Friday, February 19, 2016

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje azungumza na Mkurugenzi wa Shirika la Trade Mark East Africa

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa
Dkt. Susan Kolimba (Mb.) akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la "Trade Mark East Africa", Bw. David Stanton aliyekuja kujitambulisha na kuutambulisha mradi wa maendeleo wa awamu ya pili wa Shirika hilo pamoja na kumweleza Mhe. Naibu Waziri mafanikio ya mradi wa awamu ya kwanza uliokwishamalizika kwa mwaka wa fedha 2015/2016.


Mkurugenzi wa Miundombinu katika Ushoroba wa Kati (central corridor) katika Bandari ya Dar es salaam Bw. Severine Kaombwe (kushoto), pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la "Trade Mark East Africa" wakishiriki katika mazungumzo hayo.
Shirika la "Trade Mark East Africa" ni shirika lisilo la kiserikali ambalo limekuwa likifanya kazi na Serikali ya Tanzania katika miradi ya kuendeleza na kuboresha Bandari ya Dar es Salaam, pamoja na miundombinu katika maeneo ya mipakani ili kuwezesha kukuza shughuli  za kiuchumi na kuongeza ajira kwa wananchi.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bi. Graceana  Shirima akiwa na maafisa wa Wizara wakifuatilia mazungumzo ya viongozi hao na Mhe. Naibu Waziri.
Mhe. Naibu Waziri Kolimba akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa East Africa Trade Mark  pamoja na Wakurugenzi aliofuatana nao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.