Thursday, January 14, 2016

Waziri Mahiga akutana kwa mazungumzo na Rais wa Mahakama ya Afrika

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (kulia), akimsikiliza Rais wa Mahakama ya Afrika  Jaji Mstaafu, Mhe. Augustino Ramadhani alipofika kumtembelea ofisini kwake kwa ajili ya kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa Waziri. Pia kuzungumzia masuala mbalimbali yanayoihusu Mahakama hiyo likiwemo suala la ujenzi wa Mahakama hiyo katika Jiji la Arusha.
Waziri Mahiga naye akieleza jambo ambapo alimpongeza Mhe. Ramadhani kwa juhudi anazozifanya kwenye Mahakama hiyo.

Afisa Mambo ya Nje, Bw. Elisha Suku naye akielezea jambo katika mazungumzo kati ya Waziri Dkt. Mahiga na Mhe. Ramadhani (hawapo pichani), wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Baraka Luvanda, na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Wizarani, Bi. Mindi Kasiga. 
Mazungumzo yakiendelea
Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.