Tuesday, June 14, 2022

WAZIRI MULAMULA AKUTANA NA UONGOZI WA OFISI YA MPANGO WA USIMAMIZI WA MIGOGORO (CMI) YA NCHINI FINLAND

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiongea na uongozi wa Ofisi ya Mpango wa Usimamizi wa Migogoro tarehe 13 Juni 2022 kwenye Makao  Makuu ya taasisi hiyo nchini Finland. Mazungumzo yao yalijikita kwenye masuala ya amani na usalama katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika. Pia Mhe. Waziri akaeleza amani na usalama wa ukanda huo ni kipaumbele kwakuwa huziwezesha nchi kupata utulivu wa kufanya shughuli za maendeleo na kuinua uchumi wa Taifa na maisha ya wananchi kwa ujumla.

Kutoka kushoto ni Naibu Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Usimamaizi wa Migogoro, Bi. Hanna Klinge na Mkuu wa Mpango huo Kusini mwa Jwangwa la Sahara, Bi.Tiina Kukkamaa-Bah akitoa taarifa ya utekelezaji wa mipango mbalimbali  katika taasisi hiyo, hususani katika ukanda wa Kusini mwa Afrika na Afrika Mashariki.


Mazungumzo yakiendelea, Kulia kwa Mhe. Waziri ni Balozi wa Tanzania nchini Finland mwenye makazi yake nchini Sweden, Mhe. Grace Alfred Olutu na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga wakifuatilia mazungumzo

Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na America katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Tunsume Mwangombole wakifuatilia mazungumzo

Picha ya pamoja

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.