Thursday, April 20, 2023

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI YASHIRIKI UFUNGUZI WA MICHEZO YA MAADHIMISHO YA MEI MOSI


Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wanaoshiriki katika michezo inayoendelea mjini Morogoro wameungana na maelfu ya wafanyakazi wenzao kushiriki katika sherehe ya ufunguzi wa tamasha la michezo kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani (Mei Mosi) yatakayofanyika Kitaifa mjini Morogoro.

Ufunguzi huo uliofanyika katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro umefanywa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Fatma Abubakar Mwassa na kuhudhuriwa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa Serikali na Vyama vya Wafanyakazi nchini.

Mhe. Mwassa akihutubua wafanyakazi waliojitokeza katika uwanja wa Jamhuri ametoa wito kwa Watumishi kuendeleza utamaduni wa kufanya mazoezi ili kuongeza ukakamavu na kupunguza uwezekano wa kuugua magonjwa yasiyo ambukizwa kama inavyoshauriwa na Wataalamu wa Afya. 

“Michezo ni afya, michezo ni furaha, michezo ni urafiki hivyo naendelea kusisitiza Wafanyakazi kuendeleza utamaduni wa kufanya mazoezi kama ambavyo sera inavyohimiza ilikuongeza utimamu wa mwili na akili. Mfanyakazi anayezingatia michezo au mazoezi hata ufanisi wake kazini huwa nimzuri zaidi” ameeleza Mhe. Mwassa

Sherehe za ufunguzi wa tamasha hilo lilishindikizwa na michezo na burudani mbalimbali ambapo Viongozi waliohudhuria uwanjani hapo akiwemo Mhe. Prof. Joyce Ndalichako Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenyeulemavu walipata nafasi ya kujionea ujuzi, ukakamavu na umahiri wa watumishi katika michezo.

Kwa upande wake Timu ya Wanawake ya mpira wa pete ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Nje Sports) ilicheza dhidi ya timu ya Mahakama ya Tanzania mbapo Timu ya Mahakama imeibuka na ushindi wa magoli 37 dhidi 3 

Timu ya mpira wa pete ya Nje Sports imeendelea kuwa na mwenendo wa kusua sua katika mashindano hayo ambapo Kiongozi wake Bi. Pili Rajabu ameeleza kuwa uwepo kwa majeruhi wengi katika kikosi chake kinaifanya timu hiyo kutokuwa katika nafasi nzuri ya ushindani hivyo kupoteza michenzo mingi wanayoshiriki.
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye maandamano wakati wa sherehe za ufunguzi wa michezo kuelekea maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Wafanyakazi duniani yatakayofanyika Kitaifa mjini Morogoro

Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye maandamano yaliyofanyika katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro kuelekea maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Wafanyakazi duniani yatakayofanyika Kitaifa mjini Morogoro



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Abubakar Mwassa akihutubia watumishi waliojitokeza katika uwanja wa Jamhuri mkoani humo kwenye sherehe za ufunguzi wa michezo kuelekea maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Wafanyakazi duniani (Mei Mosi).
Bi. Pili Rajab (mwenye mpira) mchezaji wa Nje Sports akiwatoka walinzi wa  Time ya Mahakama ya Tanzania katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Jamhuri.  Timu ya Mahakama iliibuka na ushindi wa magoli 37 - 3 katika mchezo huo.




Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakila kiapo cha utiifu katika michezo ya kuelekea maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Wafanyakazi duniani yatakayofanyika Kitaifa mjini Morogoro 

TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA NCHI ZA EAC KULINDA RASILIMALI ZA UVUVI ZIWA VICTORIA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe aliyeongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu akizungumza katika Mkutano huo uliofanyika tarehe 19, Aprili jijini Kampala, Uganda.

Makatibu Wakuu ambao ni Wajumbe wa Kamati ya Uratibu ya Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika tarehe 19, Aprili jijini Kampala, Uganda.


Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu ukifuatilia Mkutano huo

Ujumbe wa Uganda (kushoto) na ujumbe wa Tanzania (kulia) katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu ukifuatilia Mkutano huo

Washiriki wa Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu wakifuatilia Mkutano huo.  

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe aliyeongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu akipongezana na Kaimu Mkurugenzi Miundombinu ya Kiuchumi na Huduma za Kijamii Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Judith Ngoda baada ya kumalizika kwa Mkutano huo uliofanyika tarehe 19, Aprili jijini Kampala, Uganda.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe aliyeongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu baada ya kumalizika kwa Mkutano huo uliofanyika tarehe 19, Aprili jijini Kampala, Uganda.


 

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhakikisha rasilimali za uvuvi katika Ziwa Victoria zinalindwa ili zinufaishe jamii zinazozunguka ziwa hilo na mataifa husika kwa ujumla.

 

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe aliyeongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika tarehe 19, Aprili jijini Kampala, Uganda.

 

Prof. Shemdoe aliuhakikishia mkutano huo kuwa, Tanzania itaendelea kuchukua hatua madhubuti za kusimamia ziwa hilo kama nchi wanachama wa wa LVFO zilivyokubaliana. Alisisitiza pia kuwa Tanzania inaendelea kudhibiti matumizi ya zana haramu za uvuvi, kupiga marufuku uvuvi wa samaki wachanga, kudhibiti utoroshaji wa mazao ya uvuvi na kuhamasisha ufugaji wa samaki kwa vizimba katika Ziwa Victoria bila kuathiri mazingira.

 

Amesema pia, Tanzania imeimarisha udhibiti wa uingizaji wa zana za kuvulia samaki ili kuzuia uingizaji wa zana haramu nchini na kuendesha ukaguzi wa kina ili kuhakikisha uvuvi endelevu unafanyika kwa tija.

 

Pia Profesa Shemdoe alitanabaisha kuwa mchango wa Sekta za Uvuvi katika uchumi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ni mdogo sana kwakuwa mchango wake unahesabiwa katika maeneo ya uvuvi na ukuzaji bila kujumuisha mapato yanayotokana na shughuli zote zinazofanyika katika minyororo yake ya thamani.

 

“Mchango wa Sekta za Uvuvi katika uchumi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ni mdogo sana kwakuwa mchango wake unahesabiwa katika maeneo ya uvuvi na ukuzaji bila kujumuisha mapato yanayotokana na shughuli zote zinazofanyika katika minyororo yake ya thamaniBadala yake thamani hiyo inajumuishwa katika sekta zingine na hivyo kutokutoa picha halisi ya Sekta ya Uvuvi,” alisema.

 

Katika mkutano huo, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uganda, Dkt. Aziz Mlima, alimwakilisha Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo.

 

Kikao hiki kimehudhuriwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zilizopo katika Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa

 

 

 






 



Wednesday, April 19, 2023

WATANZANIA WALIOPO SUDAN WAPO SALAMA: DKT. TAX


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) akitoa Taarifa ya Serikali kuhusu Hali ya Amani na Usalama nchini Sudan Bungeni jijini Dodoma, tarehe 19 Aprili 2023 

 

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kuchukua hatua stahiki kwa kushirikiana na nchi jirani, Jumuiya za Kikanda, Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa ili kuhakikisha watanzania na raia wengine waliopo nchini Sudan wanakuwa salama wakati huu ambapo nchi hiyo ipo katika changamoto za kiusalama.

 

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax Bungeni jijini Dodoma, tarehe 19 Aprili 2023 wakati akitoa Taarifa ya Serikali kuhusu Hali ya Amani na Usalama nchini Sudan.

 

Amesema tangu kuibuka kwa mapigano mjini Khartoum tarehe 15 Aprili 2023 kati ya vikosi vya Serikali (Sudan Armed Forces - SAF) na Vikosi vya Msaada yaani Rapid Support Forces (RSF) na kusambaa katika maeneo mengine ya nchi hiyo, tayari athari mbalimbali zimeanza kujitokeza ikwemo vifo vya watu 185 majeruhi zaidi ya 1,000 na uharibifu wa mali.

