Wednesday, January 29, 2014

Mhe. Membe kumwakilisha Mhe. Rais Kikwete Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa AU

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bbernard K. Membe (Mb) akiwa katika moja ya vikao vya Baraza la Mawaziri wa Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa. Mhe. Membe atamwakilisha Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika unaofanyika kuanzia tarehe 30 hadi 31 Januari, 2014 mjini hapa.

==========================


WAZIRI MEMBE KUMWAKILISHA MHE. RAIS KIKWETE MKUTANO WA WAKUU WA NCHI WA AU ADDIS ABABA.

Na Mwandishi wetu, Addis Ababa

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) atamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye Mkutano wa 22 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) unaotarajiwa kuanza kesho Alhamisi tarehe 30 Januari, 2014 mjini Addis Ababa, Ethiopia.

Mkutano huo ulitanguliwa na Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa AU uliofanyika tarehe 27 na 28 Januari, 2014 ambao Mhe. Membe aliongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo.

Kaulimbiu ya Mkutano wa mwaka huu ni “Kilimo na Usalama wa Chakula” unalenga kuweka mikakati madhubuti katika kuhakikisha kilimo kinakuwa mkombozi wa watu Barani Afrika kwa kuwainua kiuchumi na kuondokana na wasiwasi wa njaa unaolikabili Bara hili mara kwa mara.

Mkutano wa Wakuu wa nchi pia utapokea Ripoti mbalimbali ikiwemo ile ya Kamati ya Kimataifa ya Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (CAHOSCC) iliyokuwa chini ya Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mkutano huo wa Wakuu wa Nchi na Serikali unatarajiwa kumalizika tarehe 31 Januari, 2013.

-Mwisho-




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.