Thursday, June 2, 2022

SERIKALI NA KAMPUNI YA LONGPIN WAKUBALIANA KUHARAKISHA UWEKEZAJI KATIKA KILIMO CHA SOYA


Viongozi,Watendaji na Maafisa Waandamizi wa Serikali wamekutana na kufanya mazungumzo na Watendaji wa Kampuni ya Longping High Tech ya China inayotarajia kuwekeza katika kilimo cha soya nchini. Mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ofisi ya Wizara ya Kilimo jijini Dodoma yalilenga kujadili namna ya kuharakisha utekelezaji wa mradi huo. 

Akizungumza katika mkutano huo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Antony Mavunde amesema kuwa Serikali inashauku kubwa kuona uwekezaji huu ambao unaenda kuwainua wakulima wadogo kiuchumi, unaanza kutekelezwa mapema iwezekanavyo. Naibu Waziri mavunde aliongeza kuwa kwa upande wa serikali tayari imeshaweka mazingira mazuri na rafiki ya kuhakikisha kuwa mradi huu unatekelezwa kwa mafanikio nchini. 

“Pamoja na mambo mengi muhimu tuliyofanya ili kuharakisha uwekezaji huu wa kuongeza uzalishaji na ubora wa soya nchini, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo kwa kuanzia imetenga takriban hekari 27000 ambazo zitatumika katika uzalishaji wa mbegu za soya” Alisema Naibu Waziri Mavunde.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Longping High Tech Bw. Liang Shi ameeleza kuwa baada ya ziara waliyoifanya katika maeneo mbalimbali nchini wamepata mwamko zaidi wa kuanza uwekezaji haraka iwezekavyo.

“Katika kipindi tulichokuwepo hapa nchini tumetembelea maeneo mbalimbali tumeona ardhi na hali ya hewa nzuri kwa uzalishaji wa soya, utayari wa wakulima na zaidi utayari wa Serikali katika kupokea uwekezaji wetu ambao pamoja masuala mengine unatoa uhakika wa soko la soya za wakulima. Tumefarijika na kuhamasika zaidi hivyo tuna ahidi uwekezaji wetu utaanza mara moja”. Amesema Bw. Shangyang Wu

Watendaji wa Kampuni ya Longping High Tech wamekuwepo nchini kwa kipindi cha takribani wiki mbili ambapo wametembelea maeneo mbalimbali ikiwemo Ruvuma, Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma, Iringa, Njombe, Mbeya, Rukwa na Katavi kwa lengo la kuangalia maeneo ya uzalishaji wa soya sambamba na kuonana na kufanya mazunguzmo na wadau katika sekta hiyo. 
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Antony Mavunde akizungumza wakati wa kikao baina ya Viongozi,Watendaji na Maafisa Waandamizi wa Serikali na Watendaji wa Kampuni ya Longping High Tech ya China kilichofanyika katika ofisi ya Wizara hiyo jijini Dodoma.
Balozi wa Tanzania nchini Brazil Mhe. Balozi Prof. Adelardus Kirangi akizungumza wakati wa kikao baina ya Viongozi, Watendaji na Maafisa Waandamizi wa Serikali na Watendaji wa Kampuni ya Longping High Tech ya China kilichofanyika katika ofisi ya Wizara hiyo jijini Dodoma.
Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki akizungumza wakati wa kikao baina ya Viongozi, Watendaji na Maafisa Waandamizi wa Serikali na Watendaji wa Kampuni ya Longping High Tech ya China kilichofanyika katika ofisi ya Wizara hiyo jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Biashara za Nje na Fedha wa Kampuni hiyo Bw. Shangyang Wu akizungumza kwenye kikao baina ya Viongozi, Watendaji na Maafisa Waandamizi wa Serikali na Watendaji wa Kampuni ya Longping High Tech ya China kilichofanyika katika ofisi ya hiyo jijini Dodoma.
Mkutano ukiendelea
Mkutano ukiendelea
Viongozi,Watendaji, Maafisa Waandamizi wa Serikali, wadau kutoka sekta binafsi na Watendaji wa Kampuni ya Longping High Tech ya nchina China wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mkutano uliofanyika katika ofisi ya Wizara ya Kilimo jijini Dodoma

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.