 

Amesema mapigano hayo pia yamechangia kurudisha nyuma jitihada zinazoendelea za kutafuta amani Sudan na kwamba Serikali ya Tanzania inasikitishwa na kuzorota kwa hali ya amani na usalama inayoendelea nchini humo.

 

Ameongeza kusema Tanzania kama zilivyo nchi nyingine inao raia wake wapatao 210 nchini Sudan wakiwemo wanafunzi 171, wanadiplomasia na raia wengine ambao hadi sasa wapo salama na hakuna aliyeathiriwa na mapigano hayo.

 

 

Mhe. Dkt. Tax amesema kuwa, jitihada za pamoja za Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na nchi na taasisi mbalimbali zimefanikisha kusitishwa kwa mapigano nchini Sudan kwa muda wa saa 24 kuanzia tarehe 18 Aprili 2023 jioni ili kutoa nafasi kwa misaada ya kibinadamu kutolewa kwa raia.

 

Pia  Mhe. Dkt. Tax amempongeza Balozi wa Tanzania nchini Sudan, Mhe. Silima Haji Kombo kwa kuendelea kuhakikisha usalama wa watanzania waliopo Sudan na kwamba Serikali inaendelea kufuatilia hali nchini humo pamoja na kuandaa mpango wa kuwaondoa raia wa Tanzania kadri itakavyohitajika.

 

Amesema  Tanzania ambayo ni Mjumbe wa Baraza la Amani la Afrika inaendelea kuunga mkono tamko lililotolewa na Baraza hilo katika mkutano wake uliofanyika tarehe 16 Aprili 2023 la kulaani mapigano yanayoendelea na kutoa wito kwa pande zote mbili katika mgogoro huo kusitisha mapigano hayo.

 

Pia Tanzania inaendelea kuzitaka pande hizo mbili hasimu kutatua mgogoro huo kwa njia za amani na usalama huku zikihakikisha mahitaji ya kibinadamu, usalama na ustawi wa raia wa Sudana na raia kutoka nchi nyingine.

 

 

TUSAMBAZE ELIMU YA UKUZAJI VIUMBE MAJI NCHI NZIMA - BALOZI MLIMA

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Kijamii, Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Bi. Judith Ngoda (kulia) akimuelezea Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uganda Mhe. Dkt. Aziz Mlima (hayupo pichani) kuhusu Mkutano wa Tano Baraza la Mawaziri la kisekta la Uvuvi Ukuzaji Viumbe Maji la Jumuiya ya Afrika Mashariki waliofika Ubalozini kumpa taarifa kuhusu mkutano huo unaoendelea jijini Kampala, Uganda, kushoto ni Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Didas Clemence


Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uganda Mhe. Dkt. Aziz Mlima (wa pili kulia ) katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Tanzania wanaoshiriki Mkutano wa Tano Baraza la Mawaziri la kisekta la Uvuvi Ukuzaji Viumbe Maji la Jumuiya ya Afrika Mashariki waliofika Ubalozini kumpa taarifa kuhusu mkutano huo unaoendelea jijini Kampala, Uganda



 

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uganda Mhe. Dkt. Aziz Mlima ameisihi sekta ya uvuvi nchini kuangalia namna ya kufanya ili juhudi za ukuzaji viumbe maji zisambae nchi nzima.

Mhe. Balozi Mlima ametoa rai hiyo jijini Kampala alipozungumza na washiriki wa Mkutano wa Tano Baraza la Mawaziri la kisekta la Uvuvi Ukuzaji Viumbe Maji la Jumuiya ya Afrika Mashariki waliofika Ubalozini kumpa taarifa kuhusu mkutano huo unaoendelea jijini Kamapala.

Akizungumza na wataalamu hao Mhe. Balozi Dkt. Mlima amesema sekta ya Uvuvi kupitia eneo la ukuzaji viumbe maji lazima ihakikishe programu za ufugaji samaki zinaenea katika maeneo mengine yenye maziwa na isiishie maeneo ya Ziwa Victoria pekee ili nchi itumie fursa hiyo vizuri na kunufaika nayo.

