Wednesday, March 2, 2016

Mkurugenzi Mkuu Msaidizi wa UNESCO kwa upande wa Afrika atembelea Wizara ya Mambo ya Nje

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu Msaidizi wa UNESCO kwa upande wa Afrika, Bw. Firmin Matoko walipokutana kwa ajili ya mazungumzo kwenye Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje.


Balozi Mushy akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu Msaidizi wa UNESCO kwa upande wa Afrika, Bw. Firmin Matoko. Mazungumzo hayo pamoja na Mambo mengine yalijikita katika vipaumbele vya UNESCO ambavyo ni elimu na jinisia. Kwa upande wa elimu, Balozi Mushy alieleza hatua ya Serikali ya awamu ya tano kutoa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari. Kuhusu jinsia, alieleza hatua ya Serikali ya kujumuisha wanawake katika nafasi za uongozi ikiwa ni pamoja na kuimchagua Makamu wa Rais Mwanamke wa kwanza. Mwingine katika picha ni Mwakilishi wa UNESCO nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues.

Wajumbe wakiendelea na mazungumzo


Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Ngusekela Nyerere na Afisa wa UNESCO wakinukuu mambo muhimu ya mazungumzo.


Balozi Mushy akisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa Bw. Matoko.


Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.