Friday, February 5, 2016

Balozi Haule akutana na Mkurugenzi wa Mashariki mwa Afrika wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa.

Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. John Haule (kushoto) akizungumza na Mkurugenzi wa Mashariki mwa Afrika wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Udhibiti wa Madawa ya Kulevya na Uhalifu, Bw. Jose Vila De-Castillo, alipotembelea Ubalozini, Jijini Nairobi, jana.
Katika mazungumzo yao, Bw. De-Castillo aliomba Ubalozi uwe kiungo kati ya Taasisi yake na Serikali ya Tanzania. Taasisi hiyo inaendesha mpango wa miaka mitano wa udhibiti wa rushwa, mitandao ya uhalifu, biashara na matumizi ya madawa ya kulevya, ujangili na biashara ya binadamu kwa nchi za Tanzania, Burundi,Comoro, 
Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Madagascar, Mauritius, Rwanda, Seychelles na Somalia. Kulia ni Ofisa wa Ubalozi, Bw. Mussa Haji.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.