Monday, August 28, 2023

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI NAMIBIA WASHIRIKI MAONESHO YA MWAKA YA KIBIASHARA YA ONGWEDIVA

Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania nchini Namibia, Bi. Upendo Mwasha (kushoto) akimwonesha mteja vazi aina ya batiki kutoka Tanzania wakati wa Maonesho ya Mwaka ya Kibiashara ya Ongwediva ambayo yanafanyika nchini humo kuanzia tarehe 27 Agosti, 2023. Maonesho hayo ambayo yalifunguliwa rasmi na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara wa Namibia, Mhe. Verna Sinimbo yamewashirikisha Wajasiriamali kutoka Tanzania na Diaspora wanaoishi nchini Namibia. Mbali na kuonesha bidhaa mbalimbali za Tanzania, Ubalozi  umetumia maonesho hayo kutangaza Lugha ya Kiswahili kwa kuweka vitabu vya kiswahili katika Banda la Ubalozi na kuhamasisha wateja kusoma na kujifunza Lugha hiyo kupitia Ubalozi ambao umeanzisha Maktaba ya Kiswahili.  
Wadau mbalimbali wakitembelea Banda la Tanzania kwenye maonesho hayo

Baadhi ya Wajasiriamali wa Tanzania wakishiriki maonesho ya Mwaka ya Kibiashara ya Ongwediva yanayofayika nchini Namibia

Banda la Tanzania kama linavyoonekana pichani. Bidhaa mbalimbali kutoka Tanzania zinazooneshwa kwenye maonesho hayo ikiwa ni pamoja na nguo za batiki, vikapu, viatu vya asili, shanga, kahawa na majani ya chai.



Sunday, August 27, 2023

DKT. TAX AWAPA WAKUU WA MIKOA MBINU ZA KUTEKELEZA DIPLOMASIA YA UCHUMI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amewapa Wakuu wa Mikoa mbinu mbalimbali za kutekeleza Diplomasia ya Uchumi katika Mikoa yao.

Dkt. Tax ametoa mbinu hizo tarehe 26 Agosti, 2023 wakati wa Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kibaha mkoani Pwani.

“Mbinu za kuibua na kutekeleza diplomasia ya uchumi ni nyingi kama vile kufungua balozi, kukusanya taarifa na uchambuzi, majadiliano,……………….lakini kwenu nyie Wakuu wa Mikoa mnaweza kufanya makongamano ya biashara na uwekezaji na kuzitangaza fursa mbailmbali za biashara katika mikoa yenu pamoja na elimu kwa Umma,” alisema Dkt. Tax.

“Kupitia mikoa yenu mnaweza mkafanya makongamano ya biashara na uwekezaji na kuzitangaza fursa za biashara katika mikoa yenu, ninyi ni wadau wakubwa wa kutekeleza diplomasia ya uchumi kwa vitendo na kuchangia maendeleo,” alisema Dkt. Tax

Alisema kuwa Serikali itaendelea kuboresha  mifumo ya sheiria, kiutendaji na kukuza mazingira ya kushindana Kimataifa na Ofisi za Wakuu wa Mikoa zina mchango mkubwa kufanikisha utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi na hivyo kuchangia maendeleo ya kiuchumi nchini.

“Serikali itaendelea kuboresha mifumo ya kisheria, kiutendaji na kukuza mazingira wezeshi kushindana kimataifa ambapo ofisi za wakuu wa Mikoa zina nafasi na mchango mkubwa wa kufanikisha utekelezaji wa Diplomasia ya uchumi, na kuchangia kasi ya maendeleo nchini,” alisema Dkt. Tax. 

Waziri Tax aliongeza kuwa Wakuu wa Mikoa ni wadau wakubwa katika kutekeleza diplomasia ya uchumi kwenye mikoa yao kwani huibua fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji zinazopatikana katika mikoa yao.

Pamoja na mambo mengine Waziri Tax aliongeza kuwa ofisi za Wakuu wa Mikoa ni wadau muhimu na wanalo jukumu la kibua fursa katika maeneo yao kama Mamlaka za msingi zinazobuni mipango ya biashara, miradi ya uwekezaji, uzalishaji, na utumiaji wa rasilimali katika ngazi ya mikoa.

Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere, Kibaha mkoani Pwani yalianza tarehe 21 – 28 Agosti, 2023.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwaeleza Wakuu wa Mikoa (hawapo pichani) mbinu za kutekeleza Diplomasia ya Uchumi katika mikoa yao.  Dkt. Tax ametoa mbinu hizo tarehe 26 Agosti, 2023 wakati wa Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kibaha mkoani Pwani.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwaeleza Wakuu wa Mikoa (hawapo pichani) mbinu za kutekeleza Diplomasia ya Uchumi katika mikoa yao.  Dkt. Tax ametoa mbinu hizo tarehe 26 Agosti, 2023 wakati wa Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kibaha mkoani Pwani.



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwaeleza Wakuu wa Mikoa mbinu za kutekeleza Diplomasia ya Uchumi katika mikoa yao.  Dkt. Tax ametoa mbinu hizo tarehe 26 Agosti, 2023 wakati wa Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kibaha mkoani Pwani.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwaeleza Wakuu wa Mikoa mbinu za kutekeleza Diplomasia ya Uchumi katika mikoa yao.  Dkt. Tax ametoa mbinu hizo tarehe 26 Agosti, 2023 wakati wa Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kibaha mkoani Pwani.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwaeleza Wakuu wa Mikoa mbinu za kutekeleza Diplomasia ya Uchumi katika mikoa yao.  Dkt. Tax ametoa mbinu hizo tarehe 26 Agosti, 2023 wakati wa Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kibaha mkoani Pwani.

Sehemu ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa wakifuatilia mafunzo katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kibaha mkoani Pwani



Wednesday, August 23, 2023

TANZANIA NA CUBA KUIMARISHA MISINGI YA KISIASA

Tanzania na Cuba zimekubaliana kushirikiana na kuimarisha misingi ya kisiasa, ujengaji wa uwezo kwa wanasiasa vijana, sekta za elimu, afya, utalii, biashara na uwekezaji 

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.) alipokutana na kuzungumza na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Yordenis Despaigne Vera katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

“Tanzania imekuwa ikishirikiana na Cuba kwa muda mrefu na ushirikiano baina ya mataifa haya umekuwa imara tangu ulipooasisiwa na viongozi wakuu wa Mataifa hayo Hayati Fidel Castro na Hayati Baba wa Taifa  Mwalimu Julius Kambarage Nyerere,” alisema Balozi Mbarouk.

Balozi Mbarouk ameongeza kuwa kwa sasa Cuba imeonesha dhamira ya kushirikiana Tanzania katika kuimarisha misingi ya siasa, kuwajengea uwezo wanasiasa vijana pamoja na sekta nyingine kama vile elimu, afya, na utalii pamoja na kuimarisha ushirikiano kwenye sekta ya biashara na uwekezaji 

Kwa upande wake Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Yordenis Despaigne Vera amesema kwamba Cuba inajivunia kuwa na uhusiano imara na Tanzania kwa takribani miaka 60. 

Cuba itaendelea kushirikiana na Tanzania kuimarisha misingi ya kisiasa kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili. “Wakati umefika sasa kwa serikali zetu mbili (Cuba na Tanzania) kuimarisha ushirikiano wake kisiasa na kuhakikisha kuwa mataifa yetu yanakuwa na misingi imara ya kisiasa, kijamii, na kiuchumi pia kwa manufaa ya pande zote mbili,” alisema Balozi Vera.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Yordenis Despaigne Vera walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Yordenis Despaigne Vera walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Yordenis Despaigne Vera baada ya kumaliza mazungumzo yao  katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Yordenis Despaigne Vera pamoja na maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Ubalozi wa Cuba



Tuesday, August 22, 2023

TANZANIA, INDONESIA KUIMARISHA USHIRIKIANO

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Indonesia zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta za biashara na uwekezaji, viwanda, kilimo, nishati, madini, mafuta na gesi pamoja na uchumi wa buluu. 

Makubaliano hayo yamefikiwa wakati wa hafla ya utiaji Saini wa Hati mbalimbali za makubaliano ya ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Indonesia iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mheshimiwa Joko Widodo.

