Wednesday, January 29, 2014

Waziri Mkuu wa Finland ahutubia Wadau wa Maendeleo

Waziri Mkuu wa Finland akitoa mada katika kikao maaulum kilichofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro. Kikao hicho kilijadili mbinu ambazo nchi za Afrika na Ulaya zikishirikiana kwa pamoja, zinaweza kuzitumia kukuza uchumi kwa faida ya wananchi wao. Katika mada yake Waziri Mkuu alisisitiza umuhimu wa kuimarisha Jumuiya za Kikanda kwa ajili ya kuleta maendeleo ya kiuchumi na utulivu wa kisiasa. Wazungumzaji wengine walisisitiza umuhimu wa Afrika na Ulaya kuwa na ushirikiano wenye uwiano sawa ambao utaleta maendeleo ya kiuchumi kwa pande zote mbili bila kudhulumiana. 





Wadau wakijadili fursa na changamoto za maendeleo katika nchi za Afrika na Ulaya.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule wa pili kushoto akisikiliza kwa makini michango mbalimbali kuhusu kuboresha ushirikiano wa kiuchumi baina ya nchi za Afrika na Ulaya.


Mjumbe akichangia mada.












No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.