Thursday, February 4, 2016

Balozi Mwinyi akutana na Katibu Mtendaji wa ALAT

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Ramadhani Mwinyi akiwa katika mazungumzo na Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa Tanzania (Association of Local Authorities of Tanzania-ALAT), Bw. Abraham Shamumoyo. Katika mazungumzo hayo, Bw. Shamumoyo alitoa taarifa fupi kuhusu muundo na utendaji kazi wa ALAT. Aidha, Bw. Shamumoyo alitoa taarifa za awali kuwa Jumuiya hiyo kwa upande wa Kanda ya Mashariki mwa Afrika inakusudia kutuma maombi Serikalini ili makao makuu yake yawe Tanzania.
Mazungumzo yakiaendelea, wengine katika picha, kutoka kulia ni Bw. Elisha Suku na Balozi Baraka Luvanda ambao ni maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje. Pembeni kwa Bw. Shamumoyo ni maafisa wa ALAT.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.