Wednesday, March 9, 2016

Rais wa Vietnam afungua Kongamano la Pili la Biashara kati ya Tanzania na Vietnam.


 Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan San kwa pamoja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kassim wakiwa meza kuu kabla ya kufungua rasmi  Kongamano la Pili la Biashara kati ya Tanzania na Vietnam lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam

 Rais wa Vietnam,  Mhe. Truong Tan Sang akifungua rasmi Kongamano la Pili la Biashara kati ya Tanzania na Vietnam  ambapo alieleza  nia ya wazi ya Serikali yake ya kushirikiana na Tanzania katika sekta ya Teknolojia, Kilimo na biashara ili  kuzidi kuimarisha uhusiano.
Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa akiwasilisha mada katika Kongamano hilo ambapo alieleza kuwa uhusiano wa Tanzania na Vietnam ni mzuri hivyo ni vema sasa wananchi wa nchi zote mbili wakatumia fursa hiyo katika kuwekeza katika biashara na viwanda ili kukuza uchumi.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles John Mwijage akitoa mada ambapo alieleza fursa za uwekezaji zilizopo nchini Tanzania  na akawakaribisha wafanyabiashara wa Vietnam kuja kuwekeza nchini Tanzania.
Mwenyekiti wa Wafanyabiashara nchini, Mhe. Regnald Mengi akiwasilisha mada katika Kongamano hilo ambapo alieleza kuwa wafanyabiashara nchini Tanzania wapo tayari kushirikiana na wafanyabiashara wa nchini Vietnam.
Washiriki wa kongamano wakifuatilia ufunguzi wa kongamano hilo.


Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki akifuatilia ufunguzi Kongamano hilo.


Mkataba wa Makubaliano ya  Ushirikianmo katika masuala ya Uwekezaji kati ya Tanzania na Vietnam ukisainiwa
Mhe. Rais Truong na Mhe. Majaliwa katika picha ya pamoja na Mawaziri na Viongozi kutoka sekta mbalimbali
Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.