Hati za makubaliano (MoUs) zilizosainiwa ni saba ambazo ni uanzishwaji wa Tume ya Pamoja ya Kudumu (JPC), msamaha wa visa kwa wamiliki wa hati za kusafiria za Kidiplomasia, Huduma za Afya, nishati, mafuta na gesi mapoja na madini. 

Mara baada ya kusainiwa kwa Hati hizo za makubaliano, Marais wote wawili waliongea na vyombo vya Habari ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia alisema kuwa chimbuko la uhusiano kati ya Tanzania na Indonesia ni Mkutano wa Bandung uliofanyika mwaka 1955 ambapo nchi nyingi za Afrika na Asia zilikuwa katika utawala wa kikoloni kwa kipindi hicho. 

“Tanzania na Indonesia zina uhusiano wa muda mrefu na wa kihistoria. Uhusiano huo uliasisiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Rais wa Kwanza wa Indonesia Mheshimiwa Soekarno. Uhusiano wa kidiplomasia ulianza mwaka 1964, ambapo Indonesia ilifungua Ubalozi wake nchini mwaka 1964 na kuwa miongoni mwa nchi za mwanzo kabisa kufungua Ubalozi wake nchini miaka michache baada ya uhuru,” alisema Rais Samia.

Rais Dkt. Samia ameongeza kuwa Tanzania na Indonesia zimekubaliana kukuza biashara na uwekezaji kwa kuzileta pamoja sekta za umma na binafsi ili kuimarisha ushirikiano katika sekta za biashara na uwekezaji, viwanda, kilimo, nishati, madini, mafuta na gesi, uvuvi na utalii pamoja na uchumi wa buluu.

Kadhalika, Mhe. Rais Samia amesema majadiliano baina yake na mgeni wake pamoja na mambo mengine, wamebainisha nia ya Tanzania kupata uzoefu wa uzalishaji mafuta ya mawese kutoka kwa Indonesia ambapo imekuwa mzalishaji mkubwa zaidi wa mafuta ya mawese duniani.

Kwa upande wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Mheshimiwa Joko Widodo amesema kuwa Indonesia itaendelea kushirikiana na Tanzania na kuhakikisha uhusiano wa kidiplomasia uliopo baina ya mataifa hayo unazidi kuimarika zaidi.

“Indonesia itaendelea kushirikiana na Tanzania katika sekta mbalimbali hususan sekta ya afya ambapo tumekusudia kuanzisha kiwanda cha dawa na vifaa tiba nchini Tanzania kwa maslahi ya pande zote,” alisema Mhe. Widodo

Rais Widodo ameongeza kuwa Indonesia imekubaliana na Tanzania katika kuboresha kilimo na kukifanya kuwa cha kisasa na chenye tija. “Indonesia itaendelea kuboresha Kituo cha Mafunzo ya Kilimo kwa Wakulima Vijijini (FARTC) kilichopo Mkindo – Morogoro na kuwawezesha wakulima wengi nchini Tanzania kulima kisasa zaidi,” aliongeza Rais Widodo.

Rais Widodo aliwasili nchini tarehe 21 Agosti 2023 kwa ziara ya Kitaifa ya siku mbili na amehitimisha ziara yake leo tarehe 22 Agosti 2023 na kureje Indonesia.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) Ikulu Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Mhe. Joko Widodo akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) Ikulu Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (kulia) pamoja na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Mhe. Joko Widodo (kushoto) wakizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) Ikulu Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Indonesia, Mhe. Retno Marsudi wakisaini Hati za Makubaliano (MoUs) kati ya Tanzania na Indonesia. Kati ya MoUs saba zilizosainiwa viongozi hao wawili wamesaini Hati za uanzishwaji wa Tume ya Pamoja ya Kudumu (JPC), msamaha wa visa kwa wamiliki wa hati za kusafiria za Kidiplomasia pamoja Huduma za Afya.




Monday, August 21, 2023

RAIS WA INDONESIA AWASILI NCHINI

Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Mheshimiwa Joko Widodo amewasili nchini kwa ziara ya Kitaifa ya siku mbili kuanzia tarehe 21 – 22 Agosti, 2023.

