Thursday, January 21, 2016

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje akutana na Kaimu Balozi wa Nigeria nchini.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Ramadhani Mwinyi Muombwa (kulia) akizungumza na Kaimu Balozi wa Nigeria hapa nchini, Mhe. Salisu Umaru baada ya Balozi huyo kumtembelea Ofisini kwake kwa mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizi mbili.
Mazungumzo yakiendelea huku Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga, Pamoja na Afisa wa Wizara hiyo Bw. Elisha Suku wakifuatilia kwa makini mazungumzo hayo.

Naibu Katibu Mkuu akifurahia jambo na Kaimu Balozi wa Nigeria hapa nchini wakati wa mazungumzo yao.
 Naibu Katibu Mkuu, Balozi Muombwa na Kaimu Balozi Umaru wakibadilishana kadi za mawasiliano  baada ya mazungumzo yao.
===================
PICHA NA REUBEN MCHOME

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.