Saturday, June 18, 2022

TANZANIA NA NORWAY KUANZISHA USHIRIKIANO KATIKA MASUALA YA BUNGE

Serikali ya Tanzania na Norway zimeahidi kuanzisha ushirikiano katika masuala ya Bunge kufuatia ziara ya kikazi ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika Bunge hilo tarehe 17 Juni 2022 jijini Oslo, Norway.

Kufuatia ziara hiyo Mhe. Balozi Mulamula na ujumbe wake walipata fursa ya kukutana na Wajumbe wa Kamati ya Mambo ya Nje na Ulinzi wa Bunge la Norway.

Mhe. Mulamula na Wajumbe wa Kamati ya Mambo ya Nje na Ulinzi walijadili kuhusu umuhimu wa ushirika kwa vyama vya siasa na madhara ya chuki na uhasama, umuhimu wa kupigania na kujenga amani na umuhimu wa maridhiano kwa vyama kunapotokea tofauti.

Masuala mengine yaliyojadiliwa ni pamoja na ulinzi na usalama katika ukanda wa Afrika na Ukanda wa Ulaya pamoja na madhara mbalimbali yanayosababishwa na migogoro inayoendelea duniani.

Hata hivyo, Waziri Mulamula ametumia wasaha huo kujadili na kamati hiyo juu ya changamoto mbalimbali zinazoendelea ulimwenguni na madhara yake kwa nchi na jamii kwa ujumla. Ameiomba Norway kuendele kufadhili Mfuko wa Afya, na kushukuru kwa michango mbalimbali kutoka katika hiyo mathalan msaada wa mapambano juu ya homa ya UVIKO-19.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiongea na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ulinzi ya Norway alipofanya ziara katika Bunge hilo tarehe 17 Juni 2022 jijini Oslo, Norway. 

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ulinzi wa Bunge la Norway wakijadili juu ya kuimarisha ushirikiano kati ya Bunge la Norwaya na Bunge la Tanzania.

Mazungumzo yakiendelea.

Mhe. Waziri Mulamula na Ujumbe wake wakifuatilia mazungumzo.



Mazungumzo yakiendelea.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.