Ni majira ya saa 4:40 alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb).

Viongozi wengine walioshiriki mapokezi ya Mheshimiwa Widodo ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Balozi wa Tanzania nchini Indonesia, Mhe. Macocha Tembele, Balozi wa Indonesia nchini, Mhe. Tri Yogo Jatmiko pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.



Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Mheshimiwa Joko Widodo akipokelewa na Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya Kitaifa ya siku mbili tarehe 21 - 22 Agosti, 2023






DKT. TAX AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA COMORO

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini, Mhe. Dkt. Ahamada El Badaoui Mohamed katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 

Viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano ikiwemo maandalizi ya Mkutano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika sekta za kipaumbele hususan bishara na uwekezaji, afya, uchukuzi, elimu, utamaduni, uchumi wa buluu na maeneo mengine.

“Tanzania itaendelea kushirikiana Comoro ili kuendeleza ushirikiano uliodumu kwa kipindi kirefu kwa maslahi ya pande zote mbili hususan katika sekta za biashara na uwekezaji,” amesema Dkt. Tax 

Kwa upande wake Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini, Mhe. Dkt. Ahamada El Badaoui Mohamed amesema kwamba Comoro inajivunia kuwa na uhusiano imara na Tanzania ambapo uhusiano huo umekuwa imara na umedumu kwa muda mrefu. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisalimiana na Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini, Mhe. Dkt. Ahamada El Badaoui Mohamed katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini, Mhe. Dkt. Ahamada El Badaoui Mohamed akimueleza jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini, Mhe. Dkt. Ahamada El Badaoui Mohamed katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini, Mhe. Dkt. Ahamada El Badaoui Mohamed katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini, Mhe. Dkt. Ahamada El Badaoui Mohamed katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni Maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na watumishi wa Ubalozi wa Comoro. 



RAIS WA INDONESIA KUANZA ZIARA YA KIKAZI LEO NCHINI

Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mheshimiwa Joko Widodo anatarajia kuanza ziara ya Kitaifa ya siku mbili nchini Tanzania kuanzia tarehe 21 hadi 22 Agosti 2023

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ziara hiyo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amesema ziara hiyo ni matokeo ya kazi kubwa anayoifanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na mataifa mengine.

 “Ziara ya Mheshimiwa Widodo itakuwa ni ziara ya pili kwa kiongozi wa taifa hilo kutembelea nchini. Ziara ya kwanza ilifanywa na Mheshimiwa Soeharto, Rais wa Pili wa Indonesia mwaka 1991, ikiwa ni miaka 32 iliyopita,” alisema Dkt. Tax. 

“Mheshimiwa Rais Widodo atawasili Leo tarehe 21 Agosti 2023 na atapokelewa rasmi na Mwenyeji wake, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 22 Agosti, 2023, Ikulu Jijini Dar es Salaam,” aliongeza Waziri Tax.

Waziri Tax ameongeza kuwa, baada ya mapokezi viongozi hao watakuwa na mazungumzo ya faragha na baadaye mazungumzo rasmi na kufuatiwa na hafla ya utiaji saini Hati za Makubaliano ya Ushirikiano kwenye sekta mbalimbali.

“Tanzania na Indonesia zina uhusiano wa muda mrefu na wa kihistoria. Uhusiano huo uliasisiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Rais wa Kwanza wa Indonesia Mheshimiwa Soekarno. Uhusiano wa kidiplomasia ulianza mwaka 1964, ambapo mwaka huohuo Indonesia ilifungua Ubalozi wake nchini na kuwa miongoni mwa nchi za mwanzo kabisa kufungua Ubalozi wake nchini miaka michache baada ya uhuru. Aidha, Tanzania ilifungua Ubalozi wake nchini Indonesia Agosti, 2022, na kuzinduliwa rasmi mwezi Juni 2023,” aliongeza Dkt. Tax 

Pamoja na mambo mengine, Dkt. Tax amesema kuwa Tanzania na Indonesia zimekuwa zikishirikiana katika sekta za Uwekezaji ambapo hadi kufikia mwaka 2023, Indonesia imewekeza nchini miradi ipatayo mitano (5) katika sekta za Kilimo, uzalishaji wa viwandani, ujenzi. 

