Wednesday, January 13, 2016

Waziri Mahiga ashiriki Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono wananchi walioshiriki katika kilele cha Sherehe za Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kutimia miaka 52 katika Uwanja wa Amaan Studium leo akiwa katika gari maalum.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Ali Mohamed Shein akikagua gwaride la Vikosi vya Ulinzi lililoandaliwa rasmi katika kilele cha sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,zilizofanyika leo katika Uwanja wa Amaan Studium Mjini Unguja.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe. Susan Kolimba (kushoto), na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mhe. Sophia Simba wakifuatilia matukio wakati wa maadhimisho ya miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Rais Shen akiwapungia mkono vijana waliokuwa wakipita mbele yake (hawapo pichani).
Vijana wa Chama cha Mapinduzi wakibeba Picha la Marehemu Rais wa Kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Karume wakati wa Maandamano ya kusherehehekea Kilele cha Mapinduzi Kutimia miaka 52 leo katika uwanja wa Amaan Studium Mjini Unguja.  
Rais Shen akiwahutubia wananchi wa Zanzibar wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 52  
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Afrika Mashariki, Kikanda na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi (katikati juu), akiwa pamoja na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakati wa maadhimisho ya miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar.  
Sehemu ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa maadhimisho ya miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiteta na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli wakati wa kilele cha sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,zilizofanyika leo katika Uwanja wa Amaan Studium Mjini Unguja. 
Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (mwenye tai nyekundu) akifurahia jambo na na Waziri wa Mambo ya Nje Afrika Mashariki, Kikanda na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mwenye Tai Nyeusi yenye mistari meupe), pamoja na Mama Salma Kikwete (mwenye kilemba kichwani).
Waziri Mahiga (katikati) akisalimiana na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mohammed Othmani Chande (wa kwanza kushoto), wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Afrika Mashariki, Kikanda na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Silima Haji Kombo.
Waziri Mahiga (katikati) akizungumza jambo na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (kushoto) mara baada ya kumalizika kwa Sherehe za maadhimisho ya miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar, kulia ni Balozi Silima Haji Kombo 
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (kushoto)  akisalimiana na Balozi Silima


Picha na Reginad Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.