Monday, January 18, 2016

Balozi Mlima akutana na Kaimu Balozi wa China

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Aziz Ponary Mlima (kulia) akisalimiana na Kaimu Balozi wa China nchini Tanzania, Mhe. Zhang Biao wakati wawili hao walipokutana kwa ajili ya kufanya mazungumzo Ofisini kwa Katibu Mkuu.
Balozi Mlima akiwa katika mazungumzo na Kaimu Balozi wa China, Mhe. Zhang. Katika mazungumzo hayo, wawili hao waliahidi kuwa nchi zao zitaendelea kushirikiana na kuungana mkono katika masuala mbalimbali ya kimataifa.
Maafisa kutoka Ubalozi wa China uliopo hapa nchini wakifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Balozi Mlima na Mhe. Zhang Biao (hawapo pichani).
Balozi Mlima akimsikiliza Kaimu Balozi wa China, Mhe. Biao
Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa wakinukuu mambo muhimu yaliyojitokeza katika Mazungumzo kati ya Balozi Mlima na Mhe. Biao (hawapo pichani).
Mazungumzo yakiendelea
Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.