kwenye ushirikiano wake na mataifa mengine.  

Hata hivyo, Tanzania kupitia sekta ya kilimo inaweza  kuzalisha mazao ya biashara na hivyo kuongeza nafasi ya ajira kwa vijana sambamba na kuinua wanawake kiuchumi. Pia katika suala hilo akafafanua umuhimu wa kuwawezesha wanawake kwani wamekuwa mstari wa mbele kuzalisha mashambani na kuwa tegemeo kwa chakula cha familia na malezi kwa ujumla. 

Aidha, akafafanua umuhimu wa ushirikishwaji na kujenga uwezo kwa makundi hayo mawili sambamba na uwezeshaji katika teknolojia ili kuyafikia malengo ya kitaifa ya uzalishaji na kuyafikia masoko ya bidhaa ya kimataifa.

Naye Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Norway alieleza kuwa Serikali yake kwasasa imeelekeza ushirikiano na mataifa mengine katika biashara badala ya utoaji wa misaada. Mabadiliko haya ni sehemu ya jitihada katika kuhakikisha mataifa rafiki ya Norway yanapiga hatua kiuchumi kwa manufaa ya pande zote mbili za ushirikiano.

Kadhalika, Mhe.Tvinnereim  alipongeza kwa jitihada zinazofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuboresha utendaji kazi. Moja ya mafanikio ya wazi katika hilo alisema ni kufikiwa kwa makubaliano kati ya serikali na Kampuni ya Equinor ya Norway inayojishughulisha na utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi.

Pia akaongeza kusema Norway inafurahishwa na mikakati iliyowekwa na Serikali ya Awamu ya Sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kukuza uchumi wa bluu na kwamba ipo tayari kushirikiana katika hilo ili kuyafikia malengo yaliyowekwa kwakuwa inao uzoefu mkubwa katika sekta hiyo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) amefanya mazungumzo na Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Norway, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim katika ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje ya Norway tarehe 16 Juni 2022 jijini Oslo, Norway. Waziri Mulamula yupo nchini Norway kwa ziara ya kikazi itakayomalizika tarehe 18 Juni 2022.

Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Norway, Mhe. Anne Beathe Tvinnereim akizungumza na Mhe. Balozi Mulamula  katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje ya Norway tarehe 16 Juni 2022 jijini Oslo, Norway.
Kutoka kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Norway mwenye makazi yake nchini Sweden, Mhe. Grace Alfred Olutu, Mkurugenzi Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga na Afisa Mambo ya Nje, Bi Kisa Doris Mwaseba wakifuatilia mazungumzo.

Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme, Afisa Ubalozi, Bi. Tunsume Mwangolombe na Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Seif Kamtunda wakifuatilia mazungumzo.

Mazungumzo yakiendelea, Mhe. Tvinnereim na ujumbe wake.

Mhe. Tvinnereim akimkabidhi zawadi ya kitabu cha Diplomasia, Mhe. Balozi Mulamula.