“Tanzania tuna eneo kubwa la maji lakini ufugaji wa samaki kwetu sio mzuri Inabidi tuoneshe njia, suala hili linatoa ajira na lina soko kubwa niwaambie tu kuwa bidhaa zitakazozalishwa soko liko DRC,” alisema na kuongeza kuwa Tanzania lazima kufanya ufugaji samaki kuwa suala la kimkakati.

Amesema kinachotakiwa kufanywa au kuangaliwa ni suala la kuzalisha chakula cha samaki ili kuwa na uhakika wa malisho yao na hapo mambo yataenda vizuri kwani suala la kutengeneza chakula ni kubwa na ana hakika chuo cha uvuvi na Taasisi ya Utafiti ya uvuvi wanaweza kusimamia eneo hilo.

Amesema sekta inabidi ioneshe njia na kutilia mkazo suala la ufugaji wa samaki nchini kwani ajira nyingi zitatengenezwa katika eneo hilo na kwa kuzingatia kuwa kuna soko kubwa kwa nchi jirani ya DRC na hivyo nchi itanufaika na fursa hii kuwa na mashine za uhakika za uzalishaji wa chakula cha Samaki

“Tuangalie na tufanye suala hili kimkakati hasa katika eneo la kutengeneza chakula cha samaki ni suala kubwa na la msingi, nina hakika chuo cha uvuvi na taasisi ya utafiti wakilisimamia hili tutapata mitambo ya kuzalisha chakula cha samaki.

Amesema anaona ufugaji Samaki ukizingatia masharti na vigezo vyake ni kitu rahisi kwa mwananchi kufanya kwakua changamoto pekee inayoweza kumsumbua mfugaji husika ni wizi wa mazao yake tu na kwamba akijipanga kudhibiti hilo hakuna shida nyingine kama ana uhakika wa chakula bora.

Mhe.Balozi Dkt. Mlima atashiriki katika Mkutano huo utakaofanyika tarehe 19 Aprili akimuwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo utaongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo Prof. Riziki Shemdoe kwa ngazi ya Makatibu Wakuu.






Tuesday, April 18, 2023

KAMATI KUTATHMINI UTEKELEZJI WA DIPLOMASIA YA UCHUMI YAANZA KAZI RASMI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Kamati ya Kutathmini Utendaji wa Wizara alipokutana nayo jijini Dodoma tarehe 18 Aprili 2023 kama ishara ya kuanza rasmi kwa kazi ya Kamati hiyo. Kamati hiyo ambayo iliundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 28 Machi, 2023 inao wajumbe saba (7) na inaongozwa na Balozi Msatafu, Mhe. Hassan Simba Yahya (wa kwanza kushoto)
Kikao na Kamati kikiendelea
Mwenyekiti wa Kamati ya Kutathmini utendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikianio wa Afrika Mashariki, Balozi Mstaafu, Mhe. Hassan Simba Yahya akizungumza wakati wa kikao kati ya Kamati hiyo na Mhe. Dkt. Tax
Mjumbe wa Kamati, Mhe. Balozi Mwanaidi Maajar akiwa kwenye Kikao kati ya Kamati hiyo na Mhe. Dkt. Tax. Kushoto ni Mjumbe wa Sekretarieti ya Kamati hiyo
Wajumbe wengine wa Kamati ambao ni Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi (kulia) na Balozi Peter Kalaghe wakati wa kikao kati ya kamati hiyo na Mhe. Dkt. Tax

Mjumbe wa Kamati, Mhe. Balozi Jack Mugendi Zoka (kulia) akiwa na Mjumbe wa Sekretarieti ya Kamati (kushoto)
Wajumbe wengine wa Kamati ambao ni Balozi Tuvako Manongi (kushoto) na Mhe. Balozi George Madafa wakati wa kikao kati ya Kamati na Mhe. Waziri Tax
Wajumbe wa Sekretarieti ya Kamati wakifuatilia kikao

