Wednesday, January 29, 2014

Hafla ya Mapokezi Rasmi ya Waziri Mkuu wa Finland, Ikulu Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete aliyeketi kulia na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Sadik Meck Sadik wakijadili jambo wakati wakiwa wanamsubiri Waziri Mkuu wa Findland, Mhe. Jyrki Katainen kuwasili Ikulu, Dar es Salaam.

Rais Kikwete (kulia) akiongozana na Mgeni wake, Waziri Mkuu wa Findland kuelekea katika jukwaa maalum kwa ajili ya kupigiwa Nyimbo za Taifa na Mizinga 19 ya kumkaribisha rasmi Mhe. Waziri Mkuu nchini Tanzania. 

Rais Kikwete (kulia) na Mgeni wake, Waziri Mkuu wa Findland wakifurahia jambo huku wakielekea kwenye jukwaa maalum.

Rais Kikwete (kulia) pamoja na Mgeni wake, Waziri Mkuu wa Findland wakiwa wamesimama huku Nyimbo za Taifa za Mataifa yao zikiwa zinapigwa.


Mizinga 19 ikipigwa kwa ajili ya heshima ya Waziri Mkuu wa Findland.

Waziri Mkuu wa Findland anakagua gwaride.

Waziri Mkuu wa Findland akiwapungia viongozi na watu wengeine wakati alipokuwa anaingia Ikulu, Dar es Salaam.

Mazungumzo Rasmi


Rais Kikwete akitambulisha ujumbe wake kwa Waziri Mkuu wa Findland hayupo pichani kabla ya kuanza mazungumzo rasmi Ikulu, Dar es Salaam.

Ujumbe wa Rais Kikwete katika mazungumzo rasmi, kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb).

Wajumbe wengine.

Ujumbe wa Tanzania (kulia) pamoja na ule wa Finland katika mazungumzo rasmi Ikulu, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.