Sunday, September 4, 2022

WAJUUMBE WA KAMATI YA NUU WATEMBELEA MIRADI YA KIKANDA YA EAC



Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia Mipango, Miundombinu, Fedha na Utawala, Mhandisi Steven Mlote akiongea jambo wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) ilipotembelea Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mshariki jijini Arusha kabla ya kuanza kutembelea miradi ya miundombinu ya EAC inayotekelezwa mkoani humo. Mwingine katika picha ni Mwenyekiti wa Kamati ya NUU, Mhe. Vita R. Kawawa

Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akiwasilisha mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC kwa wajumbe wa Kamati ya NUU jijini Arusha.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) wakifuatilia kwa makini mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) wakifuatilia kwa makini mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota.

Mwenyekiti wa Kamati ya NUU, Mhe. Vita R. Kawawa akichangia hoja baada ya kuwasilishwa mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya NUU, Mhe. Vicent Mbogo akichangia hoja baada ya kuwasilishwa mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC

Mjumbe wa Kmati ya NUU, Mhe. Janeth Masaburi akichangia jambo kuhsu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC

Waheshimiwa Wajumbe wa Kamati ya NUU na wajumbe wengine wakisikiliza mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya kikanda ya miundombinu ya EAC

Wajumbe wa Kamati ya NUU wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Vita Kawawa wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia Mipango, Miundombinu, Fedha na Utawala, Mhandisi Steven Mlote pamoja na watumishi wengine wa Serikali mbele ya Jengo la Makao Makuu ya EAC.

Mwenyekiti wa Kamati ya NUU, Mhe. Vita R. Kawawa akipokelewa na watumishi wa Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga, mara baada ya kuwasili na kamati yake katika kituo hicho kwa ajili ya kuangalia utendaji wa Kituo.

Meneja wa Mamlaka ya Mapato wa Mkoa wa Arusha, Bw. Paul Kamukulu akifafanua jambo kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga kwa wajumbe wa Kamati ya NUU walipotembelea kituo hicho tarehe 03 Septemba 2022.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Lungido, Bw. Kamana Juma Simba akitambulisha ujumbe wa Wilaya yake ulioshiriki katika ziara ya wajumbe wa Kamati ya NUU katika Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga

Meneja wa Mamlaka ya Mapato wa Mkoa wa Arusha, Bw. Paul Kamukulu akisoma taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga kwa wajumbe wa Kamati ya NUU
Afisa kutoka Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii, Bw. Imail Abdalla akifanya majumuisho ya ziara ya Kamati ya NUU katika miradi ya miundombinu ya EAC iliyofanyika kuanzia tarehe 02 hadi 04 Septemba 2022 

Wajumbe wa Kamati ya NUU wakisikiliza majumuisho ya ziara yao kutoka kwa Afisa kutoka Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii, Bw. Imail Abdalla

Mjumbe wa Kamati ya NUU, Bw. Cosato Chumi akijumuika na wajasiriamali wanaofanya biashara maeneo ya kuzunguka Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga



Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mahariki, Bw. Justin Kisoka akijumuika na wajasiriamali wanaofanya biashara maeneo ya kuzunguka Kituo cha Pamoja cha Mpakani cha Namanga

Picha ya pamoja






 

Friday, September 2, 2022

BALOZI MULAMULA AIHAKIKISHIA JUMUIYA YA KIMATAIFA UTAYARI WA TANZANIA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akiwa katika meza kuu wakati wa hafla ya ufungaji wa Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam . Mkutano huo uliandaliwa kwa pamoja na Serikali ya Tanzania na Uingereza na kushirikisha wajumbe kutoka nchi 20 . 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifunga Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam. 

 

Bw. Matt Toombs kutoka Uingereza  akizungumza katika hafla ya ufungaji wa Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam.


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri wa Nchi Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) akimpa mkono wa pongezi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula baada ya kufunga Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam.

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akishukuru baada ya kufunga Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam.