Kikao kikiendelea

Mhe. Dkt. Tax (katikati mstari wa kwanza) akiwa katika picha ya pamoja  na Mwenyekiti wa Kamati Kutathmini utendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Simba (wa pili kushoto mstari wa kwanza) pamoja na Wajumbe wa Kamati hiyo

Mhe. Dkt. Tax (katikati mstari wa kwanza) akiwa katika picha ya pamoja  na Mwenyekiti wa Kamati ya Kutathmini utendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Simba (wa pili kushoto mstari wa kwanza), Wajumbe wa Kamati pamoja na Sekretarieti ya Kamati hiyo


STATEMENT BY THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, ON THE SECURITY SITUATION IN THE REPUBLIC OF SUDAN


 

Monday, April 17, 2023

TANZANIA - WADAU WAMAENDELEO KUENDELEA KUSHIRIKIANA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) ameeleza utayari wa Serikali ya Awamu ya Sita chini na usimamizi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wa kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo katika kuboresha maisha ya wananchi. 

Waziri Tax ameeleza hayo leo tarehe17 Aprili 2023 alipokutana na kufanya mazungumzo kwa nyakati tofauti na Balozi wa Ireland nchini Mhe. Mary O’Neill, na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Bw. Zlatan Milisic jijini Dodoma. 

Waziri Tax akizungumza Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Bw. Milisic ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka miwili ya Uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita yamefayika madiliko na maboresho makubwa yanayolenga kukuza Demokrasia na Utawala Bora na Haki za Binadamu. 

Waziri Tax sambamba na kumshukuru Bw. Malisic kwa kuendelea kusaidia programu mbalimbali za maendeleo nchini, aliongeza kusema mafanikio yaliyopatikana katika kuboresha maeneo hayo yameendelea kuwavutia wadau wa maendeleo kuwekeza na kusaidia katika sekta mbalimbali za maendeleo nchini. 

“Dunia imeendelea kushuhudia kazi nzuri inayoendelea kufanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi mahiri wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha hali ya Demokrasia na Utawala Bora nchini, hali hii imeendelea kuwavutia wadau wengi wa maendeleo kushirikiana na Tanzania; na Serikali ya Tanzania inaahidi kuendelea kushikiana na wadau wote katika kuondoa umaskini na kuboresha maisha ya Wananchi” ameeleza Dkt. Tax.

Kwa upande wake Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Bw. Milisic amepongeza juhudi zilizofanywa na Serikali ya Tanzania katika kuboresha hali ya Demokrasia na Utawala Bora nchini, huku akiahidi kuendelea kufanya kazi kwa ukaribu na Serikali kupitia nyanja mbalimbali ili kuendelea kuboresha hali ya maisha ya Wananchi.

Wakati huohuo Waziri Tax ameipongeza na kuishukuru Serikali ya Ireland kupitia Balozi wake nchini Mhe. O’Neil kwa kuendelea kufadhili programu na miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ya kuondoa umaskini kupitia TASAF. 

Kwa upande wake Balozi O’Neil ametoa pongezi na kueleza kuridhishwa kwake na namna Serikali ya Tanzania inavyojidhatiti katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijami kwa wananchi huku ikizingatia na kufuata misingi ya Utawala Bora, huku akitolea mfano usimamizi mzuri wa progamu na miradi ya kuondoa umaskini nchini kupitia TASAF. 

Kadhali Waziri Tax alitumia fursa hiyo kumweleza Balozi wa Ireland Mhe. O’Neill kuwa Serikali ya Tanzania inaendelea kuwakaribisha wawekezaji kutoka nchini Ireland kuwezekeza nchini katika sekta mbalimbali kama vile kilimo, viwanda na uchumi wa buluu. 

