Thursday, June 16, 2022

WAZIRI MULAMULA AFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA FINLAND


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula amefanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Finland, Mhe. Pekka Haavisto pembezoni mwa  Mkutano wa 19 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Afrika na Nordic uliofanyika tarehe 13 hadi 15 Juni 2022 jijini Helsinki, Finland.

Serikali ya Tanzania na Finland zinashirikiana katika masuala ya ubunifu wa kutengeneza ajira, usimamizi wa fedha kwa taasisi za umma, kujenga uwezo kwenye masuala ya kodi pamoja na utawala bora.
Maeneo mengine ya kipaumbele katika ushirikiano huo ni pamoja na elimu,kuinua ubia kati serikali na sekta binafsi, kuhamasisha uwekezaji, umarishaji wa demokrasia na utawala wa sheria na kukuza biashara. 
Balozi wa Tanzania nchini Finland mwenye makazi yake nchini Sweden, Mhe. Grace Alfred Olutu na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga wakifuatilia mazungumzo.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Finland, Mhe. Pekka Haavisto akieleza utayari wa Serikali ya Finland katika kuimarisha ushirikiano wa kihistoria uliopo baina ya Serikali yake na Tanzania.
Ujumbe ulioambatana na Mhe. Haavisto ukifuatilia mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.