 

Baadhi ya washiriki wa Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam wakifuatilia hotuba ya ufungaji wa mkutano huo iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamulahayupo pichani


Baadhi ya washiriki wa Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam wakifuatilia hotuba ya ufungaji wa mkutano huo iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamulahayupo pichani


 

 

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula ameihakikishia jumuiya ya Kimataifa utayari na ushiriki thabiti wa Tanzania katika jitihada za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

 

Balozi Mulamula ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam wakati wa kufunga Mkutano  wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo ulioandaliwa kwa pamoja na Serikali ya Tanzania na Uingereza na kushirikisha wajumbe kutoka nchi 20 .

 

“Tanzania iko tayari na itaendelea kuwa mshiriki thabiti wa jitihada za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, na niwahakikishie kwamba Tanzania ni muumini wa ushirikiano wa kimataifa katika kulinda na kuhifadhi mazingira kama nguzo kanuni na miongozo ya Umoja wa Mataifa inavyosema,” alisema Balozi Mulamula.

 

 

Balozi Mulamula pia amesema Tanzania ni muumini wa ushirikiano wa kimataifa kama nguzo ya kulinda mazingira sambamba na maadili na miongozo ya Umoja wa Mataifa inavyosema.

 

Ametumia nafasi hiyo kuwasihi wajumbe wa mkutano huo na mikutano mingine kama hiyo kuhakikisha wanakuwa na ajenda moja itakayosaidia harakati za dunia katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi duniani.

 

Awali akitoa maelezo mafupi kuhusu mkutano huo Bw. Matt Toombs kutoka Uingereza alisema washiriki wa mkutano huo wamejadili maeneo mblimbali yanayohusiana na  utunzaji wa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi na kukublina kuendelea kushirikiana na jumuiya ya kimataifa kuona namna ya kuweza kukbiliana na changamoto hiyo.

  

Mkutano huo wa Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo ulioandaliwa na Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano na Serikali ya Uingereza na kushirikisha zaidi ya nchi 20 duniani ulianza tarehe 1 Septemba na kufunguliwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo kwa niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango


VACANCY ANNOUNCEMENT AT THE COMMONWEALTH SECRETARIAT


 

BALOZI MULAMULA AKUTANA NA MKURUGENZI MKAZI WA IOM




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa na Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji (IOM) Bw. Maurizio Busatti ambaye alifika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha rasmi.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza na Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji (IOM) Bw. Maurizio Busatti ambaye alifika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha rasmi.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza na Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji (IOM) Bw. Maurizio Busatti ambaye alifika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha rasmi.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza na Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji (IOM) Bw. Maurizio Busatti ambaye alifika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha rasmi.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza na Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji (IOM) Bw. Maurizio Busatti ambaye alifika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha rasmi.



mazungumzo yakiendelea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) katika picha ya pamoja na Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji (IOM) Bw. Maurizio Busatti na maafisa walioshiriki mazungumzo hayo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha rasmi.

 

 

 

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) amekutana na kuzungumza na Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji (IOM) Bw. Maurizio Busatti ambaye amejitambulisha rasmi kwa Mhe. Waziri katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

 

Akizungumza katika kikao hicho Waziri Mulamula ameipongeza IOM kwa kazi inazofanya nchini na amemuhakikishia Bw. Busatti kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kufanya kazi na Shirika hilo.

 

Amesema Shirika hilo (IOM limekuwa mstari wa mbele kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika masuala ya wakimbizi, majanga ya asili na kuongeza kuwa ni matumaini yake kwamba Bw. Busatti ataendeleza uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na IOM kwa kuzingatia uzoefu wa muda mrefu alionao kwa kufanya kazi kwa muda mrefu ndani ya shirika hilo.

 

 

Balozi Mulamula ameipongeza IOM kwa kuendelea na shughuli za kuwarejesha nyumbani rai awa Ethiopia waliokuwa katika magereza nchini na kuongeza kuwa kitendo hicho kimesaidia Tanzania kukabiliana na msongamano wa watu katika magereza yake.

