Saturday, July 9, 2022

WAZIRI MULAMULA: WAFANYABIASHARA CHANGAMKIENI FURSA ZA MASOKO KATIKA JUMUIYA ZA KIKANDA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula ametoa rai kwa Wafanyabiashara wa Tanzania kuchangamkia fursa za masoko zinazopatikana katika Jumuiya za Kikanda ambazo Tanzania ni mwanachama kama vile Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na fursa zitokanazao na Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA)

Waziri Mulamula ametoa rai hiyo wakati akizungumza na wafanyanyabisha kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba “Bukoba Expo" yaliyofanyika katika Viwanja ya CCM mjini Bukoba. Maonesho hayo yaliyobebwa na kauli mbiu isemayo “Biashara, viwanda na utalii ni fursa ya uwekezaji Mkoani Kagera”.

Akizungumza na wafanyabiashara wakati wa akifunga maonesho hayo Waziri Mulamula alieleza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan inayo dhamira ya dhati ya kukuza uchumi wa nchi kupitia biashara na uwekezaji kwa kudumisha ushirikiano na nchi jirani na kutafuta fursa za masoko kwa bidhaa zinazozalishwa nchini. Aliongeza kusema wakati Serikali inafanya hayo ni vyema sekta binafsi ikaunga mkono juhudi hizo za Serikali kwa kuchangamkia fursa za masoko zinazopatikana katika Jumuiya za Kikanda ili kujiongezea tija zaidi katika shughuli zao. 

"Mtakumbuka kuwa Tanzania pamoja na kuwa mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki pia ni mwanachama wa SADC na hivi karibuni tumeridhia mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (Africa Continental Free Trade Area-AfCFTA). Eneo Huru la Biashara la Afrika ni soko kubwa kuliko masoko yote yaliyoanzishwa ulimwenguni kwa kuwa na uwingi wa nchi wanachama zinazofikia 55. Soko hili linakadiriwa kuwa na idadi ya watu wapatao Bilioni 1.3 na Pato ghafi la Taifa (GDP) lenye jumla ya Dola za Marekani trilioni 3.4 na fursa za uchumi unaokua kwa kasi". Alieza Waziri Mulamula

Akizungumzia kuhusu maonesho hayo Waziri Mulamula ameleeza kuwa ubunifu wa waandaji umeakisi maono ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha Mkoa wa Kagera na wananchi wake wanapata maendeleo kwa kushiriki kikamilifu katika shughuli za uchumi, biashara na uwekezaji kwa kutumia fursa zilizopo katika Mkoa huo na nafasi ya Kijiografia ya Mkoa kwa kupakana na nchi za Rwanda, Burundi na Uganda.

Kwa upande wake mratibu na mwandaaji wa Maonesho ya Bukoba Bw. William Rutta ameeleza kuwa maonesho hayo ambayo yamewavutia washiriki zaidi ya 350 wakiwemo wajasiliamari, wafanyabiashara, Taasisi za serikali na washiriki kutoka nchi za Burundi, Uganda, na Congo yametembelewa na wateja zaidi ya 10,000.

Aidha Bw. Rutta amebainisha malengo ya amonesho hayo kuwa ni pamoja na kuweka mwendelezo wa wiki ya uwekezaji ya Kagera ya mwaka 2019, kuunganisha wafanyabiashara na wananchi wote kushiriki katika shughuli za kuzalisha, mali, kuendeleza utalii na kubadilishana teknolojia ya uzalishaji na kuhamasisha utalii kwa kuandaa safari katika mbuga za wanyama asili za Burigi, Ibanda kyerwa, Runanyika Karagawe, Hifadhi ya Rubondo, Seregeti na vivutio vya asili kama fukwe za ziwa Victoria. Lengo lingine ni uboreshaji wa mazingira kwa kuhamasishwa upandaji miti aina ya palm tree katika mji wa Bukoba.

