Wednesday, January 29, 2014

Waziri Mkuu wa Findland awasili Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku mbili

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Peter Pinda (Mb), mwenye tai nyekundu akiongozana na Waziri Mkuu wa Findland, Mhe. Jyrki Katainen ambaye amewasili nchini Tanzania usiku wa tarehe 29 Januari, 2014 kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.


Waziri Mkuu wa Findland, Mhe. Jyrki Katainen wa kwanza kushoto akipeana mkono na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere alipowasili kwa ziara ya kikazi. Anayeangalia kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Mohammed Mzale.


Mhe. Katainen akiendelea kusalimiana na viongozi waliojitokeza katika Uwanja wa Ndege kwa ajili ya kumlaki. Katika picha hii, Mhe. Waziri Mkuu anasalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Dora Msechu.

Salamu zinaendelea, Bibi Victoria Mwakasege, Mkurugenzi Msaidizi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa naye akisalimiana na Waziri Mkuu wa Findland

Mhe. Mizengo Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyeketi kulia akibadilishana mawazo na mgeni wake Waziri Mkuu wa Findland alipowasili nchini usiku wa tarehe 29 Januari, 2014

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.