 

Ameipongeza IOM na jitihada zake za kukijengea uwezo kituo cha mafunzo cha maafisa Uhamiaji Kanda ya Afrika kilichoko ndani ya Kituo cha mafunzo cha Maafisa Uhamiaji cha mjini Moshi ambapo pia maafisa uhamiaji wa Tanzania wananufaika nacho.

 

Naye Bw. Busatti ameishukuru Serikali kwa jinsi inavyoshirikiana na Shirika hilo katika kutekeleza majukumu yake hapa nchini.

 

Bw. Busattia ameahidi kuendeleza ushirikiano mzuri ambao shirika hilo umekuwa na Serikali ya Tanzania kwani imekuwa mdau wake mkubwa katika kufanikisha majukumu yake.

 

Thursday, September 1, 2022

BALOZI FATMA: WATUMISHI FANYENI KAZI KWA BIDII, USHIRIKIANO

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab amewasihi watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Qatar kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na kwa ushirikiano mkubwa ili kuiwezesha Serikali kufikia malengo yake iliyojiwekea. 

Balozi Fatma ametoa maelekezo hayo wakati alipokutana na watumishi wa Ubalozi katika kikao kazi kilichofanyika katika ofisi za ubalozi Jijini Doha, Qatar na kuwataka kufanya kazi kwa bidii, ubunifu, weledi na uaminifu kwa kuzingatia maslahi mapana ya Taifa.

"Nawasihi kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano pamoja na kuwa wabunifu wa kuitangaza lugha ya Kiswahili, pamoja na Filamu ya Roya Tour, pamoja na vipaumbele vya Serikali hasa katika kutekeleza Diplomasia ya Uchumi," amesema Balozi Fatma.

Kwa upande wake Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Bi. Patricia Kiswaga amemhakikishia Balozi Fatma kuwa watafanya kazi kwa umoja, bidii, weledi na ubunifu kwa maslahi mapana ya Taifa.

Pamoja na mambo mengine, Bi. Kiswaga ameongeza kuwa ushirikiano kati ya Tanzania na Qatar ni mzuri na unaendelea kuimarika kila wakati.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akizungumza na watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Qatar katika kikao kazi kilichofanyika katika ofisi za ubalozi huo Jijini Doha, Qatar 

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akizungumza na watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Qatar katika kikao kazi kilichofanyika katika ofisi za ubalozi huo Jijini Doha, Qatar 



Wednesday, August 31, 2022

KAMATI YA NUU YARIDHISHWA NA MIKAKATI YA UTEKELEZAJI WA DIPLOMASIA YA UCHUMI




Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akisoma taarifa ya Mikakati ya Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU)

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akiendelea kusoma taarifa ya Mikakati ya Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) huku wajumbe hao wakimsikiliza kwa makini.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), Mhe. Victor Kawawa akisema jambo wakati wa kikao kati ya Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU). 

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) wakifuatilia kwa makini taarifa ya Mikakati ya Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi iliyokuwa ikiwasilishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), Mhe. Alexander Pastory Mnyeti akichangia jambo katika kikao hicho

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), Mhe. Cosato Chumi akichangia jambo katika kikao hicho

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), Mhe. Ali Hassan Omar King akichangia jambo katika kikao hicho
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akinukuu hoja za Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU)

Kaimu Mkurugenzi wa  Idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Justin Kisoka akifafanua jambo wakati wa  kikao kati ya Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU)

Mkurugenzi wa  Kitengo cha Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi James Bwana akifafanua jambo wakati wa  kikao kati ya Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU)
Kaimu Mkurugenzi wa  Idara ya Diplomasia ya Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw.Magabilo Murobi akifafanua jambo wakati wa  kikao kati ya Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU)
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) 
walioshiriki kikao kati ya Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kamati hiyo.
Baadhi ya Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioshiriki kikao kati ya Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kamati ya NUU.
Sehemu ya Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioshiriki kikao kati ya Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kamati ya NUU.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Taasisi, Idara na Vitengo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioshiriki kikao kati ya Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kamati ya NUU.