Waziri Mulamula kwenye maadhimisho ya kilele cha maonesho hayo pamoja na wajumbe wengine aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Meja Jenerali, Charles Mbuge, Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Moses Machali na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera Bi. Costansia Guhiye.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na mmoja wa washiriki wa Maonesho ya Bukoba 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (aliyevalia kilemba) na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Meja Jenerali Charles Mbuge akiwa katika picha ya pamoja Waandaaji wa Maonesho ya Kagera na Washiriki wa maonesho hayo. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Moses Machali alipowasili kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba yaliyofanyika katika viwanja vya CCM Bukoba mjini
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi cheti cha kufanyavizuri mmoja wa washiriki wa Maonesho Bukoba kutoka nchini Burundi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza hadhira iliyojitokeza kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha na mmoja wa washiriki wa Bukoba Expo mzalishaji wa bidhaa za mafuta ya asili ya ngozi
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akipokelewa katika viwanja vya CCM mjini Bukoba alipowasili kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba “Bukoba Expo”.
Meza kuu wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea kwenye madhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwasili kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba “Bukoba Expo” yaliyofanyika katika viwanja vya CCM Bukoba mjini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na mmoja wa washiriki wa Maonesho ya Bukoba
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiangalia bidhaa za mmoja wa washiriki wa Bukoba Expo 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Mati Super Brands Ltd Bw. Living Munishi kwenye maadhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifurahia jambo baada zoezi la upandaji mti kwenye madhimisho ya kilele cha Maonesho ya Bukoba

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA NSSF ZAJADILI FURSA ZA UWEKEZAJI NJE YA NCHI

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine amefanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii - NSSF, Bw. Masha Mshomba tarehe 8 Julai 2022 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.


Viongozi hao wamejadili juu ya umuhimu wa kukuza na kuimarisha ushirikiano baina ya Wizara na mfuko huo wa NSSF.  


Pamoja na mambo mengine viongozi hao wamezungumzia kuhusu uwekezaji kwenye viwanja vya Serikali nje ya nchi ili kuona namna ambavyo Wizara na NSSF wanaweza kushirikiana katika miradi ya ujenzi wa ofisi na vitega uchumi.


Aidha, Balozi Sokoine akaeleza kuwa Serikali ina miliki viwanja zaidi ya 40 kwenye maeneo ya uwakilishi nje ya nchi, hivyo akatoa rai kwa taasisi hiyo kushirikiana na Wizara katika kuviendeleza kwa kujenga majengo ya Ofisi za Balozi pamoja na vitega uchumi ili kuipunguzia Serikali gharama ya kupanga lakini zaidi  kupata faida kutokana na vitega uchumi hivyo.


Naye Bw. Mshomba aliafiki wazo hilo la uwekezaji na kueleza kuwa  NSSF imeshakuwa na mipango ya miradi ya uwekezaji nje ya nchi hivyo, wazo hilo limekuja wakati mwafaka na kwamba NSSF inaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita za kufungua mipaka hususan katika sekta ya biashara na uwekezaji.


Aidha, Kikao hicho kiliridhia kuundwa kwa timu ya Wataalamu kutoka katika pande zote mbili ili kuruhusu kufanyika kwa tathmini ya kina juu ya uwekezaji huo na faida zake ili kuweza kuwa na miradi ya pamoja na Wizara wenye tija kwa Taifa.


======================================


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Joseph Sokoine (kulia) amefanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii - NSSF, Bw. Masha Mshomba tarehe 8 Julai 2022 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii - NSSF, Bw. Masha Mshomba (wa pili kulia) akiwa katika mazungumzo na Balozi Joseph Sokoine (hayupo pichani) katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.
 Kulia ni Mkurugenzi wa Mipango na Utawala - NSSF, Bw. Gabriel Silayo na wa tatu kutoka kulia ni Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma - NSSF, Bi. Lulu Mengele.

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sera na Mipango, Bw. Justin Kisoka akifafanua juu ya uwekezaji wa miradi ya pamoja na namna Wizara na NSSF zinavyoweza kushirikiana katika kutathmini uwekezaji kwenye maeneo ya miradi.

Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi James Bwana na kulia ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara hiyo wakifuatilia mazungumzo.

Picha ya pamoja

 


Friday, July 8, 2022

WIZARA YAAHIDI KUALIKA WASHIRIKI WENGI ZAIDI WA NJE KATIKA MAONESHO YA SABASABA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk N. Mbarouk amesema kuwa Wizara pamoja na balozi zake, itaendelea kuhamasisha nchi marafiki na mashirika ya kimataifa kushiriki maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) ambayo amesema yanazidi kuimarika ukilinganisha na miaka ya nyuma.

Kauli hiyo ameitoa leo tarehe 08 Julai 2022 alipotembelea maonesho hayo yanayofanyika kwenye viwanja vya Julius Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar Es Salaam.

Balozi Mbarouk amesema kuwa kushiriki kwa wageni wengi kutoka nje ya nchi, kuna faida kubwa kwa wafanyabiashara wa hapa nyumbani, kwa kuwa kuna wapa fursa ya kujifunza teknolojia mpya, kupata masoko ya bidhaa wanazozizalisha na wabia wa kushirikiana nao katika biashara na uwekezaji.

Akiwa kwenye viwanja hivyo, Mhe. Naibu Waziri alitembelea mabanda mbalimbali ya washiriki wa maonesho hayo, hususan wale wa kutoka nje ya nchi ili kujionea bidhaa, huduma na teknolojia walizokuja nazo. Katika maongezi na washiriki hao alisisitiza umuhimu wa kubadilishana teknolojia na uzoefu na wafanyabiashara wa hapa nchini ili kujenga uwezo wa kuzalisha bidhaa bora zitakazokuwa na uwezo wa kukabili ushindani wa soko la dunia.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Joseph Sokoine aliahidi kuwa Wizara yake itashirikiana na wadau wengine kama Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TANTRADE) na Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wengi zaidi kutoka nje ya nchi wanashiriki maonesho hayo. “Wizara yetu ni mdau mkubwa katika utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi na maonesho ni jukwaa muhimu katika diplomasia ya uchumi, hivyo tutaongeza nguvu zaidi kushajihisha kampuni nyingi zaidi kutoka nje, zishiriki maonesho haya mwakani na miaka mingine”, Alisema Balozi Sokoine.

Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya mwaka 2022 yalianza tarehe 28 Juni na yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 13 Julai 2022 ambapo nchi 20 zinashiriki kwa kuoenesha bidhaa, huduma na teknolojia mbalimbali.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisaini Kitabu cha Wageni baada ya kuwasili katika Bnada la Wizara ya Mambo ya Nje lilipo katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba). Aliyesimama ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akipewa maelezo kuhusu ushiriki wa Wizara katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akiwa katika moja ya banda yaliyopo kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba)
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisikiliza maelezo ya mshiriki wa Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) kutoka nje ya nchi
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje wanaoshiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba)


KATIBU MKUU KATIKA MAONESHO YA SABASABA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akiwa kwenye viwanja vya Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) kwa ajili ya kutembelea mabanda mbalimbali kujionea bidhaa, huduma na teknolojia..

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akisaini Kitabu cha Wageni baada ya kuwasili katika Bnada la Wizara ya Mambo ya Nje lilipo katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba).

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akipewa maelezo kuhusu ushiriki wa Wizara katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akisalimiana na Balozi wa Marekani hapa nchini ambaye alifika kutembelea 

Bnada la Wizara ya Mambo ya Nje lilipo katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba).

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje wanaoshiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba

 

Thursday, July 7, 2022

UONGOZI WA CCM MKOANI KAGERA WAPONGEZA UTENDAJI WA WAZIRI MULAMULA

Uongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kagera wamempongeza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya ya kuimarisha Uhusiano wa Kidiplomasia baina ya Tanzania na Mataifa mengine ulimwenguni sambamba na kutekeleza vyema diplomasia ya uchumi. 

