Monday, January 11, 2016

Naibu Waziri awataka Vijana kuiwakilisha vizuri Tanzania wanapopata fursa za kwenda nje ya nchi

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (Mb.) akikabidhi Bendera ya Taifa kwa Vijana 12 wa Kitanzania  kutoka Mpango utakaohusisha safari ya meli (the Ship for  World Youth Program) kuzunguka nchi nne Barani Asia ambazo ni India, Sri Lanka, Singapore na Japan kwa lengo la kujadili masuala ya kijamii pamoja na mitazamo mbalimbali kuhusu mwingiliano wa tamaduni pamoja na kuangalia fursa miongoni mwa nchi mbalimbali. Mpango huo ulioandaliwa na Serikali ya Japan unatarajia kuanza tarehe 13 Januari hadi 02 Machi, 2016. 
Mhe. Dkt. Kolimba akizungumza na vijana hao (hawapo pichani) kuhusu ziara yao na kuwataka kuiwakilisha vizuri Tanzania na kuwa mfano miongoni mwa vijana kutoka nchi nyingine zitakazoshiriki mpango huo. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Aziz Ponary Mlima na kushoto ni Balozi wa Japan hapa nchini, Mhe. Masaharu Yoshida.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki akiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Wizarani hapo, Bi. Mindi Kasiga wakimsikiliza Naibu Waziri (hayupo pichani) alipozungumza na vijana 12 watakaoiwakilisha Tanzania kwenye mpango wa safari ya meli kuzunguka nchi nne Barani Asia.
Sehemu ya Vijana hao
Baadhi ya vijana hao 12
Balozi Yoshida nae akizungumza na vijana hao (hawapo pichani)
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Masahriki, Kikanda na Kimataifa, Bi. Eva Ng'itu na Bw. Emmanuel Luangisa wakimsikiliza Balozi Yoshida hayupo pichani
Mkutano ukiendelea

Sehemu nyingine ya viajana.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.