Sekta nyingine za ushirikiano ni pamoja na kilimo ambapo mwaka 1996 Indonesia ilianzisha Kituo cha Mafunzo ya Kilimo kwa Wakulima Vijijini (Farmers’ Agriculture and Rural Training Centre-FARTC), kilichopo Mikindo mkoani Morogoro. Kituo hicho kimekuwa kikitoa mafunzo mbalimbali kwa wakulima. 

“Ziara hii inatarajiwa kuimarisha ushirikiano katika sekta mbalimbali kama itakavyoonekana katika Hati za Makubaliano zitakazosainiwa, na matokeo ya mazungumzo kati ya Viongozi wetu yatakayojikita katika diplomasia, biashara, kilimo, uvuvi, elimu, nishati, madini, uchumi wa buluu na uhamiaji,” alisema Dkt. Tax.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dk. Stergomena Tax akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam kuhusu ziara ya Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mheshimiwa Joko Widodo anayetarajia kuanza ziara ya Kitaifa ya siku mbili nchini Tanzania kuanzia tarehe 21 - 22 Agosti 2023

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dk. Stergomena Tax akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam kuhusu ziara ya Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mheshimiwa Joko Widodo anayetarajia kuanza ziara ya Kitaifa ya siku mbili nchini Tanzania kuanzia tarehe 21 - 22 Agosti 2023. wwengine pichaani (kulia) ni Balozi wa Tanzania nchini Indonesia, Mhe. Balozi Macocha Tembele, (kushoto) ni Balozi wa Tanzania nchini Namibia, Mhe. Balozi Ceaser Waitara.







Sunday, August 20, 2023

BALOZI SHELUKINDO AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NJE YA INDONESIA

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo amekutana kwa mazungumzo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Indonesia Bw. Cecep Herawan katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam

Pamoja na Mambo mengine, mazungumzo ya viongozi hao yamejikita katika kujadili masuala ya ushirikiano baina ya Tanzania na Indonesia katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara na uwekezaji, kilimo, afya, elimu na nishati.

Balozi Shelukindo amemhakikishia Katibu Mkuu huyo ushirikiano wa dhati katika kuendelea kuimarisha uhusiano wa muda mrefu na na Indonesia. Aidha,  amemueleza kwamba mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ni mazuri na salama na kuwasihi wawekezaji kutoka Indonesia kuchangamkia fursa zilizopo.

Naye, Bw. Herawan amepongeza uhusiano imara uliopo baina ya serikali hizi mbili (Tanzania na Indonesia) na kuongeza kuwa Indonesia itaendelea kushirikina na Tanzania katika sekta mbalimbali kwa maslahi ya nchi zote mbili.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Indonesia, Bw. Cecep Herawan katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Indonesia, Bw. Cecep Herawan katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Indonesia, Bw. Cecep Herawan (aliyevaa miwani kushoto) akizungumza wakati wa kikao chake na mwenyeji wake Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo (katikati kulia) akimsikilza Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Indonesia, Bw. Cecep Herawan wakati wa mazungumzo yao katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mazungumza baina ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Indonesia, Bw. Cecep Herawan yakiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam




Thursday, August 17, 2023

BALOZI WA TANZANIA NCHINI UMOJA WA FALME ZA KIARABU(UAE) AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mhe. Lt. Jen. (Mst) Yacoub Hassan Mohamed akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Mhe. Sheikh Mohammed Bin Zayed Al Nahyan katika Ikulu ya nchi hiyo (Qasr Al Watan) iliyopo mjini Abu Dhabi.


==============================================

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mhe. Lt. Jen. (Mst) Yacoub Hassan Mohamed mapema wiki hii amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Mhe. Sheikh Mohammed Bin Zayed Al Nahyan katika Ikulu ya nchi hiyo (Qasr Al Watan) iliyopo mjini Abu Dhabi.

Viongozi hao pia walipata wasaa wa mazungumzo ambapo Mheshimiwa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu alimhakikishia Mhe. Mohamed ushirikiano wa Serikali yake katika kutekeleza majukumu yake nchini UAE kwa manufaa ya pande zote mbili hususan kiuchumi.