Haya yamesemwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera Bi. Costansia Guhiye wakati wa mazungumzo yaliyofanyika baina ya Viongozi wa Chama wa Mkoa huo na Waziri Mulamula alipotembelea Ofisi Kuu ya Chama Mkoa wa Kagera mjini Bukoba.

Katika mazungumzo hayo Waziri Mulamula alitoa rai kwa viongozi hao kuendelea kuwahamasisha na kuwahimiza wananchi wa Mkoa wa Kagera kuchangamkia fursa zinazopatika katika Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kama vile biashara na fursa za kufundisha Kiswahili zinazopatikana katika Nchi wanachama wa Jumuiya. 

Sambamba na hayo Waziri Mulamula amepongeza jitihada zinazofanywa na viongozi hao katika kulea na kukuza Chama, kuhamasisha amani, maendeleo, umoja na mshikamano kwa wananchi wa Mkoa huo. Aidha amewatakia maandalizi mema ya uchaguzi wa Chama unaotarajiwa kufanyika katika siku za usoni. 

Waziri Mulamula amewasili Mkoani Kagera leo tarehe 7 Julai 2022 ambapo anatarijiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya kilekile cha Monesho ya Bukoba “Bukoba Expo” tarehe 8 Julai 2022 yanayofanyika katika viwanja vya CCM mjini humo. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Uongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kagera 
Kuotaka kushoto, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera Bi. Costansia Guhiye, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Katibu wa CCM Mkoa wa Kagera Ndugu Christopher Paranjo wakifurahia jambo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa CCM Mkoa wa Kagera.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Uongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kagera 
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera Bi. Costansia Guhiye akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo baina ya Uongozi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera na Waziri Mulamula
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Ofisi Kuu ya Chama Mkoa wa Kagera mjini Bukoba
Katibu wa CCM Mkoa wa Kagera Ndugu Christopher Paranjo akielezea jambo wakati wa mazungumzo baina ya Uongozi wa Chama cha Mapinduzi wa Mkoa huo na Waziri Mulamula

DIPLOMASIA KUENDELEA KUWA CHACHU YA KUKUZA NA KUBIDHAISHA KISWAHILI DUNIANI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango ametoa rai kwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuweka jitihada za makusudi za kukikuza Kiswahili nje ya mipaka ya Tanzania.

Rai hiyo imetolewa wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa Leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Mhe. Mpango akiwa Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo ameeleza kuwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeendelea kubeba jukumu la kizalendo ambapo, kupitia Balozi zake ilifanikiwa kushawishi majukwaa ya kimataifa kuitambua lugha ya Kiswahili na kupewa siku ya kuadhimishwa duniani ambayo inafanyika leo kwa mara ya kwanza.

“Ninatoa pongezi kwa Balozi zetu kwa jitihada wanazofanya za kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili, nimeona mitandaoni jinsi Balozi zilivyojitoa kufanya makongamano na midahalo ya Kiswahili katika kusherehesha siku hii” alisema Mhe. Mpango.

Pamoja na kutolewa kwa pongezi kwa Wizara, Mhe. Mpango ametoa pongezi za kipekee kwa Mabalozi wa Tanzania wanaowakilisha Jijini New York, Marekani, Mhe. Kennedy Gaston; Addis Ababa, Ethiopia, Mhe. Innocent Shio na Paris, Ufaransa, Mhe. Samuel Shelukindo kwa kukamilisha mchakato wa kutambulika kwa Kiswahili duniani.

Aidha, uwepo wa siku maalum ya kuadhimishwa lugha ya Kiswahili duniani kukupa nguvu ikiwa ni lugha rasmi ya kazi katika Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na kufanya jumuiya nyingine ambazo Tanzania ni mwanachana kuipa upekee lugha ya Kiswahili.

