Tuesday, January 26, 2016

Dkt. Mlima akutana na Katibu Mkuu wa EAC

Katibu Mkuu wa Sekretariati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Richard Sezibera (kushoto) akutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Dkt. Aziz P. Mlima. Dkt. Sezibera alikutana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje kwa madhumuni ya kusalimia pamoja na kutoa taarifa fupi ya masuala mbalimbali yanayoendelea katika Jumuiya.
Kutoka kushoto ni Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ambao ni Mkurugenzi wa Siasa, Ulinzi na Usalama, Bw. Stephen Mbundi; Mhandisi John Kiswaga; Bw. Amos Tengu na Bw. Antony Ishengoma wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.