MKUTANO WA TANO WA BARAZA LA MAWAZIRI LA SEKTA YA UVUVI NA UKUZAJI VIUMBE MAJI WA EAC WAANZA KAMPALA, UGANDA


Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unafanyika jijini Kampala, Uganda tarehe 17-21 Aprili, 2023

Meza Kuu ikiongoza Mkutano wa Maafisa Waandamizi wakati wa Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijini Kampala, Uganda kuanzia tarehe 17-21 Aprili 2023 ikiongozwa na mwenyeji Uganda na Katibu wa Sekretarieti ya LVFO

Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijini Kampala, Uganda kuanzia tarehe 17-21 Aprili 2023
Ujumbe wa Jamhuri ya Kenya katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijini Kampala, Uganda kuanzia tarehe 17-21 Aprili 2023

Ujumbe wa Jamhuri ya Burundi katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijini Kampala, Uganda kuanzia tarehe 17-21 Aprili 2023
Ujumbe wa Jamhuri ya Uganda katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijini Kampala, Uganda kuanzia tarehe 17-21 Aprili 2023



Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unafanyika jijini Kampala, Uganda kuanzia tarehe 17-21 Aprili 2023.

Mkutano huo umeanza kwa kuwakutanisha Maafisa Waandamizi kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki za Burundi, Kenya, Tanzania na Uganda unafanyika tarehe 17 - 18 Aprili 2023. 

Mkutano huo utafuatiwa na Mkutano wa Makatibu Wakuu utakaofanyika tarehe 19 Aprili 2023 na Mkutano wa Mawaziri utakaofanyika tarehe 20 - 21 Aprili 2023.

Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kikao cha Maafisa Waandamizi unaongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Nazael Madalla. Aidha, ujumbe wa Tanzania unajumuisha ushiriki wa maafisa  kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania

Katika kikao hicho, maafisa waandamizi wanajadili na kuandaa nyaraka zitakazojadiliwa katika kikao cha Makatibu Wakuu kinachotarajiwa kufanyika tarehe 19 Aprili 2023 kitakachojadili taarifa nyingine na kupitia utekelezaji wa maamuzi/maagizo ya mikutano iliyopita na Utekelezaji wa Program na Miradi ya Uvuvi na Ukuzaji wa Viumbe maji katika Ziwa Victoria.

Ujumbe wa Tanzania katika Kikao cha Makatibu Wakuu unatarajiwa kuongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe na kujumuisha ushiriki wa Balozi wa Tanzania nchini Uganda Mhe. Dkt. Aziz Mlima ambaye atamuwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo.

Tarehe 20 - 21 Aprili 2023 kitafanyika kikao cha Baraza la Mawaziri ambacho pamoja na mambo mengine kitakamilisha Mkutano wa Nne ulioishia ngazi ya Makatibu Wakuu, kupitia, kujadili na kuridhia taarifa ya kikao cha Makatibu Wakuu itakayowasilishwa katika kikao hicho.

Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Kikao cha Mawaziri unatarajiwa kuongozwa na Naibu Waziri wa  Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa David Silinde.

 

 

      

 

 


Ujumbe wa Jamhuri ya Burundi katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijini Kampala, Uganda kuanzia tarehe 17-21 Aprili 2023

 

Ujumbe wa Jamhuri ya Uganda katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijini Kampala, Uganda kuanzia tarehe 17-21 Aprili 2023
 







Friday, April 14, 2023

MFUMO WA KIELEKRTONIKI WA KUSAJILI DIASPORA KUKAMILIKA MWEZI JUNI 2023 - BALOZI MBAROUK

 

 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipojibu swali la Mhe. Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Mikumi aliyetaka kujua idadi ya Diaspora wa Tanzania na mchango wao katika uchumi wa nchi


 

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inakamilisha mfumo wa Kidigitali wa uandikishaji wa Diaspora unaotarajiwa kukamilika mwezi June 2023 ili kuwezesha ukusanyaji endelevu wa takwimu za Diaspora.

 

Kauli hiyo imetolewa Bungeni jijini Dodoma tarehe 14 Aprili 2023 na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipojibu swali la Mhe. Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Mikumi aliyetaka kujua idadi ya Diaspora wa Tanzania na mchango wao katika uchumi wa nchi.

