Tuesday, January 21, 2014

Mhe. Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Oman nchini



Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Oman hapa nchini Mhe.Soud Ali Bin Mohamed Al Ruqaishi. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 21 Januari, 2014.

Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Balozi Ruqaishi Mhe. Mahadhi Juma Maalim, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Balozi Ruqaishi, Balozi Simba Yahya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Mhe. Rais Kikwete katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Ruqaishi (wa pili kushoto) na Maafisa waliofuatana na Balozi huyo.

Mhe. Rais Kikwete akiwa katika mazungumzo na Balozi Ruqaishi mara baada ya kupokea hati zake za utambulisho.


Mhe. Mahadhi (wa kwanza kushoto),  Balozi Yahya (wa pili kushoto) na Maafisa Waandamizi katika Ofisi ya Rais wakifuatilia mazungungumzo ya Mhe. Rais na Balozi Ruqaishi (hawapo pichani)

Maafisa wakinukuu mazungumzo ya Mhe. Rais Kikwete na Balozi Ruqaishi (hawapo pichani). Kutoka kulia ni Dkt. Laurean Ndumbaro, Msaidizi wa Rais katika masuala ya Siasa, Bw. Muhidin Michuzi, Mwandishi wa Habari Msaidizi wa Rais na Bw. Abbas Mngwali, Afisa Mambo ya Nje.

Balozi Ruqaishi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.

Balozi Ruqaishi (katikati) akisikiliza wimbo wa Taifa lake uliokuwa ukipigwa na Bendi ya Polisi kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu. Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Maharage Juma na Mnikulu, Bw. Shaaban Gurumo.

Kikosi cha Bendi ya Polisi kikiwa kazini.

Balozi Ruqaishi akimshukuru Kiongozi wa Bendi ya Polisi.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.