Thursday, January 28, 2016

Naibu Katibu Mkuu akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Comoro nchini

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Balozi Ramadhani Mwinyi Muombwa akutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Comoro nchini, Mhe. Ahmed El Badaoui Mohamed Fakih. Mazungumzo hayo yalijikita katika kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na Comoro.  
Maafisa wa Ubalozi wa Commoro nao wakifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Balozi Fakih na Balozi Muombwa (hawapo pichani), wa kwanza kutoka kulia ni Naibu Balozi Bw. Bacar Salim na kulia ni Afisa Mwandamizi wa Ubalozi huo Bw. Failladhu Mbae Charif.
Balozi Fakih naye akimwelezea jambo Balozi Muombwa (Kulia) wakati wa mazungumzo yao.

Picha na Reginald Philip



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.