Kwa upande wa Balozi Mohamed alimuahidi Mheshimiwa Rais kuwa atahakikisha Watanzania na Waemirati wananufaika na fursa za uchumi zilizopo pande zote mbili.

Tanzania na UAE zina fursa nyingi za kushirikiana kiuchumi hususan katika sekta za nishati ambayo UAE ni miongoni mwa nchi tajiri katika uzalishaji wa mafuta. Kadhalika Tanzania ina eneo kubwa la kilimo hivyo ina soko kubwa la bidhaa za Kilimo na Mifugo ambapo ushirikiano huo utawezesha uzalishaji wa kisasa na kuongeza thamani ya bidhaa.

Bidhaa zenye soko kubwa kwa Tanzania nchini UAE ni pamoja na mbogamboga, matunda, nyama, korosho, karafuu, chai, karanga, asali, samaki na kahawa. Hivyo Ubalozi unaendelea na jitihada za kuwashawishi wawekezaji wa UAE kuja kushirikiana na Watanzania kuwekeza kwenye sekta ambazo zitatoa ajira kwa Watanzania wengi na zenye soko kubwa UAE kwa manufaa ya pande zote mbili.

Pamoja na Umoja wa Falme za Kiarabu ubalozi huo pia unawakilisha nchi za Bahrain, Pakistan na Iran. 

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mhe. Lt. Jen. (Mst) Yacoub Hassan Mohamed akiteta na Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Mhe. Sheikh Mohammed Bin Zayed Al Nahyan katika Ikulu ya nchi hiyo (Qasr Al Watan) iliyopo mjini Abu Dhabi.

Picha ya pamoja.

 

Monday, August 14, 2023

SADC YAJADILI UMUHIMU WA RASILIMALI WATU NA FEDHA KATIKA MAENDELEO YA VIWANDA





Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stegomena Tax (Mb) akifuatilia hotuba za ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambao ni maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo utakaofanyika Luanda, Angola tarehe 17 Agosti 2023.

Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa SADC aliyemaliza muda wake ambaye ni Waziri wa Ushirikiano wa Kikanda wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mhe. Antipas Nyamwisi akikabidhi uenyekiti wa baraza hilo kwa Waziri wa Uhusiano wa Nje wa Angola, Mhe. Téte António 

Waheshimiwa Mawaziri wa SADC wakiendelea na mkutano wao ikiwa ni maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo utakaofanyika Luanda, Angola tarehe 17 Agosti 2023

Saturday, August 12, 2023

DKT. KIKWETE AHIMIZA AMANI KATIKA NCHI ZA SADC

 
Rais Mstaafu wa Awamu ya NNne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwasilisha mada kuhusu Amani na Usalama kama msingi wa kufikia maendeleo ya kweli katika nchi za Kusini mwa Afrika. Mada hiyo iliwasilishwa kwenye Chuo cha Diplomasia cha Angola ikiwa ni moja ya matukio ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaofanyika Luanda, Angola kuanzia tarehe 08 hadi 17 Agosti 2023. Wengine katika picha ni Waziri Mkuu Mstaafu wa Msumbiji, Mhe. Luisa Diogo (kulia) na Katibu Mtendaji wa Zamani wa SADC, Mhe. Tomaz Salomão 

Wahuriki wakisikiliza mada kuhusu Amani na Usalama kama msingi wa kufikia maendeleo ya kweli katika nchi za Kusini mwa Afrika iliyokuwa ikiwasilishwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya NNne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye Chuo cha Diplomasia cha Angola ikiwa ni moja ya matukio ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaofanyika Luanda, Angola kuanzia tarehe 08 hadi 17 Agosti 2023

Washiriki wakisikiliza mada

Rais Mstaafu wa Awamu ya NNne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (mwenye tai nyekundu) akiwa na ujumbe wa Tanzania ulioshiriki katika Mhadhara wa Umma ambao aliwasilisha mada kuhusu Amani na Usalama kama msingi wa kufikia maendeleo ya kweli katika nchi za Kusini mwa Afrika