Friday, January 31, 2014

Tanzania na Colombia zajidili namna ya kuboresha ushirikiano wa kiuchumi.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Balozi Rajabu Gamaha (kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Asia, Afrika na Oceania kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Colombia, Bibi Sandra Salamanca. katika kikao hicho, viongozi hao walijadili namna Tanzania na Colombia zitakavyoweza kushirikiana ili kutumia fursa zinazopatikana katika nchi hizo kwa madhumuni ya kuinua kipato cha wananchi wao.


Bibi Salamanca (kulia) akisisitiza jambo huku Balozi wa Colombia nchini Tanzania mwenye makao yake Nairobi, Kenya Mhe. Maria Lugenia Correa akisikiliza kwa makini.

Mkurugenzi wa Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dora Msechu akifafanua jambo katika kikao hicho huku Bw. Graison Ishengoma, Afisa Mambo ya Nje akinukuu masuala muhimu ya mazungumzo. 



Picha ya pamoja, wa tatu kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu ambapo kulia kwake ni Mratibu wa Masuala ya Afrika, Mashariki ya Kati na Asia ya Kati kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Colombia, Balozi Betty Escorcia.



Picha na Reginald Philip Kisaka.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.