Monday, February 1, 2016

Kampuni Binafsi za Tanzania zashiriki Maenesho ya Utalii nchini Uholanzi


Mhe. Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Irene Kasyanju akiwa katika ya pamoja na Bi. Selma Kamm-Melai (kulia) na Bw. Yohannes Ngomi- Kamm (wa pili kutoka kulia) Wawakilishi wa Kampuni ya Utalii ya MAKASA SAFARIS iliyopo Moshi, Tanzania walioshiriki katika Maonesho ya Utalii ya Holiday Fair 2016 (Vakatiebeurs 2016) yaliyofanyika hivi karibuni mjini Utrecht.  Kushoto ni Bi. Agnes Kiama Tengia, Afisa Ubalozi.

Baadhi ya Makampuni binafsi ya Utalii nchini Tanzania yalishiriki katika Maonesho hayo maarufu yanayofanyika kila mwaka katika miji ya Amsterdam, Utrecht na Maastricht, Uholanzi ambapo huvutia maelfu ya washiriki kutoka nchi mbalimbali duniani. Maonesho ya Vakantiebeurs hutoa fursa kwa nchi kujitangaza hususan katika sekta ya utalii. Ubalozi wa Tanzania ulihudhuria Maonesho hayo na kukutana na Wawakilishi wa baadhi ya Makampuni hayo binafsi kutoka Tanzania.


Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Uholanzi wakiwa katika picha ya pamoja na Bw. Kassim Abdallah, Mwakilishi wa Kampuni ya BOBBY TOURS kutoka Arusha Tanzania aliyeshiriki katika Maonesho ya Vakantiebeurs 2016 yaliyofanyika katika miji ya Amsterdam na Utrecht, Uholanzi hivi karibuni. Kutoka kulia ni Bi. Flora Williams, Bw. Peter Mihyona Bi. Agnes K. Tengia.


Mhe. Balozi Irene F.Kasyanju akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa Kampuni ya KILIDOVE ya Arusha, Tanzania walioshiriki katika Maonesho ya Vakatiebeurs 2016 yaliyofanyika mjini Utrecht hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.