Friday, January 31, 2014

Mhe. Membe akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mhe. Ahmed Davutoglu walipokutana Mjini Addis Ababa kwa mazungumzo kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Uturuki. Mhe. Membe yupo Addis Ababa akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika kuanzia tarehe 30 hadi 31 Januari, 2014.
Mhe. Membe (katikati) akiwa na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa, Mhe. Balozi Tuvako Manongi (kushoto) pamoja na Bw. Togolani Mavura, Msaidizi wa Waziri wakati wa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki (hayupo pichani)
Mhe. Membe (kushoto) akimsikiliza Mhe. Davutoglu (wa pili kulia) wakati wa mazungumzo yao.
Mhe. Membe akifurahia jambo na Mhe. Davotoglu huku akiondoka baada ya mazungumzo yao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.