Mhe. Balozi Mbarouk amesema Diaspora kama walivyo raia wengine wa Tanzania wana mchango mkubwa kwa  uchumi wa nchi na maendeleo kwa ujumla kupitia shughuli mbalimbali wanazozifanya ikiwemo utumaji wa fedha za kigeni nchini (remittances), uwekezaji, kuleta mitaji, utaalam na teknolojia ambayo huchangia katika kukuza uzalishaji wa mazao, bidhaa na huduma mbalimbali zenye tija kiuchumi.

Ameongeza kuwa, Diaspora pia wanachangia uchumi wa nchi kwa kutangaza fursa za kiuchumi, biashara, utalii na uwekezaji zinazopatikana nchini na kwamba kwa mujibu wa taarifa kutoka Balozi za Tanzania na maeneo yake ya Uwakilishi, hadi sasa idadi ya Diaspora wa Tanzania ni Milioni 1.5.

Amesema katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la utumaji wa fedha za kigeni nchini kutoka kwa Diaspora hadi kufikia Shilingi Trilioni 2.6 mwezi Desemba 2022.

 

“Diaspora huchangia katika maendeleo ya nchi kwa kutuma fedha za kigeni nchini (Remittances); kuwekeza, kuleta mitaji, utaalamu na Teknolojia inayoweza kuchangia kukuza uzalishaji wa mazao, bidhaa na huduma mbalimbali zenye tija kiuchumi. Mathalan katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Desemba 2022, Diaspora walituma nchini kiasi cha Dola za Marekani Bilioni 1.1 sawa na Shilingi Trilioni 2.6. Vilevile, katika kipindi hicho Diaspora wamewekeza kupitia ununuzi wa nyumba na viwanja wenye thamani ya Shilingi Bilioni 4.4 na ununuzi wa Hisa zenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.5” amesema Balozi Mbarouk. 

 

DKT. TAX AKUTANA NA RAIS MSTAAFU WA MSUMBIJI

 




Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Msumbiji Mhe. Joaquim Chisano akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax aliyefika kumsalimia. Mhe Chisano yuko nchini kwa mwaliko wa kushiriki utoaji wa Tuzo za Taifa za Uandishi Bunifu za Mwl. Nyerere uliyofanyika  tarehe 13 Aprili, 2023.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akimsikiliza  Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Msumbiji Mhe. Joaquim Chisano walipokutana jijini Dar es Salam kwa mazungumzo. Mhe Chisano yuko nchini kwa  mwaliko wa kushiriki utoaji wa Tuzo za Taifa za Uandishi Bunifu za Mwl. Nyerere uliyofanyika  tarehe 13 Aprili, 2023.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akimsikiliza  Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Msumbiji Mhe. Joaquim Chisano walipokutana jijini Dar es Salam kwa mazungumzo. Mhe Chisano yuko nchini kwa  mwaliko wa kushiriki utoaji wa Tuzo za Taifa za Uandishi Bunifu za Mwl. Nyerere uliyofanyika  tarehe 13 Aprili, 2023.
mazungumzo yakiendelea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Msumbiji Mhe. Joaquim Chisano walipokutana jijini Dar es Salam kwa mazungumzo.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax amekutana na kuzungumza na Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Joaquim Chisano jijini Dar es Salam.

Mhe.Dkt. amemshukuru Mhe. Chisano kwa kukubali mwaliko wa kuja kushiriki utoaji wa Tuzo za Taifa za Uandishi Bunifu za Mwl. Nyerere zilizofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 13 Aprili, 2023.

“Mhe. Chisano naomba nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kitendo cha kukubali kuja nchini na kuwa mgeni rasmi katika utoaji wa tuzo uliofanyika jana, tunakushukuru sana na karibu tena Tanzania,” alisema Dkt Tax.

Amesema kitendo hicho kinaonesha uhusiano wa kidugu na wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na Msumbiji na pia kunaongeza jitihada za kuitangaza lugha ya Kiswahili katika bara la Afrika na Duniani kwa ujumla