Thursday, June 9, 2022

MKUTANO WA SADC WA WIZARA ZINAZOSHUGHULIKIA MASUALA YA JINSIA WAFANYIKA MALAWI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ameongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao cha ngazi ya Makatibu Wakuu wa Wizara zinazoshughulikia masuala ya Jinsia na Wanawake kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kilichofanyika hivi karibuni jijini Lilongwe, Malawi.


Pamoja na mengineyo, kikao hicho kilijadili masuala mbalimbali yakiwemo; Maboresho ya Program za SADC za masuala ya Jinsia kwa mwaka 2021/2022; Mpango wa Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi katika nyanja mbalimbali za Kikanda; Utekelezaji wa Mkakati wa Kikanda wa SADC; Mfumo wa Kukabiliana na Unyanyasaji wa Kijinsia wa mwaka 2018-2030; Wanawake katika Siasa na nafasi za maamuzi na hatua kuelekea Usawa wa Kijinsia kwenye Sekretarieti ya SADC.

Kikao hili kitafuatiwa na Mkutano wa Kamati ya Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Jinsia na Wanawake wa Nchi Wanachama wa SADC. 


 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Zaynab  Chaula akishiriki Kikao cha Makatibu Wakuu wa Wizara zinazoshughulikia masuala ya Jinsia kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)  kilichofanyika hivi karibuni Lilongwe - Malawi. Wengine katika picha ni ujumbe wa Tanzania ulioshiriki mkutano huo. Pichani ni Balozi Agnes R. Kayola, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Grace Mwangwa, Mkurugenzi Msaidizi na Bw. Timotheo Mgonja, Afisa Mkuu kutoka Idara ya Maendeleo ya Jamii, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.

Picha ya pamoja ya wajumbe walioshiriki  
Kikao cha Makatibu Wakuu wa Wizara zinazoshughulikia masuala ya Jinsia kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)  kilichofanyika hivi karibuni Lilongwe - Malawi.hicho

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Zaynab  Chaula  akizungumza jambo na Bi. Roselyn Makhumula, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jinsia, Watoto, Watu wenye Ulemavu na Ustawi wa Jamii wa Jamhuri ya Malawi ambaye pia ni Mwenyekiti katika kikao hicho cha Makatibu Wakuu.


 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.