Friday, February 26, 2016

Waziri Mahiga aongoza maadhimisho ya Siku ya Taifa la Kuwait

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki Kikanda na Kimataifa, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), akizungumza katika hafla  ya kusheherekea Siku ya Taifa la Kuwait iliyofanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es Salaam tarehe 25 Februari, 2016. Kushoto ni Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al Najem. Katika hotuba yake Waziri Mahiga alilipongeza Taifa la Kuwait kwa kuendeleza mahusiano mazuri kati yake na Tanzania  katika sekta mbalimbali zikiwemo za biashara, kilimo na maj.
Waziri akiendelea kuhutubia
Balozi Al Najem naye akizungumza katika hafla hiyo.


Sehemu ya Mabalozi na viongozi mbalimbali kutoka Serikalini wakisikiliza hotuba  zilizotolewa na Mhe.Dkt. Mahiga na Mhe. Al Najem (hawapo pichani). 
Waziri Mahiga (kulia) akisalimiana na Rais Mstaafu Mhe. Ali Hassan Mwinyi ambaye alihudhuria hafla hiyo.
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa iliyokuwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Mhe. Mwinyi.   
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na  Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al Najem.
Waziri Mahiga  kwa pamoja na Balozi Al Najem na Mabalozi wengine  wakishiriki kukata keki kama ishara ya kuadhimisha wakati wa hafla hiyo. Anayeshhudia pembeni ni Rais Mstaafu Mhe.Mwinyi. 
Picha ya pamoja

Picha na Reginald Philip 



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.