Naye Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na Mwakilishi wa kudumu katika Umoja wa Afrika, Mhe. Balozi Innocent Shio ameeleza kuwa lugha ya Kiswahili ina nafasi kubwa katika kukuza na kuimarisha mtangamano kwa maendeleo ya Afrika kwakuwa, mawasiliano huleta amani na kuongeza mshikamano.

Pia, akaeleza wakati huu ambapo Umoja wa Afrika unaenda kutathmini Agenda 2030 na kutekeleza kikamilifu Agenda 2063 ya Umoja huo ni wakati sasa wa kukibidhaisha kiswahili ili kuunganisha mataifa ya Afrika na kuweza kuyafikia malengo ya mpango wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCTA) katika kukuza sekta za kiuchumi na kuinua pato la Wananchi na Taifa kwa ujumla.

“Lugha ni bidhaa hivyo ni muhimu kusimamia kikamilifu soko lake ili kuleta fursa zinazotarajiwa, mathalan ajira kwa Walimu, Wakarimali, huduma ya kutafsiri, utangazaji, uandishi wa vitabu vya Kiswahili, Sanaa ya uigizaji na uhariri” alisema Balozi Shio.

Tarehe 23 Novemba 2021, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) lilitangaza Siku Maalumu ya Kiswahili Duniani inayoadhimishwa tarehe 7 Julai kila mwaka.

Sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani, zimeandaliwa na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo na kuhudhuriwa na Viongozi wa Wizara, Taasisi, Idara, sekta binafsi na taasisi ya za elimu nchini na Wananchi.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akihutubia wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Elimu wa Afrika Kusini, Mhe. Matsie Angelina Motshekga akihutubia wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika tarehe 7 Julai 2022 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mhe. Motshekga ameeleza kuwa Serikali ya Afrika Kusini ipo tayari kuingiza somo la lugha ya kiswahili katika shule za msingi na hivyo itaendelea kuhitaji usaidizi wa vitabu na maboresho ya mitaala kwa ajili ya kufundishia.

Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na Mwakilishi wa Kudumu katika Umoja wa Afrika, Mhe. Innocent Shio akihutubia kwenye sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Fatma Rajab (aliyeshika bendera) akifuatilia sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Kushoto ni aliyekuwa Balozi wa Tanzania na Mwakilishi wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa, Balozi Modest Mero na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bi Ellen Maduhu wakifuatilia sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Kushoto Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda na Waziri wa Elimu wa Afrika Kusini, Mhe. Matsie Angelina Motshekga wakitia saini makubaliano ya kuanza kufundisha kiswahili katika elimu ya msingi nchini Afrika Kusini.

Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Mpango akimshukuru Naibu Waziri wa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mabarouk Nassor Mbarouk baada ya kumlizika kwa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na Mwakilishi wa Kudumu katika Umoja wa Afrika, Mhe. Innocent Shio akipokea tuzo ya ngao kutoka kwa Waziri wa Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mhe. Mphamed Mchengerwa kwenye sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Hafla ikiendelea.


Viongozi wa meza kuu wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa na wa Afrika Mashariki ukipigwa kwenye sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kitaifa leo tarehe 7 Julai 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Waziri Wizara  ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk.

Picha ya pamoja meza kuuna viongozi Wakuu wa Wizara, Taasisi na Idara za Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) 

 

DKT. MWINYI AZISIHI NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI KUBUNI MBINU ZA KUENEZA KISWAHILI

Na Mwandishi wetu, Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amezisihi nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kubuni mbinu bora za kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili katika ukanda huo na duniani kwa ujumla.

Dkt. Mwinyi ametoa wito huo wakati akifunga Kongamano la Kiswahili Duniani lililoanza jana na kuhitimishwa leo Zanzibar ambapo amezisihi nchi wanachama wa Jumuiya hiyo kuhakikisha kuwa zinashirikiana na Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoa mafunzo ya Isimu na Fasishi katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuandaa mikakati madhubuti ya kuendeleza lugha ya Kiswahili Duniani.

“Natoa wito pia kwa taasisi za elimu ya juu kushirikiana na Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutumia lugha ya Kiswahili kama fursa kwa vijana wetu kwani lugha hii ni kama bidhaa,” amesema Dkt. Mwinyi.

