Tuesday, January 28, 2014

Tanzania na Algeria kudumisha ushirikiano

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria, Mhe. Ramtane Lamamra (hayupo pichani) walipokutana pembezoni mwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Umoja wa Afrika (AU) unaoendelea mjini Addis Ababa. Mazungumzo hayo yalihusu ushirikiano kati ya Algeria na Tanzania katika masuala mbalimbali ikiwemo sekta ya gesi na umeme. Wengine katika picha ni Balozi Vincent Kibwana (kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Togolani Mavura, Msaidizi wa Waziri na Bi. Zuleikha Tambwe, Afisa Mambo ya Nje.
Mhe. Lamamra naye akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yao.
Mhe. Membe akiagana na Mhe. Lamamra mara baada ya mazungumzo yao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.