Tuesday, June 28, 2022

BALOZI MULAMULA APOKEA ZAWADI PICHA KUTOKA SERIKALI YA CHINA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akipokea zawadi ya picha kutoka kwa Bw. Ahmed Salim mtoto wa Dkt. Salim Ahmed Salim ambaye alikabidhiwa na Serikali ya China ikiwa ni ishara ya kuutambua mchango wa Dkt. Salim ulioiwezesha China kurejesha kiti cha Kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mwaka 1971

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (kushoto) akizungumza na  Bw. Ahmed Salim (katikati) mtoto wa Dkt. Salim Ahmed Salim ambaye alifika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kumkabidhi zawadi ya picha iliyotolewa  na Serikali ya China ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wa Dkt. Salim ulioiwezesha China kurejesha kiti cha Kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mwaka 1971


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) amepokea zawadi ya picha kutoka Serikali ya China ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wa Dkt. Salim Ahmed Salim ulioiwezesha nchi hiyo kurejesha kiti cha kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mwaka 1971.

Zawadi hiyo ya picha imekabidhiwa na Mtoto wa Dkt. Salim Ahmed Salim Bw.  Ahmed Salim katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Bw. Ahmed amesema zawadi ya picha iliyotolewa na Serikali ya China inaonesha picha za Dkt. Salim katika vikao vya Umoja wa Mataifa, alama na nembo za Serikali ya China ambazo zinaonesha heshima ya nchi hiyo kwa Dkt. Salim.

 




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.