Tuesday, January 5, 2016

Mhe. Rais Magufuli apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa EU nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) hapa nchini, Mhe. Roeland Van De Geer. Hafla hiyo fupi ilifanyika Ikulu, Jijini Dar es Salaam tarehe 05 Januari, 2016.
 
Mhe. Rais Magufuli akimtambulisha kwa Balozi Roeland Van De Geer,  Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (Mb.).
Mhe. Balozi Roeland Van De Geer akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga
Mhe. Balozi Roeland Van De Geer akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Mona Mahecha
Mhe. Balozi Roeland Van De Geer akisalimiana na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Anthony Mtafya.
Mhe. Rais Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Roeland Van De Geer
Mhe. Rais akizungumza na Balozi Roeland Van De Geer mara baada ya kupokea Hati zake za Utambulisho

Mhe. Rais akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Van De Geer, Mhe. Dkt. Kolimba, Msaidizi wa Rais masuala ya Diplomasia, Bi. Zuhura Bundala (wa kwanza kulia)  pamoja na wajumbe kutoka Ubalozi wa EU.
Balozi Roeland Van De Geer akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu
Balozi Roeland Van De Geer akisikiliza wimbo wa taifa wa Tanzania na EU kutoka Bendi ya Polisi ikiwa ni kwa  heshima yake
Mhe. Balozi Roeland Van De Geer akiagana na Kiongozi wa Bendi ya Polisi

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.