Friday, February 26, 2016

Waziri Mahiga arudisha Fomu Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga  akiwasili katika Jengo la Sukari "Sukari House" zilipo Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ili kuweza kukabidhi Fomu za Uadilifu na Tamko la Mali kwa Viongozi kama taratibu za Maadili ya Utumishi wa Umma zinavyowataka viongozi wote wa Umma kukamilisha zoezi hilo mara baada ya kuingia madarakani.
Waandishi wa Habari wakimuhoji Mhe. Waziri Mahiga mara baada ya kuwasili katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, ambapo Mhe. Waziri Mahiga alieleza kuwa ujazaji wa fomu hizo ni taratibu za kawaida za kiutumishi na kwa upande wake ameshawahi kujaza fomu hizo mara kadhaa katika Utumishi wake hivyo kwa sasa anahuisha taarifa zake.
Waziri Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Charles Kitwanga walipokutana katika Ofisi za Sekretarieti ya Uongozi wa Maadili ya Umma katika zoezi la kukabidhi fomu za Uadilifu na Tamko la Mali, kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga.




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.