Pamoja na mambo mengine, Dkt. Mwinyi ameihakikishia Kamisheni ya Kiswahili na Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa zitaendelea kuunga mkono jitihada za kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili duniani kote.

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote amesema Jumuiya ya Afrika Mashariki itaendelea kushirikiana na wadau wa Lugha ya Kiswahili ili kuweza kuanzisha mabaraza ya Kiswahili ikiwa ni njia moja wapo mahsusi ya kukuza na kuendeleza lugha hiyo.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine amesema kuwa ni lugha ya Kiswahili ni lugha ya kwanza kutumika katika shughuli rasmi za Umoja wa Afrika, pia ni lugha ya kwanza Afrika na ya nane duniani kuwa na siku maalum ya kuadhimishwa

“Kutumia lugha ya Kiswahili katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  kutasaidia kuongeza umoja baina ya wananchi wa ukanda huo kuliko ilivyokuwa awali na kuongeza maelewano na baina ya nchi na nchi” amesema balozi Sokoine

Balozi Sokoine ameongeza kuwa, lugha ya Kiswahili ikitumika vizuri itasaidia kuimarisha ushirikiano kati ya wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika masuala mbalimbali yakiwemo masuala ya kisiasa, biashara, uchumi, elimu utamaduni na ustawi wa jamii.

Pamoja na mambo mengine, Balozi Sokoine amezisisi nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Masahriki kuongeza kasi ya kutangaza na kuhamasisha matumizi ya lugha ya Kiswahili katika shughuli zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki” 

Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Zanzibar (BAKIZA), Dkt. Mwanahija Ali Juma amezisihi nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhakikisha kuwa wanakuza na kuendeleza matumizi ya lugha ya Kiswahili kwa kuanzisha mabaraza ya Kiswahili

Dkt. Mwanahija ameongeza kuwa njia nyingine ya kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili ni pamoja na nchi wanachama kuungana pamoja na Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kufanya tafiti za kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili.

Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani limehudhuriwa na nchi wanachama sita kutoka ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jamhuri ya Kenya, Jamhuri ya Rwanda, Jamhuri ya Burundi, Jamhuri ya Rwanda na Jamhuri ya Sudani kusini.

Novemba 23, 2021 Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) lilitangazwa rasmi kuwa tarehe 7 Julai ya kila mwaka ni siku maalumu ya kuadhimisha Siku ya Kiswahili Duniani. Vilevile, Februari 2022, Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika katika Mkutano wake wa kawaida wa 35 walipitisha Kiswahili kama Lugha ya Kazi na mawasiliano mapana Barani Afrika.

Aidha, Mwezi Septemba, 2022 Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa  ulianza kuitangaza na kuisamba lugha ya Kiswahili, nchini Ufaransa kwa kushirikiana na Chama cha Watanzania Ufaransa (CCWU), ambapo ulianza kutoa mafunzo ya lugha ya Kiswahili kwa mwaka wa masomo 2021/22, ambayo yaliendeshwa na Kituo cha Utamaduni na Lugha cha Kitanzania (CCLT).

Washiriki wa matembezi kutoka ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakionesha baadhi ya Bendera za nchi wananchama wa Jumuiya hiyo wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika leo Zanzibar




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akipokelewa na viongozi mbalimbali alipowalisi kuhitimisha Kongamano la Kiswahili Duniani leo Zanzibar

   
Washiriki wa Kongamano la Kiswahili Duniani wakifuatilia Hotuba ya Rais wa Zanzibaar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wa kufunga kongamano hilo leo Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwasilisha Hotuba yake wakati wa kuhitimisha Kongamano la Kiswahili Duniani leo Zanzibar

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote akitoa hotuba yake katika Kongamano la siku ya Kiswahili Duniani lililohitimishwa leo Zanzibar



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali waliohudhuria Kongamano la Kiswahili Duniani leo Zanzibar