Thursday, February 4, 2016

Kaimu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Balozi wa India kuhusu kudhalilishwa kwa Mtanzania nchini India

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi (kulia) akizungumza na Balozi wa India hapa nchini, Mhe. Sandeep Arya alipomwita Wizarani kufuatia taarifa za kushambuliwa na kudhalilishwa kwa mwanafunzi wa kike kutoka Tanzania na kundi la watu nchini India. Katika mazungumzo yao Balozi Mwinyi alisema Serikali ya Tanzania imesikitishwa  na inalaani vikali kitendo hicho. Pia alimtaka kufikisha ujumbe kwa Serikali yake ya kuchukua hatua kali kwa wote watakaopatikana na hatia ya tukio hilo na kuwahakikishia ulinzi Watanzania waliopo nchini India.Mazungumzo yalifanyika tarehe 04 Februari, 2016.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga kwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mwinyi na Balozi Arya (hawapo pichani)
Mazungumzo yakiendelea.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.