Wednesday, January 22, 2014

Naibu Waziri akutana na Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda wa Afrika Kusini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akizungumza wakati wa kikao chake na Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda wa Afrika Kusini, Mhe. Elizabeth Thabethe (wa pili kushoto). Mhe. Thabete anaongoza ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Afrika Kusini utakaoshiriki Semina kuhusu Biashara na Uwekezaji itakayofanyika hapa nchini tarehe 23 Januari, 2014. Wengine katika picha ni Mhe. Radhia Msuya (kushoto), Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini na Mhe. Thanduyise Chiliza, Balozi wa Afrika Kusini hapa nchini.
Mama Hellen Rwegasira (wa pili kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa kikao kati ya Mhe. Maalim na Mhe. Thabethe (hawapo pichani)
Wajumbe wengine kutoka Afrika Kusini na Tanzania wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Maalim na Mhe. Thabete (hawapo pichani). Kulia ni Bw. Adam Isara, Msaidizi wa Mhe. Maalim.
Mhe. Maalim akiagana na Mhe. Thabete mara baada ya mazungumzo yao.
Picha ya pamoja.






No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.