Tuesday, January 5, 2016

Mhe. Rais Magufuli apokea Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Palestina nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Palestina hapa nchini, Mhe. Hazem Shabat. Hafla hiyo fupi ilifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 05 Januari, 2016.
Mhe. Rais Magufuli akimtambulisha kwa Balozi Shabat Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (Mb.).
Mhe. Balozi Shabat akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya  Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bw. Batholomeo Jungu.
Mhe. Rais Magufuli akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi Shabat
Mhe. Rais Magufuli akiwa kwenye mazungumzo na Balozi Shabat mara baada ya kupokea Hati zake za Utambulisho
Mazungumzo yakiendelea
Balozi Shabat akisaini Kitabu cha wageni alipowasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho
Balozi Shabat (katikati) akisikiliza wimbo wa taifa lake ulipopigwa na Bendi ya Polisi kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho. Kushto kwake ni Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohammed Juma Maharage na kulia kwake ni Mnikulu.
Mkurugenzi Msaidizi katika Idara ya Itifaki, Bw. James Bwana akifuatilia wimbo wa Taifa
Balozi Shabat akiagana na Kiongozi wa Bendi ya Polisi.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.