Tuesday, January 5, 2016

Mhe. Rais Magufuli apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea hapa nchini, Mhe. Song Geum-young. Hafla hiyo fupi ilifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 05 Januari, 2016.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (wa kwanza kulia) akiongoza ujumbe wa Wizara kwenye hafla ya uwasilishwaji wa Hati za Utambulisho zilizofanyika Ikulu. Wengine ni Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki ( wa pili kulia), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga (wa pili kushoto) na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Khatib Makenga
Mhe. Rais Magufuli akimtambulisha kwa Balozi Song Geum-young Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (Mb.).
Mhe. Rais akizungumza na Balozi Song Geum-young
Balozi Song Geum-young akisaini Kitabu cha wageni alipowasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho
Picha ya Juu: Balozi wa Jamhuri ya Korea hapa nchini Mhe. Song Geum-young akisikiliza wimbo wa taifa uliopigwa na Bendi ya Polisi (picha ya chini) wakati alipowasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais. Wengine katika picha ni Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohammed Juma Maharage na Mnikulu.

Balozi Song Geum-young akiagana na kiongozi wa Bendi ya Polisi

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.