Saturday, June 18, 2022

WAZIRI MULAMULA AFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA NORWAY

Waziri wa mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. BaloziLiberata Mulamula amefanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway, Mhe. Anniken Huifeldt katika ofisi za Wizara hiyo tarehe 17 Juni 2022  jijini Oslo, Norway.

Mazungumzo ya mawaziri hao yalihusu juu ya kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo mbili mathalan katika diplomasia, siasa na uchumi.

Pamoja na hayo masuala mengine yaliyojadiliwa kwenye mazungmzo hayo ni pamoja na umuhimu wa kufanyika kwa mageuzi ya kiuchumi ili kuwa na maendeleo jumuishi kwa wananchi wote, uhuru wa kisisasa na uhuru wa kuongea ili kuruhusu ushirikishwaji kwa makundi yote katika jamii hususan wanawake na vijana.

Aidha, nchi za Tanzania na Norway zitaendelea kushirikiana katika masuala ya afya ili kupunguza vifo vya uzazi, vifo vya watoto na masuala mengine ya ugonjwa wa UVIKO-19.

Kadhalika viongozi hao wamejadili umuhimu wa usalama na amani katika kusaidia jamii kuinuka kiuchumi na utulivu wa kufanya shughuli za kijamii kwa maendeleo ya taifa na jamii kwa ujumla.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa kwenye mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway, Mhe. Anniken Huifeldt tarehe 17 Juni 2022 jijini Oslo, Norway. 
Waziri Mulamula yupo nchini Norway kwa ziara ya kikazi ambapo pamoja na mambo mengine viongozi hao wamezungumza juu ya kuimarisha ushirikiano wa kihistoria uliopo baina ya nchi hizo mbili ili kukuza biashara, uwekezaji na utalii.

Mazungumzo yakiendelea kati ya Mhe.  Waziri Mulamula na Mhe.Anniken Huifeldt
 

Kutoka kushoto Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano katika Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga na Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Seif Kamtunda wakifuatilia mazungumzo.

Kutoka kulia Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme, Afisa Ubalozi Norway, Bi. Tunsume Mwangolombe na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Kisa Doris Mwaseba wakifuatilia mazungumzo.

Wakibadilishana zawadi.

Picha ya pamoja Mhe. Waziri Mulamula (kati), Balozi wa Tanzania nchini Norway mwenye makazi yake nchini Sweden, Mhe. Grace Alfred Olutu  (wa tatu kulia), Balozi wa Norway nchini Tanzania, Mhe. Elisabeth Jacobsen (wa tatu kushoto) pamoja na ujumbe ulioambana na Mhe. Waziri kutoka Wizarani.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.